Sehemu salama ya mwanaume ni wapi?

Sehemu salama ya mwanaume ni wapi?

Mshangazi dot com

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2011
Posts
1,345
Reaction score
3,503
Afya ya akili kwa wanaume imekua tatizo linalokua kwa kasi sana na kusababisha matatizo na majanga ambayo tumekua tukiyasikia kila siku.

Naomba kuuliza wanaume mliopo JF:
  1. Huwa unazungumza na nani kuhusu matatizo au changamoto binafsi ulizonazo?

  2. Je ukikwama kikazi, kibiashara, kimahusiano n.k, msaada huwa unapata wapi?

  3. Una mtu maishani ambaye unaweza kumwambia mambo yako ya ndani kwa uhuru bila kuogopa kuwa judged (kuhukumiwa au kuonekana ndivyo sivyo)?

  4. Una mambo au vitu unavyopenda kufanya wewe mwenyewe ambavyo vinakupa furaha?

  5. Unaamini kwenye kutafuta msaada wa kisaikolojia au kitabibu (therapy / couseling) pale utakapoelemewa au watu wakikishauri kufanya hivyo?

Nauliza genuinely kwa sababu nataka kujifunza kama mama wa watoto wa kiume ambao watakuja kuishi kama wanaume kwenye jamii zetu siku za usoni.
 
Mwanaume ukiona umezidiwa kabisa kisaikolojia/msongo wa mawazo, piga push ups.

Kama una hasira ya kuachwa piga push ups utakuja kunishukuru.

Kuna watu ndoa zikiwazidia, ugomvi usiokwisha huwa wanaenda kwa washauri wa ndoa,

Halafu unakuta mshauri mwenyewe mwanamke.
 
Afya ya akili kwa wanaume imekua tatizo linalokua kwa kasi sana na kusababisha matatizo na majanga ambayo tumekua tukiyasikia kila siku.

Naomba kuuliza wanaume mliopo JF:
  1. Huwa unazungumza na nani kuhusu matatizo au changamoto binafsi ulizonazo?
  2. Je ukikwama kikazi, kibiashara, kimahusiano n.k, msaada huwa unapata wapi?
  3. Una mtu maishani ambaye unaweza kumwambia mambo yako ya ndani kwa uhuru bila kuogopa kuwa judged (kuhukumiwa au kuonekana ndivyo sivyo)?
  4. Una mambo au vitu unavyopenda kufanya wewe mwenyewe ambavyo vinakupa furaha?
  5. Unaamini kwenye kutafuta msaada wa kisaikolojia au kitabibu (therapy / couseling) pale utakapoelemewa au watu wakikishauri kufanya hivyo?

Nauliza genuinely kwa sababu nataka kujifunza kama mama wa watoto wa kiume ambao watakuja kuishi kama wanaume kwenye jamii zetu siku za usoni.
Hiyo sentensi yako ya mwisho inabeba majibu yote unayoyataka, kwa namna hizi;

1. Unamwonaje baba wa watoto wako..??

2. Baba wa watoto wako, anazungumza na wewe kuhusu matatizo au changamoto alizonazo?

3. Akikwama kikazi, kibiashara, kimahusiano n.k, baba wa watoto wako, msaada huwa anapata kwako?

4. Baba wa watoto wako, ana mtu maishani ambaye anaweza kumwambia mambo yake ya ndani kwa uhuru bila kuogopa kuwa judged (kuhukumiwa au kuonekana ndivyo sivyo)? huyo mtu ni wewe?

5. Baba wa watoto wako, ana mambo au vitu anavyopenda kufanya yeye mwenyewe ambavyo vinampa furaha?

6. Baba watoto wako anaamini kwenye kutafuta msaada wa kisaikolojia au kitabibu (therapy / couseling) pale atakapoelemewa au watu wakimshauri kufanya hivyo?
 
Back
Top Bottom