Sayansi na matokeo ya tafiti yanapinga hoja za Dkt. Ananelia Nkya juu ya ukubwa wa bunge na serikali

However, Bar-Yam points out that the correlation is only true on average. In fact, the data show some important exceptions. For example, Australia, Canada and New Zealand have large cabinets but high efficiency scores.
Mbona tafiti yako imejipinga yenyewe, au hizo exceptions hujaziona? Kwamba hiyo Canada ina mawaziri kibao ila bado ina ufanisi. Tatizo elimu ya kuunga unga alafu ujuaji mwingi.
 
Nawe umeona udhaifu wake siyo? Amekariri hako ka page ndiyo anataka kudhalilisha dada yetu msomi na tafiti yake?? No way
sijui kama mnajitambua; tuhuma zenu siyo sahihi kwa sababu sijacopy chochote ispokuwa nimeweka ripoti yote ya utafiti. Mgekuwa na uelewa na hoja niwashauri mlete hapa utafiti wa Nkya (PhD) wenu ili tuone hoja yake imesimama kwenye misingi gani?
 
Yeye inaonekana ana faidika na bunge au seriali kubwa, ulaji.. hivyo anaona kupungua kwake itakuwa shida. Lakini ni fact kuwa, kwa nchi zetu hizi masikini ukubwa wa serikali na viongozi wengi wenye nafasi zisizo na msingi vinaongeza umasikini kwa raia.
 
nani kasema causation? Wakiitwa wasomi unampekea Nkya- au ndiye wa kwenza kwenu?
Tukirudi kwenye hoja correlation; tafiti zimethibitisha kuwa upo uhusiano wa maendeleo na ukubwa wa serikali; maendeleo zaidi serikali ndogo; maendeleo kidogo serikali kubwa. Sasa sijui wewe unapinga nini na kwa tafiti ipi?
 
Mkuu leta tafiti ujenge hoja yako;mimi nimeunga mkono hoja yangu na tafiti. kama huna muombe Nkya (PhD) akusaidie maana huwezi kujisimamia
 
Mbona tafiti yako imejipinga yenyewe, au hizo exceptions hujaziona? Kwamba hiyo Canada ina mawaziri kibao ila bado ina ufanisi. Tatizo elimu ya kuunga unga alafu ujuaji mwingi.
Kwa hiyo aya Tanzania tuko sahihi kuwa na serikali na bunge kubwa na lililo na ufanisi kama hayo yaliyotajwa. Au serkali yetu haiendeshwi kwa ufanisi?
 
Uhusiano sio kisababishi.... maana yake it can be a a result of any other factor mfano nchi zenye maendeleo nyingi zina ugatuzi so hauhitaji serikali kubwa, kuna masuala ya separation of power so kama bunge lina nguvu sana na mahakama ipo strong huhitaji wizara nyingi maana mambo mengi yameshagawanywa kwa mihimili mingine, kuna masuala kama nchi nyingi zilizoendelea ni capitalist so kuanzia TANESCO, Babdari, Afya ziko mikononi mwa watu binafsi sasa wizara obvious zinakua ndogo.

Kwahiyo kwenye tafiti ukisema correlation haina mashiko kuliko causation maana ukifanya tafiti ndio ungeweka hizo factor nilizotaja kama control/intervening variables ili kupima uhusiano kati ya maendeleo ya nchi vs ukubwa wa serikali/baraza la mawaziri.

Cc Mayor Quimby
 
Kwa hiyo aya Tanzania tuko sahihi kuwa na serikali na bunge kubwa na lililo na ufanisi kama hayo yaliyotajwa. Au serkali yetu haiendeshwi kwa ufanisi?
Hiyo aya inasema kuna nchi zina baraza kubwa na bunge kubwa ila bado zina ufanisi kuliko nchi zenye bunge dogo!! Mfano Canada na Australia.

Kwa Tanzania ina maana tatizo letu sio ukubwa wa bunge au wizara ila kuna changamoto nyingi kama ufisadi, kukosa vipaumbele, sera mbovu, kukosa coordination, demokrasia mbovu hivyo viongozi hawawajibiki n.k

Sasa hayo unayapima kwa kufanya regression analysis ama structure models sio correlation!! Dr Nkya is right but you're wrong.
 
Mkuu acha kujitoa ufahamu- Nkya (PhD) anaongelea ukubwa wa serikali. Sijui hayo mengine wewe umeyatoa wapi. Ukiwa una nijibu naombapia uje na utafiti wa Nkya (PhD) ile nione hoja yake ambayo wewe unashobokea imesima wapi.
 
Mkuu siyo to causation haina mashiko ila pia kweny mjadala huu haipo kabisa.
Nkya (PhD)anaongelea ukubwa wa serikali- UKUBWA TU. Wewe kheri yako umetoa mazingira yanayoweza kufanya serikali iwe kubwa au ndogo- Mawazo ya KI PhD kabisa siyo huyo mama Nkya. Hana aliko simama anagilibu watu tu
 
Mkuu kausome tena hasa hii aya
In fact, the data show some important exceptions. For example, Australia, Canada and New Zealand have large cabinets but high efficiency scores.
Soma comment yangu iliyopita kabla ya hiyo Uliyoinukuu hapa.
 
Hawa ndiyo mawaziri wa Tanzania sasa walivyo
 
Tafiti inapingwa kwa tafiti kapinge na wewe upate phd
 
Mi mpaka kesho ninaamin hii nchi inaongozwa kutoka nje. Haiwezekan viongoz wakat mwingine kabisa wanaona wanachofanya hakina maslahi na nchi na bado wanaendelea kufanya.
 
Ccm wanakuwaje na akili? Zanzibar ni sawa na Dar Es Salaam kijiografia na licha ya kuwa Dar Es Salaam ina idadi kubwa ya watu karibu mara 5 ya waliopo Zanzibar lakini Dar Es Salaam ina wabunge 8 tu wakati Zanzibar yenye watu milioni moja na kitu sawa na wakazi wa wilaya ya Ubungo pekee ina wabunge 50. Halafu mleta mada anahoji Ph.D ya Dr Nkya anadhani ni ya kupewa kama wanavyopewa wana ccm.
 
Ukiwa CCM akili zinaisha
 
Tafiti inapingwa kwa tafiti kapinge na wewe upate phd
Kwa ufahamu wako unadhani sina PhD?
Achana na hayo; leta hapa utafiti wa huyo Nkya (PhD)
 
Nina mashaka makubwa sana na uelewa wako na elimu yako.
Umenifanya niamini maneno ya Prof. Bisanda kuwa wenye vyeti feki na vilaza ndio huwa na viherehere vya kujifanya wajuaji sana.
 
Wewe kweli unaendelea kututhibitishia ukilaza wako ulivyo mkubwa.

Yule anayetuhumu,ndiye anayetakiwa kuweka ushahidi wa tuhuma hizo.

Umenukuu kitu ambacho hata hukielewi.
Unaambiwa ukweli,unakuwa mkali.
Kama una Ph.D kweli, ni zile za Msukuma.
Aliyeelimika hajisifii,bali elimu yake ndiyo itakayompigania.
Kwa ufahamu wako unadhani sina PhD?
Achana na hayo; leta hapa utafiti wa huyo Nkya (PhD)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…