Sekondari za Vipaji maalum takribani miaka 40 tangu kuanzishwa kwake umaalum wake uko kwenye nini? Hatuoni ubunifu wowote

Sekondari za Vipaji maalum takribani miaka 40 tangu kuanzishwa kwake umaalum wake uko kwenye nini? Hatuoni ubunifu wowote

Mimi nadhani umechangia wazo zuri tu hukuwa na haja ya kutukana watu.

Sasa hao wauza uchi na machawa ndio wanaoonekana. Hao unaodhani wana maana hatuwaoni. Sasa jamii ifanyeje?
Huyo muhandisi mzalendo kapuyanga sana, amedhiirisha kuwa hao wahitimu wa special schools ni wakawaida sana vichwani mwao, hili kuonesha uspecial wake hakutakiwa kabisa hata kuwafikiria hao machawa.

Huyo ilipaswa aje na Idea kwamba tutaweza vipi kufanya desalination kwa haya maji ya bahari ya Hindi hili tuweze kuyatumia majumbani kwetu tuache kutegemea maji ya mto Ruvu... halafu atwambie ni kiasi gani kinahitajika hili mimi nifund hiyo project😅😅
 
Ofcourse wote hawawezi kuwa wagunduzi. Lakini mpaka uzi umefik hapa hakuna hata mfanno mmoja uliotolewa.
Nimeona jamaa muhandisi mzalendo amekutajia PAWA AI aisee hiyo software hasa ya Sartify ni copy ya Chatgpt, alochojitahidi labda ni kugeuza lugha tu, na bado pia haiko effective kwenye data protection...na ndio maana hata bado haijulikani.

Kwa ufupi hakuna unique innovation yoyote hapa kwenye hiyo PAWA.
 
Wengi waliochaguliwa kwenye hizo shule za vipaji maalum walikuwa ni watu wenye uwezo wa kukariri masomo
Ndo sababu uvumbuzi hakuna
 
Nimeona jamaa muhandisi mzalendo amekutajia PAWA AI aisee hiyo software hasa ya Sartify ni copy ya Chatgpt, alochojitahidi labda ni kugeuza lugha tu, na bado pia haiko effective kwenye data protection...na ndio maana hata bado haijulikani.

Kwa ufupi hakuna unique innovation yoyote hapa kwenye hiyo PAWA.
Atleast kwa kuanzia si mbaya
 
Huko umeenda chini kabisa je umewahi kujiuliza SUA imekusaidia nini licha ya kuwa ni chuo kikubwa na cha muda mrefu hadi sasa? Je umenufaika nacho nini?
Kuna nyakati fulani nilipata bingo la ufadhili wa miradi wa maendeleo la kaka $200k, ile pesa nilitaka nitenge nusu yake kisha nitafute graduates hata 50 kutoka SUA tufanye kilimo cha kisasa kabisa.. ila kuna mtu akaniambia niahairishe huo mpango
 
Tumejionea wenyewe kule chini na mahala pengine kama ulaya Watoto wadogo wanaandaliwa kiwa Wanasayansi na mainjinia wabobezi. Watoto hao wanasukwa na kufinyangwa kiasi kwamba wanaanza kubuni na kuvumbua Mitambo na teknolojia za kipekee zenye mchango mkubwa ktk maendeleo ya kiuchumi kwenye nchi zao.

Hapa Tanzania mfumo wa Shule za Vipaji maalum umekuwepo kwa miaka mingi sasa.

Binafsi sikuwa na bahati ya Kujiunga na shule hizo hivyo nilitarajia pia kunufaika na Ubunifu/ innovations kutokana na kundi hili kubwa wenye vipaji Maalum/ special inteligence.

Tuna sekondari nyingi kama
1. Ilboru Arusha
2. Msalato Girls Morogoro
3.Mzumbe Boys Morogoro
4.Kibaha Boys Pwani
5. Tabora girls na Tabora Boys.

Ndio kusema Maelfu kwa Maelfu ya Wanafunzi waliopita humo hakuna hata wawili watatu walioonesha Ukipaji wao?

Tuseme basi Mtaji ni Mkubwa ku invest, hata Basi Kuwa Social influencer/ matumizi ya tech zilizopo je?

Tunaona Watu wenye elimu kiasi tu ndio wanaofaidi matumizi ya Technolojia na kunufaika na kuitangaza Tanzania.
Watu kama akina Maulid Kitenge, Kipanya, Zembwela, Diamond, Millard Ayo, Mwijaku, Baba Levo, Mobeto.

Angalau hawa hawakugundua chochote kama walivyo wale wa vipaji maalum ispokuwa wameweza kugundua matumizi sahihi ya teknolojia iliyopo.

Vipaji maalumu katika sekondari hizo ni vya mchongo au tunakwama Wapi?

Bonjour, Je M'apelle Bush Dokta habité à Makerere universite.

Bonvenué de discusio reun̈ion
Walishauwa na sasa tuna tapatapa tu nchi haina think tanks
 
Niliwahi kusikia waligundua Namba ya Panya kugundua Magonjwa ya TB kwenye Sample za Makohozi. Hadi leo sijajua imefikia wapi ile project
Vipi na yule panya aliyekuwa anategua mabomu? Aliishia wapi?
 
Ngoja nikuulize swali fulani hivi ili tuondoe contradiction.
Kuna jamaa mmoja hivi tulisomaga naye sekondari yule jamaa yeye udhaifu wake alikuwa hajui kabisa somo la kiingereza yaani kwa kifupi yeye sentensi yoyote iliyoandikwa kwa kiingereza yeye alikuwa hajui kabisa inaongelea nini na likija somo lile la kiingereza alikuwa anaambulia D akipata C ni kwa kubahatisha.
Lakini yule jamaa yeye ujanja wake ilikuwa ni kukesha usiku na mchana kukariri notsi na mitihani ikija alikuwa anapata A nyingi tu za masomo ya Sayansi na kwenye Darasa lake alikuwa anaingia 3 bora kwa watu wanaofaulu sana.
Je huyu jamaa naye ni kipanga au sio kipanga kwa uwelewa wako?
Huwezi kukalili Physics,Hesabu na Chemistry. Huwezi kwani swali moja linaweza kuulizwa kwa style zaidi ya tatu. Hayo masomo huwezi kukalili.

Hiyo Chai na ili uweze kukalili lazima ujue sentence inamanisha nini, kama ndio hivyo basi hata kujifunza hizi lugha ingekuwa rahisi.

Hii ni chai unatupanga.
 
Na
Hao ndo wanakuendeshea maisha mkuu,

Wamejaa mawizara yote, wamejaa mataasisi yote makubwa,

Kama haujui Hao ndo muhimili wa watanzania, sio wote ila like 20% wanafanya vzr na wanazibeba saana taasisi wanazozifanyia kazi
Kama hao ndio wanatuendeshea maisha basi hizi shule za vipaji zifutwe, maana hakuna wizara au taasisi yenye ufanisi wa kuridhisha.. yaani zote tu ni ovyo, wanashindana kula rushwa tu na kufanya ufisadi.
 
Na

Kama hao ndio wanatuendeshea maisha basi hizi shule za vipaji zifutwe, maana hakuna wizara au taasisi yenye ufanisi wa kuridhisha.. yaani zote tu ni ovyo, wanashindana kula rushwa tu na kufanya ufisadi.
Hahahhaa
 
Huyu hajasoma physics. HIlo dude linakiuka kanuni za kifizikia. Hilo dude halifai kuwa helicopter bali try cycle, liwekewe injini ya piki piki.
Waafrika wenye hamu ya kubuni hawajui fizikia na wanaojua fizikia hawana hamu ya kubuni kitu.
Na mnaojua fizikia ndio kama wewe hapa ambao haujawahi hata kutengeneza hata piki piki ya makoa.😂

Na hiyo fizikia kwanza mliisoma kuijibia mitihani tu hili mfaulu vizuri, halafu mwisho wa siku mje mle mashavu kwenye serikali ya ccm.
 
Umeambiwa utaje innovation yoyote ya maana iliyoleta significant impact kwenye jamii iliyofanywaa na hao wahitimu wa shule zinazoitwa za "vipaji maalumu" kwa muda wa miaka 40 iliyopita, halafu wewe unaleta maelezo meeeengi ambayo hayana kichwa wala miguu.

Tunataka significant impact zilizofanywa na nyie mliosoma shule maalumu, na sio kututajia mifano sijui anayeendesha AI ya kiswahili sasa huyo nae kafanya gunduzi gani? Kubadilisha lugha au??? Mara sijui wanafanya kazi kwenye makampuni sasa ya nini yote hayo?

Binafsi mimi namuheshimu ntu aliyesoma Technical school kama Musoma tech, Moshi Tech.. n.k huko ndio angalau huwa tunawapata hawa akina mello

Ila nyie mliosoma sijui kibaha,mzumbe, ilboru hamna innovative skills zozote mnachojua nyie ni kushindana kupata division one ya point 3 tu baasi kisha baada ya hapo muende Udsm mwisho wa siku mnaishia kugaombania kazi za TRA au TANROAD
Hizo Innovation mnazani zinafanyiwa darasani? Hivi bajeti ya serikali yako kwenye vifaa za maabara za hizi shule ya serikali unaijua? Hivi Tanzania kuna research centers ngapi? Tanzania kuna library ngapi zinazo jitosheleza kwa vitabu?

Juzi tu hapa US Trump pamoja na maendeleo makubwa ya AI waliyo kuwa nayo ,ila kaweka zaidi ya USD bil 500,kwa ajili ya AI peke yako, wewe unazani kibongo bongo USD 500bil sawa na shillingi ngapi? Hapo bado hujaenda kuiona bajeti ya vitengo vingine kama Quantum Computer, Nuclear Physics, Cybersecurity,Maswala ya anga ?

Mnavyo ongelea gunduzi na Innovation mnazani zinakuja na kutokea kama Uyoga, research centers ya IBM ya maswala ya Quantum Computing, kujengwa gharama yake ni USD 5bil ,kama hamvijui hivi vitu bora mnyamaze.Hao madogo wenyewe final year project bajeti wanazopewa ni ndogo ,sometimes wanatumia mpaka hela yao ya bumu,tena unakuta kiproject hakizidi hata Tsh 1m.Youtube kuna story za gunduzi kibao na maswala ya Innovation fuatilieni ndipo mtaona ugumu wake.

Hayo matundu ya vyoo tuu yana tupelekesha,tena yanajengwa kwa msaada wa nchi za nje. Unapoona gunduzi au Innovation ya kitu chochote kaa ukijua billions of USD zimewekwa hapo, tena zaidi ya bajeti ya nchi yako.
 
Kuna nyakati fulani nilipata bingo la ufadhili wa miradi wa maendeleo la kaka $200k, ile pesa nilitaka nitenge nusu yake kisha nitafute graduates hata 50 kutoka SUA tufanye kilimo cha kisasa kabisa.. ila kuna mtu akaniambia niahairishe huo mpango
Huyo jamaa anakupenda sana.Mshukuru mno pale hakuna kitu mkuu Nina USHAHIDI wa kutosha kuhusu wahitimu wa pale.

Yupo niliekezwa na mzee kuwa niwe na mpigia ananipa ushauri wa kilimo maana ndo bwana kilimo wa kata Cha ajabu alipofika akaanza kushangaa Tena ikabidi nianze kumpa darasa
 
Kuna nyakati fulani nilipata bingo la ufadhili wa miradi wa maendeleo la kaka $200k, ile pesa nilitaka nitenge nusu yake kisha nitafute graduates hata 50 kutoka SUA tufanye kilimo cha kisasa kabisa.. ila kuna mtu akaniambia niahairishe huo mpango
Mwenzetu una connection nzito nzito
 
Kuna nyakati fulani nilipata bingo la ufadhili wa miradi wa maendeleo la kaka $200k, ile pesa nilitaka nitenge nusu yake kisha nitafute graduates hata 50 kutoka SUA tufanye kilimo cha kisasa kabisa.. ila kuna mtu akaniambia niahairishe huo mpango
Mkuu tueleze kwa kifupi kwanini uliachana na mpango huo?
 
Huyo jamaa anakupenda sana.Mshukuru mno pale hakuna kitu mkuu Nina USHAHIDI wa kutosha kuhusu wahitimu wa pale.

Yupo niliekezwa na mzee kuwa niwe na mpigia ananipa ushauri wa kilimo maana ndo bwana kilimo wa kata Cha ajabu alipofika akaanza kushangaa Tena ikabidi nianze kumpa darasa
Sio kwamba aliishangaa bali alikuwa anakupongeza kwa kuwa umefanya vizuri. Sasa wewe ukaanza kujiona una mzidi.
 
Back
Top Bottom