Ni sahihi ; ila baadaye utafute uhalali wa ww kuendesha barabarani Vinginevyo utakamatwa na kuwajibishwa kwa mujibu wa sheria zilizopo.elewa kwamba leseni haikuondolei ujuzi wa kuendesha gari. Huo ni utaratibu usio na maana. Ukute kuna shida barabarani dereva mwenye leseni kapata shida mi nisio na leseni niache kuendesha gari kuwahisha abiria ili kutatua tatiza kwa dharura? Ujuzi kwanza
Usitoe hukumu kabla hujasikiliza Hoja(sababu) kutoka pande zote mbili husika i.e Madokta waathirika na SAUT.Hicho chuo wababe sanaaa,nimesoma hapo nawaelewa wanajifanyaga wakoloni
kwa hiyo walifutiwa wanahesabika ni debe tupu hakuna maarifa waliyonayo?Ni sahihi ; ila baadaye utafute uhalali wa ww kuendesha barabarani Vinginevyo utakamatwa na kuwajibishwa kwa mujibu wa sheria zilizopo.
Maarifa, ujuzi na Uzoefu kazini (Kwa waliopata ajira) wanavyo ila Nani atakayemdhamini mtu ambaye hana cheti cha kuthibitisha kuwa yy ni daktari? Kwa mfano Malawi wanataka kumwajiri mmojawapo (au hata zaidi ) wa hao waliofutiwa vyeti. Malawi watahitaji CV ikiambatanishwa na Vyeti. Hao madaktari watavitoa wapi? Je, hapa nchini ikitokea kunafanyika sensa ya madaktari walio kazini, wao siku ya tukio wataonesha vyeti gani? Rejea enzi za Uncle Magu na zoezi la kuhakiki vyeti vya Taaluma makazini. Yani Watumishi tuliwekwa kwenye tension kali.kwa hiyo walifutiwa wanahesabika ni debe tupu hakuna maarifa waliyonayo?
Unaweza kutoboa hapo kwa kufanya mtihani private candidate kwenye Centre utakayoona kwako itakuwia rahisi kuhudhuria. Ukifaulu mtihani huo cheti utapewa.Kwa kuwa jamii imejiwekea utambulisho huo na imezoeleka tutafuata tu utaratibu huo. Mi mwenyewe kuna kozi nilisoma na nina uwezo mkubwa wa kufanya kazi niliyoisomea muda mrefu na uzoefu ninao, kwa kuwa nilikosa cheti cha kunithibitisha kuwa nimesomea kazi hiyo ilibidi mfumo wa ajira uniteme bila kujali uwezo wangu mkubwa wa kumudu kazi hiyo. Kazi hiyo naiweza na naipenda ila mfumo hauwezi kunitambua na imebidi nifute kabisa maarifa hayo kichwani mwangu kwa kuwa hakuna mahali nitatambuliwa zaidi ya kufanywa kibarua tu kwa sababu maarifa yakiingia kichwani hayafutiki daima
Usiombe yakukute 🤔, ila SERIKALI inabidi ifanye maamuzi sahihi kuhusu ili swala ,
Chuo kikuu cha St. Augustine kimebatilisha shahada ilizotoa kwa madaktari 162 waliohitimu chuo cha udaktari cha St. Franscis kuanzia mwaka 2015-2019.
St. Augustine imechapisha tangazo kwenye gazeti la Daily news ikitoa notisi kubatilisha shahada za wanafunzi hao 162 ambao inadai wamegoma kurejesha nyaraka ya matokeo(Transcripts) ambazo walipewa bila baraza la senete la chuo kuwa na taarifa na kuziidhinisha.
Taarifa hiyo iliyosainiwa na mwenyekiti wa seneti ya chuo hicho, balozi Prof Costa Mahalu imesema maamuzi hayo yamefikiwa baada ya mkutano wa senet ilioketi mwezi wa pili.
===
Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino Tanzania (SAUT) kimewafutia shahada Madaktari 162 waliohitimu Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha St Francis (SFUCHAS) kuanzia mwaka 2015-2019.
Notisi kwa Umma iliyochapishwa katika Gazeti la Daily mnamo Jumatatu (27 Machi, 2023), ilisema wahitimu 162 walikataa kimakusudi kurudisha nakala za masomo, 'Transcript' walizopewa bila ufahamu na uidhinishaji wa seneti ya chuo kikuu licha ya kukumbushwa kwa muda mrefu.
Taarifa hiyo iliyotiwa saini na Mwenyekiti wa seneti ya SAUT Balozi Prof. Costa Mahalu inaeleza uamuzi wa kuondoa shahada hiyo umekuja baada ya kikao cha Seneti cha Chuo Kikuu kilichofanyika Februari mwaka huu.
"SAUT kupitia Seneti ya Chuo Kikuu katika Seneti yake ya 54 isiyo ya kawaida, mkutano uliofanyika tarehe 25 Februari 2023 katika chuo kikuu cha SAUT na kwa mujibu wa Kifungu cha 47(1) & (2) cha Sheria ya Vyuo Vikuu, Sheria Na. 7 ya 2005 ikisomwa pamoja na Vifungu. 6(3)(ii), 7,8 na Kanuni ya 29 (1) ya Mkataba wa SAUT GN. HAPANA. 580 ya 2020 ilifuta shahada walizopewa wahitimu 162 wa Madaktari wa Udaktari wa SFUCHAS kuanzia 2015 -2019,” inasomeka taarifa hiyo.
Source: Daily News
Hebu fikiria mtu yuko kikazi Mtwara na SAUT iko Mwanza. Gharama ya kurudisha hiyo transcript imekaaje au wanairudisha kwa mtindo gani?Mnaoshabikia hili kwamba hao madaktari wako sahihi anawadanganya, imekula kwao. Kwa nini nao kama kweli wamehitimu kihalali wasirudishe hizo transcripts? Ona sasa kilichowakuta! Niko upande wa Baraza la Seneti!
Yeah. Senet ya chuo inapaswa ioneshe kutenda na kufanya maamuzi kwa kuzingatia weledi mkubwa lakini pia kujiepusha na maamuzi yanayovuruga na kuathiri mustakabali mzima wa maisha ya Wahitimu wa chuo hicho. Inafaa Senet ione kwamba bila kuwepo kwa wanafunzi wanaosoma hapo chuoni, Senet hiyo haina sababu ya kuwepo hapo chuoni ni useless.Usiombe yakukute 🤔, ila SERIKALI inabidi ifanye maamuzi sahihi kuhusu ili swala ,
1. Kutengua aya maamuzi ya kukurupuka.
2. Kuiwajibisha hiyo seneti uchwara hususani bwana costa titch.
3. Chuo kiwe na utaratibu mzuri wa kutoa transcript kwa wahitimu.
Kuwa na heshima na shule za watu huyo Dr gwajima na Biteko wamekaa darasani heshima vyuo walivyosoma .Huo ni mwanzo tu, kuna PhD za kufutwa haraka iwesekanavyo.
1. Dr Abood
2. Dr musukuma
3. Dr Biteko
4. Dr. Gwajima Bishop
5. Dr Samia
6. Dr Hans M
6. Dr Jafo
Ongezeeni wengine
Daktaree tia neno kwa msaada wa wachache hapa JFKuna mambo ni magumu Sana natamani kuandika chochote hapa lakini sintoeleweka na wajuaji wa jamii forum bora nikae kimya aisee
BUGANDO wameshajitenga na SAUT muda sasaUspanic Mkuu Thread Iko wazi ni St Francis ni kampasi nafikiri hii itakuwa ya Ifakara kama Niko sawa.Ila Sauti Wana vyuo vingi Vya Udaktari kikiwemo Bugando.Niko tayari kurekebishwa.
Mkuu andika tu, tupo tutakao soma na kuongeza uelewa kupitia bandiko lako.Kuna mambo ni magumu Sana natamani kuandika chochote hapa lakini sintoeleweka na wajuaji wa jamii forum bora nikae kimya aisee
Asante Mkuu!Nafikiri kama ilivyo Mwenge Cha Moshi au Jordan.BUGANDO wameshajitenga na SAUT muda sasa