Security alert kwa Serikali yetu: Tuwe makini sana na Marekani, kuna kitu kinapangwa halafu wajifanye walionya kabla. Je, wanapanga kutu-Libya?

Security alert kwa Serikali yetu: Tuwe makini sana na Marekani, kuna kitu kinapangwa halafu wajifanye walionya kabla. Je, wanapanga kutu-Libya?

Wapi walikopiga kura tuoneshe? Wapi watanzania walipiga hizo kura CCM ikapata kura 99.9%?
Kama ni kweli watanzania hawavutiwi na mfumo wa uendeshaji wa serikali yetu mbona katika uchaguzi wa serikali za mitaa CCM imepata ushindi wa 99%??

Tanzania tuna akiba ya dola bilioni 4 zinazoweza kuendesha nchi kwa miezi minne.Marekani hatuwezi.Sisi ni donor country.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Paschal nilikuwa nakuheshimu Sana ukiwa ITV. Ila kwa hizi Pumba unazoziandikaga humu kujifanya Politics and Security Expert Yani nakuona Zero brain. Eti uchaguzi wa serikali za mitaa ulikuwa wa kidemokrasia na CCM ikashinda 99.9%. Jamani hata Kama ndo njaa inakusumbua na kutafuta utezui at least reason kama a professional Journalist unajitia aibu na mabandiko yako yanayoonyesha wazi uko biase.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu Pasko,andiko lako ni refu sana ila nafikiri baadhi ya source zako pia nilishazisoma na nafikiri baadhi ya source ni waandishi wa habari,watafiti na wapelelezi.Kuhusu ukweli wa hoja zilizowekwa sidhani kama kuna mjadala hapo kwamba mambo waliyosema yanaendelea nchini ni kweli kwamba yapo au yametokea kuhusu ukweli wa mambo yatakayotukia nafikiri hilo linahitaji akili kubwa sana ili kuweza kutambua kama kuna ukweli ni pia muda utatuambia.

Ni kweli vijana wa kitanzania wengi sana wamejiunga na makundi ya kigaidi-militants na pia unaona kabisa kumbwa tuna wimbi kubwa la digital activists ambao kwa hakika kuna hatua itafia wataweza kutumika kutimiza kile unachohofia.

Binafsi sikubaliana na wewe kusema kwamba hili ni security issue,hapana hili in operational issue,ni suala tu la serikali kurekebisha mambo,kutenda haki na kuonesha nia kabisa ya kutaka kujenga umoja wa kitaifa.Usitake kuwasingiza wamarekani wakati ukweli ni kwamba wao hata kama wakitu-Libya kama unavyosema watatumia internal weakness zetu kuwezesha hilo.

najua bado Msemaji wa serikali hajateuliwa ila usijali.KAMA IPO,IPO TUUUU
 
Paskali umeshusha nondo nzito kwa kweli, tena umezishusha muda muafaka, wakati huu ambapo kila tukiamka tunasikia wakristo wamechoma Quran, then wakachoma Juzuu, haya matukio yakufuatana hivi hayapangwi kweli? na kwanini yaje wakati huu tunapoelekea uchaguzi mkuu?

Hapa ninachoona, kuna jamaa wameshaona hali yao kisiasa ni mbaya, kuanzia ndani ya nchi, ndani ya chama chao, mpaka nje kwenye mahusiano na jumuia za kimataifa, sasa wanachojaribu kufanya ni ku-divert attention, tutoke kuwaza yaliyotokea hivi karibuni ( kumbuka zuio la wamarekani kwa mkuu wa mkoa wa Dsm), watulete kwenye mambo ya kidini ili wapate ahueni kisiasa.

Pia, maswali yako kuhusu hayo yanayoitwa extremist groups kwenye hiyo mikoa mitatu uliyoitaja, hebu tujaribu kukumbuka yale matukio ya Rufiji wakati ule yalivyotokea, utapata picha kwamba hali ya usalama hasa ukanda wa Pwani hairidhishi, wale watu walitoa wapi silaha za kufanyia yale matukio? kama yale yaliwezekana kwanini hayo wanayosema sasa yasiwezekane? na habari kwamba wapo wanaofanya mazoezi ya "karate" misikitini zipo muda mrefu tu, pia wale wasomali ambao huwa wanakamatwa kwenye malori wakisafirishwa, je, wote hukamatwa?.. sidhani, na kama wapo wasiokamatwa huwa wanaishia wapi?

Kwa ufupi usalama wa nchi yetu sio wa kuridhisha hata kidogo, ndio maana kwangu mimi naona bora nifunge mdomo kuliko kupinga hiyo kauli kwamba kuna makundi ya wenye itikadi kali kwenye hiyo mikoa mitatu, tena inawezekana ikawa zaidi ya hiyo mitatu.

Mwisho kabisa, mchawi wa mengi kati ya hayo uliyoandika ni viongozi wetu wenyewe, waache ukatili dhidi ya raia, wawe na mioyo mipana, wakubali kukosolewa, na wajue anaekukosoa sio adui, ubabe kwenye dunia ya sasa hauna maana, hivyo kwa hili pia siwezi kumlaumu Marekani, inshort, tumevuna tulichopanda.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mbona uhoji wapi walipata silaha wale walimshambulia Mh Lissu ndani ya eneo ya eneo la bunge?.

Aiseeee... bora taifa lisambalatike tu.. watakao baki uenda wakazaa kizazi chenye haki.

Nope:
Naunga mkono marekani na washirika wake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni rahisi sana serikali kuyaepuka hayo yote kama serikali ikijitahidi kuwatengenezea mazingira mazuri vijana wa Tanzania maana wao ndio watakao tumika kwenye machafuko yoyote yale yatakayo pangwa na hao mnao waita mabeberu.

Cha msingi [emoji117]serikali ijitahidi sana kutoa ajira kwa vijana ikiwemo fursa za kujiari zinazo eleweka na sio za ki babaishaji

Nazungumzia vijana maana wao ndio wahusika wakuu watao tumika katika ushawishi wowote ule.

Na ihakikishia serikali ikifanya hivyo mbinu za mabeberu kujaribu kuihujimu Tanzania yetu haita fanikiwa kamwe maana watanzania ni wazalendo sana na nchi yao kama viongozi wakiwa wanawajali.
True taifa lolote lenye umoja ni ngumu kulisambaratisha kosa kubwa alilofanya Gadaffi na saddam ni kutowaunganisha watu wao.Jiulize mbona Iran imeshindikana kuisambaratisha sababu ni moja.Taifa lolote lisilo na umoja haiitaji dakika kulisambaratisha je ni nani chanzo cha kuvunja umoja wetu?
 
Mkuu hawa majamaa wametupima na kujua kuwa udhaifu wetu upo kwenye dini.

Hiyo itakua njia rahisi ya kutuvuruga.

Huko kwenye sekta ya madini wameona wanapoteza.

Fahamu kuwa, Sekta ya madini mabeberu wamejaza majasusi wastaafu ndio wanaofanya hizo shughuli. ( Inabidi pia na sisi tuweke assests wetu huko, tena wale wazalendo haswa)

Kwakua sekta ya madini ni muhimu mno, na kuwabana huko ni kuwanyima ulaji hawana namna zaidi ya kuretaliate.

Serikali inapaswa kuwa makini mno, kwenye maswala ya Udini na hasa Uhaguzi wa 2020.

Kila la heri mama Tanzania.
ona ili nalo..
madini yamekuwaje?.
wakati wa tawala zingine Tanzania haikuwa na madini? kwanini hali hii iwe utawala huu tu?.

ebu nitajie kampuni hata moja tu ya Marekani inayojihusisha na madini Tanzania..

Mameee...
nipo tayali kuuza hata kuku wangu kumsapoti marekani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pascal Mayalla,

Paskali, nadhani unatakiwa kuwaambia hao watawala ndio wawe makini, unaposema tuwe makini sisi sikuelewi kabisa, sijasoma maelezo yako yote kwani yanakatisha tama hata kuyasoma yote, (kwa kutumia heading yako tu), mimi naona Marekani wanachelewa tu, wangechukua hatua ya wanachotaka kufanya ile tujue kinachofuata.
Marekani inapaswa kuwachukulia hatua mapema wote wanaoashiria uvunjifu wa amani hii itaipunguzia dunia kuingia gharama za kuhudumia wakimbizi ni heri wachache waliokosa malezi bora wakaangamizwa ili ibaki salama.Kuna watu walitakiwa wabakie kuzimu wamsaidie ibilisi kazi na sio kuwaleta duniani kuwaumiza wengine Mungu alikosea sana
 
Elimu, Ujuaji kupitiliza tena kwa maslahi ya watu wachache hili ni tatizo kwa Taifa, Niwapongeze tu wale wote wanaoikosoa serikali hii ya awamu ya 5 maana wanatia chachu ya kile kinachoonekana kukosewa kiweze kurekebishwa na ili uwe sahihi lazima ukubali kukosolewa. Ni jukumu letu kwa pamoja kuweza kuilinda amani hii, Mungu atunusuru tusije ingia katika machafuko maana itakua ni anguko letu la amani ya kudumu
 
Back
Top Bottom