Segerea: Wabunge wa CHADEMA Ester Bulaya, Ester Matiko na Halima Mdee waachiwa. Wasema sasa ni saa ya ukombozi Tanzania

hapo watawalazimisha waende majumbani kwao moja kwa moja na sio kwenye ofisi za Chama.

CCM wanahaha mno kuona hii hukumu inawapa Chadema credits.
 
Akwelina ni matokeo ya makosa yaliyofanywa na hao waliotoka leo.

Wasingeandamana bila kibali, Who knows binti wa watu angekuwa keshamaliza masomo yake anafaidi matunda ya elimu yake.
Hayo maandamano ni matokeo ya nini?
kwa nini chadema waliandamana??
 
Kwani hakukuwa na njia nyingine ya kufanya zaidi ya hiyo ya kuandamana bila kibali?? Angalia sasa vitendo vyao vimegharimu maisha ya binti asiyekuwa na hatia. Hamlioni hilo??
 
Akwelina ni matokeo ya makosa yaliyofanywa na hao waliotoka leo.

Wasingeandamana bila kibali, Who knows binti wa watu angekuwa keshamaliza masomo yake anafaidi matunda ya elimu yake.
Aliyefyatua risasi na kumuua Akwilina yuko wapi sasa hivi je amechukuliwa hatua gani!!
 
Tunahitaji mrejesho wa mzigo uliozidi(uwazi na ukweli)
Ili ufanyeje. Tumempa Mbowe kwa hiari yake akanywee bia akitaka ahonge. Hata wewe ukitaka nenda akuhonge. Hela za wanaume wenzio roho inataka kukutoka. Tafuta zako. Au sema uchangiwe
 
Erythrocyte,
Naona CCM na dola yao wamechoka na amani. Yaani wanajaribu kuwatega wananchi ili vurugu zitokee. Wanachokitaka this year watakipata wasifikirie watanzania ni wanyonge na wajinga. Wabunge wametoka magereza kuna tatizo gani wakiwapa ulinzi mpaka makao makuu ya chama.

Hivi hili ni jeshi la polisi ya watanzania au ni Jeshi la Polisi ya ccm. Siro kakaa kimya Simbachawene kakaa kimya yaani wote wanaogopa. Tunamwogopa one man show.

Kweli sisi watanzania ni mambumbu. Ndio maana tunawaruhusu wachina watuletee Corona wakati tumewazuia watoto wetu wanaosoma China wasirudi nchini. Dunia nzima wanawazuia Wachina kwa muda kuingia kwenye nchi zao. Sisi serikali yetu yenye njaa inawaruhusu
 
Kiongozi walikua wamenyimwa haki yao ya kikatiba,mkurugenzi hayupo ofsini siku mbili uchaguzi kesho yake na kampeni wamepiga kwa gharama hawana mawakala maana hawajaapishwa kisheria wangefanyaje? mbona hatuangalii chanzo cha wao kuandamana?

Mkuu mtawala mdhalimu hawezi kuangalia mantiki au chanzo au haki... Wenye haki ni walioupande wake!!
Yeye anajipofusha na kujiondoa ufahamu na kutenda kwa makusudi!

Lugha anayoielewa si kama hii ya kwako. Kuna lugha fulani fulani hivi anazisikia vizuri sana...
Kwa sasa inabidi tujifunze lugha hii kwa kuangalia historia na ufanisi wake maeneo mengine.

Na ikibidi tuitumie kufikisha ujumbe!!!
It is the only available option!!
Aluta Continua!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…