kali linux
JF-Expert Member
- May 21, 2017
- 2,192
- 5,685
Hello bosses...
Kipindi cha nyuma TerraUSD na Luna zilipopata anguko niliandika uzi humu kwa sababu hilo tukio nlikua nategemea lije kutokea kutokana na mechanics za namna hizo coins zilivokua zinafanya kazi uzi uko hapa CRYPTO-FUNZO KWA WAKURUPUKAJI: Luna coin ilikua ni sawa na $85 wiki ilopita lkn kwa sasa ni takataka(trash coin)
Lakini hili la FTX na FTT kiukweli nilikua sijategemea kama lingetokea. Bila tamaa na uhuni wa Samuel Bankman-Fried anaejulikana kama SBF hili tukio lisingetokea. Luna na TerraUSD zilifail kwa sababu ya technical problems na namna algos zao zilivokua zinafanya kazi ila hii issue ya SBF ni kwa sababu ya tamaa na uhuni. Hata kama CZ angeuza zile tokens isinge-affect sana kama FTX wangekua na management nzuri ya funds.
Kiufupi kabisa wanaodhani SBF kapoteza fedha basi wamedanganyika. Huyu jamaa alikua anatumia fedha za wateja wake kufanya manunuzi binafsi na kucover losses kwenye biashara zake nyingine. Hawa ni watu wanaochezea Balance Sheets za makampuni yao ili kuonesha utajiri usiokuwepo kiuhalisia na kuficha matumizi mabaya ya fedha za wateja wao. Na kizuri cha kuchezea balance sheets ni kwamba huwezi ficha madudu hayo milele, kuna siku tu yatajionesha, mfano mzuri ni kama case ya ENRON au huyu jamaa Ivar Kreuger ambae alijizolea jina la "Match King" kwa sababu ya kumiliki zaidi ya robo tatu ya viwanda vilivokua vinatengeneza viberiti "matches" kwenye miaka ya 1920s. Ivar Kreuger alicheza michezo hatari sana kwenye finance iliofanana kwa kiasi fln na hii hii aliocheza SBF. Tofauti tu ni kwamba Ivar alijiuwa baada ya madudu yake kuonekana. Story kuhusu huyu mwamba ntaandika siku nyingine nikipata muda.
Inasemekana wazazi wa SBF wanamiliki majumba ya kifahari huko Bahamas na mali nyingine ghali ambazo kwa kazi zao na vyanzo vyao vya fedha ni ngumu sana (kama sio impossible) kumiliki. Wazazi wake ni lecturers wa Stanford lakini majumba wanayomiliki ni juu zaidi ya makadirio ya utajiri wao. Inasemekana SBF aliingiza fedha kwenye manunuzi ya hizo mali. Bado hatujui huyu jamaa fedha nyingine kaweka wapi lkn inaonekana kwa asilimia kubwa alikua ana-reallocate hizo fedha kwa njia mbalimbali huku akiwaachia numbers tu wateja wake na ulimwengu ulokua unamfuatilia. Pia inasemekana jamaa alikua anatumia fedha za wateja wake kufanya trading na kucover hasara kwenye biashara zake nyingine.
Huwezi sema huyo mtu wa aina hio kapoteza coz yeye amesha spend hio hela kwa mambo yake, na kaficha hivo hadi ulimwengu ulipokuja kugundua. Waliopoteza ni watu walomwamini na kuinvest kwake. Utafiti unaendelea na kila baada ya siku mbili au moja kuna habari mpya kuhusu huyu jamaa. Upelelezi unaoendelea unaweza onesha huyu jamaa kaficha wapi hizo fedha nyingine, japo kwa juujuu inatengenezwa picha ionekane kweli SBF kapoteza lkn ntakua mtu wa mwisho kuamini hilo.
Happy trading....
~ kali linux
Kipindi cha nyuma TerraUSD na Luna zilipopata anguko niliandika uzi humu kwa sababu hilo tukio nlikua nategemea lije kutokea kutokana na mechanics za namna hizo coins zilivokua zinafanya kazi uzi uko hapa CRYPTO-FUNZO KWA WAKURUPUKAJI: Luna coin ilikua ni sawa na $85 wiki ilopita lkn kwa sasa ni takataka(trash coin)
Lakini hili la FTX na FTT kiukweli nilikua sijategemea kama lingetokea. Bila tamaa na uhuni wa Samuel Bankman-Fried anaejulikana kama SBF hili tukio lisingetokea. Luna na TerraUSD zilifail kwa sababu ya technical problems na namna algos zao zilivokua zinafanya kazi ila hii issue ya SBF ni kwa sababu ya tamaa na uhuni. Hata kama CZ angeuza zile tokens isinge-affect sana kama FTX wangekua na management nzuri ya funds.
Kiufupi kabisa wanaodhani SBF kapoteza fedha basi wamedanganyika. Huyu jamaa alikua anatumia fedha za wateja wake kufanya manunuzi binafsi na kucover losses kwenye biashara zake nyingine. Hawa ni watu wanaochezea Balance Sheets za makampuni yao ili kuonesha utajiri usiokuwepo kiuhalisia na kuficha matumizi mabaya ya fedha za wateja wao. Na kizuri cha kuchezea balance sheets ni kwamba huwezi ficha madudu hayo milele, kuna siku tu yatajionesha, mfano mzuri ni kama case ya ENRON au huyu jamaa Ivar Kreuger ambae alijizolea jina la "Match King" kwa sababu ya kumiliki zaidi ya robo tatu ya viwanda vilivokua vinatengeneza viberiti "matches" kwenye miaka ya 1920s. Ivar Kreuger alicheza michezo hatari sana kwenye finance iliofanana kwa kiasi fln na hii hii aliocheza SBF. Tofauti tu ni kwamba Ivar alijiuwa baada ya madudu yake kuonekana. Story kuhusu huyu mwamba ntaandika siku nyingine nikipata muda.
Inasemekana wazazi wa SBF wanamiliki majumba ya kifahari huko Bahamas na mali nyingine ghali ambazo kwa kazi zao na vyanzo vyao vya fedha ni ngumu sana (kama sio impossible) kumiliki. Wazazi wake ni lecturers wa Stanford lakini majumba wanayomiliki ni juu zaidi ya makadirio ya utajiri wao. Inasemekana SBF aliingiza fedha kwenye manunuzi ya hizo mali. Bado hatujui huyu jamaa fedha nyingine kaweka wapi lkn inaonekana kwa asilimia kubwa alikua ana-reallocate hizo fedha kwa njia mbalimbali huku akiwaachia numbers tu wateja wake na ulimwengu ulokua unamfuatilia. Pia inasemekana jamaa alikua anatumia fedha za wateja wake kufanya trading na kucover hasara kwenye biashara zake nyingine.
Huwezi sema huyo mtu wa aina hio kapoteza coz yeye amesha spend hio hela kwa mambo yake, na kaficha hivo hadi ulimwengu ulipokuja kugundua. Waliopoteza ni watu walomwamini na kuinvest kwake. Utafiti unaendelea na kila baada ya siku mbili au moja kuna habari mpya kuhusu huyu jamaa. Upelelezi unaoendelea unaweza onesha huyu jamaa kaficha wapi hizo fedha nyingine, japo kwa juujuu inatengenezwa picha ionekane kweli SBF kapoteza lkn ntakua mtu wa mwisho kuamini hilo.
Happy trading....
~ kali linux