Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,108
- 10,191
Niliwahi kutibiwa Seifee Hospital iliyoko mjini Dar es Salaam, inayopatikana ile njia kama unaenda Posta. Tangu nitibiwe pale wamekuwa wakinitumia matangazo ya madaktari wanaofika kwao. Hawa jamaa muda si mrefu nitawashtaki maana namba yangu ya simu ni taarifa binafsi na inapochukuliwa inapaswa kuchukuliwa kwa matumizi ninayoyahitaji tu sio kuanza kunitumia matangazo.
Seifee mtambu kuwa unapomtumia mtu ujumbe asiouhitaji mnakiuka haki zangu za kidigitali, lakini pia jumbe zenu hazina namna ya kujitoa ili mtu asipate meseji hizo. Naomba mtambue kuwa tayari Sheria ya Ulinzi wa taarifa binafsi imeshatungiwa kanuni, nitawazingua muda si mrefu.
Someni kifungu cha 35 cha Sheria ya Ulinzi wa Taarifa binafsi. Nimemaliza, endeleeni niwapeleke mnapostahili.
Seifee mtambu kuwa unapomtumia mtu ujumbe asiouhitaji mnakiuka haki zangu za kidigitali, lakini pia jumbe zenu hazina namna ya kujitoa ili mtu asipate meseji hizo. Naomba mtambue kuwa tayari Sheria ya Ulinzi wa taarifa binafsi imeshatungiwa kanuni, nitawazingua muda si mrefu.
Someni kifungu cha 35 cha Sheria ya Ulinzi wa Taarifa binafsi. Nimemaliza, endeleeni niwapeleke mnapostahili.