Sasa tuhamasike, kuwa na akaunti za Benki ni rahisi. Miamala ya simu gharama hazivumiliki

Sasa tuhamasike, kuwa na akaunti za Benki ni rahisi. Miamala ya simu gharama hazivumiliki

Bora wachaji kwa kilometa mtu ukiona vp unapanda boda unapeleka.
 
Daktari wa binadamu na tahama wapi na wapi! Utawala pekee anaojua ni kusimamia wagonjwa, na mgonjwa hana kauli. Akiambiwa vua nguo, hana swali.
Hivi hiyo wizara kazi zao za kila siku nini?? Je wana idara huko mikoani? Nawaza kwa kina sipat jibu,
 
Asee naona Serikali imeanza ku discourage watu kutumia mobile money, hii ni hatari sana
 
Yaani kuwa na simu Sasa ni shida mno, bando halishikiki, miamala ya kinyonyaji, bado wanataka na pesa ukiweka vocha, duh
 
Sasa ni wakati wa benki kujitanua zaidi na kila mmoja ajitahidi kuwa na akaunti ya benki, japo na wao wana makato Ila haya ya simu ni makubwa mno, yaani kusafirisha milioni wanakata 31,000 kutuma na kutoa.

Sasa nitahamia Benki, au nitasafirisha pesa kwa Gari yaani basi, pia tujitahidi kujiunga internet banking ambayo ukienda cafe nusu saa 500 unafanya muhamala kwa Bei rahisi.

Gari pia nauza siwezi kununua mafuta.

Kwa nini ufanye internet banking internet cafe wakati upo kwenye ulimwengu ambao smartphone zinapatikana hata kwa laki moja?
 
Kwani kwenye benki kutoa ni bure? Hivi ukitingwa inahitaji kuhamasika? Kuwa serious we jamaa
 
wakuu suala la kodi ni suala muhimu lakini lafaa kufanywa katika namna ambayo ni win win situation. Ukipandisha mafuta utapelekea kutokea kwa mfumuko wa bei hili wala halihitaji a rocket science degree kuling'amua. Suala la kuongeza tozo kwenye makato ya katika kuweka na kutoa pesa pia ni another rubish stanza, huwezi kuwa kikwazo cha ukuaji wa teknolojia au unataka watu waanza kutunza pesa majumbani? watu waanze kusafiri kwenda kutuma pesa benki iliyo zaidi ya km 200?
 
Hatoshi yeye au waziri wa fedha.
Nadhani waziri hana mbinu zisizoumiza.
Wabunge in ndiooooooo kila kitu.walikuwa wanauwezo kumpinga waziri

Twende tu,mdogomdogo
 
Yaan apa cha kufanya ni alie mbali ni kutuma namba ya wakala tu.. haya mambo ya nimtumie pesa nikatwe parefu atoe pesa akatwe parefu sio dili aseee..
 
Ila isiwe benki ya NMB maana wana makato ya kipumbavu sana! utasikia wamekata kwa ajili ya REA
 
Inaumiza sana.tutakuwa tunapeana pesa mkono kwa mkono maana haya ni maumivu makubwa sana.pesa hakuna mtaani alafu iingie hyo mkate pakubwa hvyo.hapana kabisa.
Sahizi kama mtu yuko jirani apande pikipiki tu afate hela!
 
Internet bank ni nafuu kweli ila kwa benki kama CRDB hawataki kabisaa watu wajiunge na hiyo huduma kwakuwa inawakosesha mapato, niliomba hiyo huduma kwa mara ya kwanza, nilijibiwa baada ya miezi 6 kupita. Mfumo wao ukazingua, nikaenda wa-reset password tu, nikakalishwa kwenye foleni siku nzima, ikapita miezi 6 tena, kwenda kuulizia tena, wakanipa fomu nijaze upya, kimbembe kikawa kwenye sahihi, wanasema haifanani na niliyosaini miaka 10 nyuma, kuwa kuna tofauti kidogo hivyo hawawezi kunipa hiyo huduma mpaka nipige sahihi kama ile.

Nikaona sio kesi, nitakapofikia maamuzi, i will kiss them good bye
duhh,

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
You send a mil kulipa 16,000 kwanini msikie uchungu namna hii?
*security
*confidential
*right time cash shift and collection
** fanyeni ya hovyo muwape ulaji majambazi.
Kuwa na cash ni jambo moja kuihamisha kwa usalama ni jambo lingine.
N.b;- yupo jamaa yangu aliwahi kujifanya bahili sana siku fulani alipata million 5 kwa ubahaili wake hata kukodi tax ni hasara akatembea nazo,yaliyomtikea liibiwa hela zote kwa ujinga wa kutochukuwa hata tax ya 30,000/-
kazi ya kukuamishia fedha pia iheshimiwe
 
Benki pia ni gharama na ina usumbufu fulani, account mantainace fee kila mwezi 10000 to 20000, atm muamala 1000 to 1500, kupada boda utafute Atm kwanza ziko mbali sana, bora kupunguza miamala esio ya lazima tu.
Bank gani account maintenance ni 10,000?
 
Yeye kama waziri wa technojia ni lazima apitie mambo yote ya mawasiliano kwa ivo hii inamhusu kwa kiasi kikubwa!! Au lawama ziende kwa nani mkuu?
Hili halikupangwa kweli na wizara ya fedha katika kutafuta vyanzo vya mapato ya serikali?

Yeye Ndugulile anahusika pale, ambapo alipeleka mapendekezo ya serikali kutoza kodi katika Youtube channels na Blogs wakati, si mali za serikali!
 
wacheni upumbavu kuchangia kodi kwa Taifa lako sio dhambi bali ni fahari, fedha unayo katwa ndio inayo enda kusaidia kuweka miundo mbinu ya elimu mizuri, afya n.k ambayo watoto wetu ndugu zetu watanufaika nayo, yeyote anaye jaribu kukwepa au kuhamasisha kukwepa huyo sio mtanzania atakuwa ana nchi nyingine.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom