Tatizo sio shule bali waliozianzisha ndio ambao akili zao zinatia mashaka .
Huwezi kuanzisha vipaji maalumu bila kulenga ugunduzi na teknolojia .
Tulitegemea pawe na shule za Vipaji maalumu zenye Maabara na workshop za ufundi na masuala ya ugunduzi na vipaji maalumu katika ubunifu na Computer.
Cha ajabu shule hizi ni za kukariri tu hesabu na sio vipaji vya ugunduzi . Wengi wao hawawezi hata kuchunga mwiko au hata kutengeneza jiko la mkaa achilia mbali Kutengeneza masufuria kama wazee wetu wa zamani .
Hata kufinyanga chungu hawawezi lakini wanauwezo wa kukariri na kupata alama A zote.
Shule za Vipaji maalumu zilitakiwa ziwe ni vipaji vya kuzaliwa na sio kukariri kama Koran tu.
Walitakiwa wapimwe kwa ujuzi usio wa kawaida na uelewa wa kuzaliwa kabla hata ya kuingia kwenye mitihani. Mfano mtoto mwenye uwezo wa kufanya hesabu ngumu kwa kichwa bila kuandika n.k.
Lakini hii ya ufaulu wa A haitatuletea Wagunduzi hata wa baiskeli achilia mbali Cherehani za Kidigitali.
[/QUOTE
Mbegu zote mpya zinatoka kwa Wazungu.
Sio kweli.
SUA wanazalisha mbegu nyingi tu, Shida hawana Marketting strategy kama chuo, Kinachofanyika ni kuuza huo uvumbuvi kwa makampuni ya Mbegu hapa Bongo