KERO Sehemu ya Kuabudia Airport izingatie Dini zote

KERO Sehemu ya Kuabudia Airport izingatie Dini zote

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
1. Sehemu za Kuabudia Airport iwe takwa la Kisheria na sio hisani kama inavyofanyika sasa au kupendelea upande moja.

2. Laiti airport pangejengwa Kanisa tu sijui hali ingekuaje mpaka sasa.


NB: JNIA Terminal 3 wamejitahidi Ila wamesahau dini nyingine, kwanini? KERO.
Sioni sababu ya hoja yako. Kuna maeneo ambayo taasisi za dini zilipewa baada ya kuyaomba zijenge nyumba zao za ibada. Uwanja wa ndege siyo eneo la taasisi za dini kujenga nyumba za ibada. Kwa ndugu zetu Waislamu kuwa na chumba cha sala uwanja wa ndege, ni understandable kutokana na mfumo wao wa kuswali sala 5 kwa siku. Taasisi zingine za dini hazina shida na hitaji hili. Hivyo, hoja kwamba hizi taasisi zipewe vyumba vya kufanyia ibada zao uwanja wa ndege, naona haina mashiko kwa sababu mwisho wa siku uwanja wa ndege utageuka kuwa nyumba za ibada za taasisi za dini mbalimbali zilizoko nchini. Wahindu, Wakristo (ambao mahitaji yao katika nyumba zao za ibada ni tofauti pia), Waislamu, dini za asili, etc.
 
Hlf cha kushangaza kuna baadhi ya nyuzi ukipitia unakuta bado wanazungumzia hizo habar,yan nashindwa kuelewa shida iko wapi?

Ukiandika mapenz ooh nchi hii watu wanawaza mapenzi,ukileta challenge ya vocha ooh tunadhalilishana,,sijui tunataka nini
Kumbe ni ww nilikua natafuta ni nani huyo anachambwa kila uzi?? 😄😄
 
1. Sehemu za Kuabudia Airport iwe takwa la Kisheria na sio hisani kama inavyofanyika sasa au kupendelea upande moja.

2. Laiti airport pangejengwa Kanisa tu sijui hali ingekuaje mpaka sasa.


NB: JNIA Terminal 3 wamejitahidi Ila wamesahau dini nyingine, kwanini? KERO.
Mitano tena. Magufuli mlimnanga sana yaani misikiti iote kama uyoga ndipo titaelewana
 
1. Sehemu za Kuabudia Airport iwe takwa la Kisheria na sio hisani kama inavyofanyika sasa au kupendelea upande moja.

2. Laiti airport pangejengwa Kanisa tu sijui hali ingekuaje mpaka sasa.


NB: JNIA Terminal 3 wamejitahidi Ila wamesahau dini nyingine, kwanini? KERO.
Usitake kushindana na mtoto wa bibi anayependa kudeka, akifichiwa ubwabwa jikoni, kula mliopewa ule mwingine jifanye haukuuona.
 
Ndo hasara ya kuacha wapumbavu wawe na wafanya maamuzi huo ni ushenzi au kwa kua wakristo si watu wa kelele na vurugu? Wangeweka la wakristo hapo ungesikia fujo ..Pale kuna siku unatafuta mchungaji mnaenda kufanya ibada kwenye sehem ya kusubiria abiria piga ibada kali sana harafu ajitokeze mtu kuwakamata mnasema mbona waislam mmewapa sehem na ikiwa na kundi hili lina watu wachache sana tz.
 
Jumapili na Jumamosi watu hawasafiri?
Kanisa liwe dhehebu gani? Wasabato au anglikan au ?
Mnapaswa muelewe sio kila kitu cha dini kiwe na usawa.
Waislam ndy wanaswali kwa wakati maalum na ni mara 5 kwa siku.

Je wakrsto wanasali mara ngp kwa siku? Na je wakristo wote wanaweza sali kanisa moja bila kujali dhehebu?
 
Ila tukiwa wakweli ni waislamu peke yake wanasali mara tano kwa siku,sasa tusitake baadhi ya mambo yawe sawa kwakuwa tu waislamu wanatengewa sehemu ya ibada basi ikawa shida

Lau kama wasio waislamu wangekuwa nao wanaswali swala tano hapo hakika ingekuwa sio haki

Hata injinia alipomjibu Makonda alimwambia duniani kote waislamu ndio hutengewa sehemu za ibada,ila Makonda alijibu kisiasa tu kuwafurahisha watu angali ukwel anujua kuwa wakristo hawana hizo ibada
Sio kweli wapo wakristo wanaofanya ibada muda mwingi
 
Back
Top Bottom