Sehemu salama ya mwanaume ni wapi?

Sehemu salama ya mwanaume ni wapi?

Yupo jamaa yangu mmoja ni binamu yangu amenizidi miaka mitano. Yeye ndio huwa namshirikisha mbanga kama hizi za biashara na mahusiano



Nikiwa na mambo au vitu napenda kuzungumza na baba yangu mzazi. Yuko poa sana. Lakini pia napenda sana mazoezi binafsi na kucheza mpira inanifanya nijione bado niko alive.

Kuna kipindi nilipitia changamoto za kimahusiano nikatafuta mwana saikolojia tukashauriana mambo kadhaa maana nilikua naelekea kubaya.
Hii imekaa vizuri sana, kuwa na support system ni muhimu na ushauri wa kisaikolojia ukizidiwa ni lazima.

Asante kwa reply yako Southern Highland
 
Mwanaume ukiona umezidiwa kabisa kisaikolojia/msongo wa mawazo, piga push ups.

Kama una hasira ya kuachwa piga push ups utakuja kunishukuru.

Kuna watu ndoa zikiwazidia, ugomvi usiokwisha huwa wanaenda kwa washauri wa ndoa,

Halafu unakuta mshauri mwenyewe mwanamke.
Kufanya mazoezi nayo ni namna mojawapo ya kurelease.

Mshauri hata akiwa mwanamke siyo shida, pale yupo kazini kwa kitu alichokisomea au kupata taaluma nacho so ana uwezo wa kukusaidia pia.
 
Afya ya akili kwa wanaume imekua tatizo linalokua kwa kasi sana na kusababisha matatizo na majanga ambayo tumekua tukiyasikia kila siku.

Naomba kuuliza wanaume mliopo JF:
  1. Huwa unazungumza na nani kuhusu matatizo au changamoto binafsi ulizonazo?
  2. Je ukikwama kikazi, kibiashara, kimahusiano n.k, msaada huwa unapata wapi?
  3. Una mtu maishani ambaye unaweza kumwambia mambo yako ya ndani kwa uhuru bila kuogopa kuwa judged (kuhukumiwa au kuonekana ndivyo sivyo)?
  4. Una mambo au vitu unavyopenda kufanya wewe mwenyewe ambavyo vinakupa furaha?
  5. Unaamini kwenye kutafuta msaada wa kisaikolojia au kitabibu (therapy / couseling) pale utakapoelemewa au watu wakikishauri kufanya hivyo?

Nauliza genuinely kwa sababu nataka kujifunza kama mama wa watoto wa kiume ambao watakuja kuishi kama wanaume kwenye jamii zetu siku za usoni.
N kutafuta bar zilizo na amsha amsha na kuinjoi na totoz kali
 
Sijafikia hatua hiyo, ila kuna wana mna share vitu vingi si mbaya kuongea nae, na kama vipi muhusishe mdingi wako, ama viongozi wa kidini.
Viongozi wa dini, usikute ba wenyewe wana changamoto! 😄 just kidding..
 
Afya ya akili kwa wanaume imekua tatizo linalokua kwa kasi sana na kusababisha matatizo na majanga ambayo tumekua tukiyasikia kila siku.

Naomba kuuliza wanaume mliopo JF:
  1. Huwa unazungumza na nani kuhusu matatizo au changamoto binafsi ulizonazo?
  2. Je ukikwama kikazi, kibiashara, kimahusiano n.k, msaada huwa unapata wapi?
  3. Una mtu maishani ambaye unaweza kumwambia mambo yako ya ndani kwa uhuru bila kuogopa kuwa judged (kuhukumiwa au kuonekana ndivyo sivyo)?
  4. Una mambo au vitu unavyopenda kufanya wewe mwenyewe ambavyo vinakupa furaha?
  5. Unaamini kwenye kutafuta msaada wa kisaikolojia au kitabibu (therapy / couseling) pale utakapoelemewa au watu wakikishauri kufanya hivyo?

Nauliza genuinely kwa sababu nataka kujifunza kama mama wa watoto wa kiume ambao watakuja kuishi kama wanaume kwenye jamii zetu siku za usoni.

Mwanaume anatakiwa apitie changamoto zote, Halafu ajue yupo mwenyewe, no one will save his S, then atakuwa amepevuka!
 
Hiyo sentensi yako ya mwisho inabeba majibu yote unayoyataka, kwa namna hizi;

1. Unamwonaje baba wa watoto wako..??

2. Baba wa watoto wako, anazungumza na wewe kuhusu matatizo au changamoto alizonazo?

3. Akikwama kikazi, kibiashara, kimahusiano n.k, baba wa watoto wako, msaada huwa anapata kwako?

4. Baba wa watoto wako, ana mtu maishani ambaye anaweza kumwambia mambo yake ya ndani kwa uhuru bila kuogopa kuwa judged (kuhukumiwa au kuonekana ndivyo sivyo)? huyo mtu ni wewe?

5. Baba wa watoto wako, ana mambo au vitu anavyopenda kufanya yeye mwenyewe ambavyo vinampa furaha?

6. Baba watoto wako anaamini kwenye kutafuta msaada wa kisaikolojia au kitabibu (therapy / couseling) pale atakapoelemewa au watu wakimshauri kufanya hivyo?
Mpe soln mkuu ..je kama ni single mama haishi na mume
 
hayo mambo yote huwa tunaongea na father na kwenye vikao vyetu, labda kama kikao cha mwisho hawakuhudhuria 😎
Sio wote wana hao mababa ambao wanaweza kuongea nao au kufunguka kwao. Wanaume wa namna hiyo wafanyaje sasa?
 
Afya ya akili kwa wanaume imekua tatizo linalokua kwa kasi sana na kusababisha matatizo na majanga ambayo tumekua tukiyasikia kila siku.

Naomba kuuliza wanaume mliopo JF:
  1. Huwa unazungumza na nani kuhusu matatizo au changamoto binafsi ulizonazo?

  2. Je ukikwama kikazi, kibiashara, kimahusiano n.k, msaada huwa unapata wapi?

  3. Una mtu maishani ambaye unaweza kumwambia mambo yako ya ndani kwa uhuru bila kuogopa kuwa judged (kuhukumiwa au kuonekana ndivyo sivyo)?

  4. Una mambo au vitu unavyopenda kufanya wewe mwenyewe ambavyo vinakupa furaha?

  5. Unaamini kwenye kutafuta msaada wa kisaikolojia au kitabibu (therapy / couseling) pale utakapoelemewa au watu wakikishauri kufanya hivyo?

Nauliza genuinely kwa sababu nataka kujifunza kama mama wa watoto wa kiume ambao watakuja kuishi kama wanaume kwenye jamii zetu siku za usoni.
Na nyie ambao ni majike dume usalama wenu upo wapi?
 
Back
Top Bottom