SATIVA adhibitiwe kwa matusi ya nguoni anayotoa mitandaoni

Yuko sawa kabisa, ungekuwa ni wewe umekoswa kuuliwa na waliofanya hivyo wapo mtaani wanafurahia maisha usingeleta huu upuuzi hapa.

Umewahi kuandika popote waliotaka kumtoa uhai wachukuliwe hatua? Basi Kaa kwa kutulia
 
Hayupo nchini kafichwa na mariah sarungi nairobi!
 
utovu wa nidhamu wa aina hiyo tena kwa kijana kama huyo, hautavumiliwa na jamii hata kidogo. Atapoteza huruma aliyoivuna kabla

namshauri ajiepushe na utovu wa nidhamu wa aina zote mara moja. akumbuke kwamba kutukana sio ujasiri au ushupavu.🐒
 
...mwenye hofu ya Mungu na mcha Mungu na aliyepata malezi mazuri ya wazazi wake hawezi kutukana wala kutoa iwe hadharani au mafichoni.
Ingawa siungi mkono matusi, lakini mbona hukosoi watesi wa Sativa, yaani watekaji na wauaji, na husemi polisi wadhibiti hao wahalifu?

Au huyo mungu wako anaruhusu kuteka na kuua watu?!

Hivi kati ya matusi kwa upande mmoja na utekaji/mauaji kwa upande mwingine ni kipi kina madhara zaidi?
 
Inawezekana na wewe kama ungepelewa kuzimu na kurudi ukiwa hai ungekuwa unawatukana kupita Sativa wale waliokupeleka kuzimu. Umekalia makalio yako unafikiri aliyopitia ni kama kubarizi mbungani?
 
Sikubaliani na lugha za matusi pasipo kuangalia nani anazitoa lakini hata wewe kuna watu wengi hawakubaliani na unachokifanya. Kiufupi maxcence akisema watu wakupigie kura za kukupa ban, hutochukua lisaa utapewa life time ban kwa hiyo tumia nguvu na akili hiyo hiyo kujisahihisha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…