Sauti ya umauti masikioni mwangu

Sauti ya umauti masikioni mwangu

Habari ya usiku wana jf!

Leo ninayofuraha kuweka bando kwenye simu yangu baada ya siku nyingi bila kuweka bando!

Kwanini hiyo heading! Ipo hivi, mm kijana wa miaka 28.6, lakini nipo kama mtu mzima wa miaka 40. Sijaoa wala sina mtoto. Maisha nayoyaishi hiki kipindi sidhani kama Mungu ndiye aliyepanga niyaishi. Naishi maisha ya ovyo sanaa. Nimelelewa na mama tu na ndiye aliyenipambania hadi kupata haka kaelimu ka ovyo ambako hakana msaada na mm kabisa.

Ipo hivi, mwaka huu tangu uanze sina hamu nao tena maana ulikaribishwa kwa majanga ya kuanza kumwuguza mama yangu. Toka mwezi wa 11 hadi huu mwez wa tatu ndo bi mkubwa amerudishwa nyumbani. Nimempambania ili nisije kubaki na uchungu hapa duniani kama mama angefariki. Ningejiona sina maana kabisa ukizingatia mama aliza vitu vyake vyote ili anisomeshe mm akiamini nikipata ajira nitamtunza. Marehemu hasemwi vibaya ila utawala wa mwamba umeniharibia future yangu kwa 100%.

Tuachane huyo marehemu na utawala wake,. Baada ya mama kulazwa ilibidi nitoe hela yangu yote hadi hela iliyokuwa kwenye biashara nikatoa yote. Haikutosha ikabidi nianze kukopa hela kwa wakopeshaji wa mitaani maana walikuwa wananiamin kuwa nitawalipa maana nilikuwa nafanya biashara na wao wanaona. Nimeingiza deni kubwa sana saiz linasoma milion 6. Mimi sina ata mia mbovu, yan ata cha kuuza. Uwanja nilishauza muda. Sasa jana nimeambiwa na mmoja wa watu niliowakopa akaniambia "nitakudai kwa namna nyingine" hii kauli imenitisha sanaa, niliwaza nitakamatwa na police ila nahisi hapana ni uchawi utatumika na jana usiku nimelala vibaya sijui n wenge sijui ndo simu ya kifo yenyewe hiyo nilipigiwa ndotoni!

Mwisho mimi nina amani kuona nimemsaidia bi mkubwa. Lakini pia nina huzuni maana nahisi nakufa muda wowote na nawaza mama atasikiaje habari ya mimi kufa, nawaza mchumba niliyekaa nae miaka mitatu akinisubiri nimuoe atasikiaje habari ya mm kufariki. Kiufupi hicho ndo kinanitisha. Lakini acha iwe hivo tu maana sina uwezo wa kulipa hizo hela mimi.

Makala ni ndefu poleni ila nawaomba tuwapende mama zetu, usimtendee baya mama yeyote huendi ndiye mama yangu ambaye nitamwacha pekee yake hapa duniani bila uwepo wangu. Upendo ni amri kuu ya Mungu!
Ni mapito tu hayo wala usiwe na hofu tena cheka hizo shida zako kwa dharau kubwa kabisa.
 
Pole sanaa mkuu... lkn mbn kama changamotp yako ni ndogo... mimi nikkusimulia yangu , yako utaona ya mtoto kunywa uji tu.
 
Mchumba miaka mitatu mnasomea degree au oa ivo ivo bwaraka zije mazee ondoa vifungo ivo vya jini mahaba, afu we wa kiume inuka kafosi wenzio wanachoma adi mishikaki , we ukifa akuna anaejali jipambanie mtot wa kiume wenzio waliofeli wameachia marinda
 
Pole sana.
Hapo awali ulikua unafanya biashara ya aina Gani na mtaji ulikua kiasi Gani?

Hao wanaokudai hawawezi kukupa Wala kukudhuru, najua sio rahisi lakini ongea nao na waeleze Hali halisi.

Pambana upate mtaji kidogo kidogo utaanza kuwalipa na fursa zingine zitajifungua kadri unavyopambana.

Mtaji wa kwanza ulionao ni afya, Bado Dua na maombi ya Mama, pia Muumba wako hatakuacha ukiwa na juhudi kwenye mambo Yako na kutegemea yeye. Lakini hayo yote yanawezekana endapo tu hautakata tamaa, endelea kuwa na Imani na kikubwa elewa kwamba hizo Hali zinawapata wengi lakini Bado wanatumaini kwamba nyakati nzuri zipo mbele ya safari.

Ni hayo tu Kwa sasa
 
Pole sana jitahidi kuongea kwa kina na huyo aliyekuambia utamlipa kwa njia nyingine umueleze hali halisi, panga mipango yako upya na Mungu akusaidie.
 
Nashukuru kwa ushauri.
Pole sana.
Hapo awali ulikua unafanya biashara ya aina Gani na mtaji ulikua kiasi Gani?

Hao wanaokudai hawawezi kukupa Wala kukudhuru, najua sio rahisi lakini ongea nao na waeleze Hali halisi.

Pambana upate mtaji kidogo kidogo utaanza kuwalipa na fursa zingine zitajifungua kadri unavyopambana.

Mtaji wa kwanza ulionao ni afya, Bado Dua na maombi ya Mama, pia Muumba wako hatakuacha ukiwa na juhudi kwenye mambo Yako na kutegemea yeye. Lakini hayo yote yanawezekana endapo tu hautakata tamaa, endelea kuwa na Imani na kikubwa elewa kwamba hizo Hali zinawapata wengi lakini Bado wanatumaini kwamba nyakati nzuri zipo mbele ya safari.

Ni hayo tu Kwa sasa
 
Mkuu usijiue tu ila could ikifika automatic ... pambana
 
Hapo aliposema utanilipa kwa vingine, uingereza unaweza kuwa Butler 'bongo maana yake chawa' mpaka deni liishe.

Hebu afafanue kwanza huyo anayekudai ni namna gani anataka ulilipe hilo deni.
 
Pole sana Kaka. Usikate Tamaa, Bado una maana kubwa kwenye huu Ulimwengu. Pambana, Piga moyo Konde. Madeni yapo tu, usifikirie sana kuhusu madeni, Songa mbele utapata uwezo wa kuyalipa hapo mbele yasikwamishe ndoto zako kwa namna yoyote ile.
 
Pole sana Kaka. Usikate Tamaa, Bado una maana kubwa kwenye huu Ulimwengu. Pambana, Piga moyo Konde. Madeni yapo tu, usifikirie sana kuhusu madeni, Songa mbele utapata uwezo wa kuyalipa hapo mbele yasikwamishe ndoto zako kwa namna yoyote ile.
Asant kwa ushauri wenu. Mmenipa nguvu kuonyesha nina nafasi nyingine tena. Mbarikiwe sanaa
 
Daaah pole sana lakini umenikumbsha Mwaka 2022
Sisi mkubwa anaumwa mdgo wangu wa mwsho anaumwa na mm nnaumwa ila nlmficha bi mkubwa nilitoka msaada Kwa ssta ma dogo wakawa sawa mm.
Niko Hali mabya Sana, yaan nilfikia hatua ya kufa yaan Ile unajiona kabsa kwmba nakufa yaan unaona kabsa gari ya maiti inakuja kukufata afu ndugu zako wanalia, usku ndo usiseme, kijoto chepesii, kibaridi, Ile kutetemka, Ile mavi yanataka kutoka na roho inatka kuchomoka,
Yule binti nilikuwa nae na mtoto wangu mdgo, anasema jamn mm ndo nitaonekana muuaji usife baba flani, jamaniii.
Nashukuru Sana Mtumishi wa Mungu Mwamposa
Afya ilirudi maana yalikuwa mambo ya kishrikina Yale,
 
Back
Top Bottom