Sema hii ngoma Harmonize aliandika tuache masihara

Sema hii ngoma Harmonize aliandika tuache masihara

Kuna NGOMA TUNDAMAN kaimba na HARMO_ BADMAN (MTU MBADI).

huu wimbo napenda kusikiliza Sana verse ya harmonizer..

Verse.
Ukienda kwa mganga ukitaja jina langu utaambiwa nimekufa / nimezikwa wewe weka matanga...Na utakula kitakacho pikwa.

Sisi tulisha penya Hadi.. TUNDU la sindano..lengo kutimiza ndoto na sio mashindano...
Sikuwahi kuizingatia, ila harmonize kwenye uandishi na melody katulia mnooo
 
Mkuu,

Nilikuwa nafikiri hivihivi lakini nikaona ngoja nikae kimya nisije kuambiwa nina bias.

Lakini, kwa sababu wewe umelianzisha hili, nataka kukuunga mkono.

Na kabla sijashambuliwa na mashabiki, this has got nothing yo do with talent.

Mimi naona kuna mambo ya management, exposure na mixing/arrangement ya muziki zaidi kuliko talent ya msanii.

Ujue wenzetu ndiyo maana wana watu wengi sana sana utaambiwa huyu producer, huyu mixer, huyu sound engineer, huyu arranger, halafu sisi tunachukulia poa mtu mmoja anaweza kufanya kazi zote hizo.

Yani unaweza kupiga ala zote sawa, ukaimba sawa, kashehe ikaja kwenye mixing and arranging chombo gani kianze, wapi chombo gani kiwe muted wapi, flow ya wimbo iendeje, bridge ikae wapi, chorus ikae wapi, harmony ikae wapi. Identity ya wimbo ijulikane kwa chombo kipi.

Hapo panahitaji utaalamu wa hali ya juu.
Nakuunga Mkono, ngoma nyingi sana za harminize zina mistari mikali, melody nzuri ila biti unaiona ipo ipo tu si kali si mbaya.

Niliacha kusikiliza muziki rasmi 2014 hiv mpaka 15, lakini siku niliisikia ngoma ya wote, huwezi amini niliisaka, nikaisikiliza kwa kuirudia rudia, ndio nikazikuta ngoma nyingine nilizoziorodhesha... Nikajikuta namtengenezea playlist na yeye.

Maana ngoma zangu nyingi ni za kitambo
 
Hii mwenyewe kuna verse sijui chorus anasema " basi kamata chupa fungua na mimina eeeeh, lewa tukuone unavyocheza kichina"
Kwingine anasema " tajiri na wanae masikini na mali zake, asiye na shida nawe muache aende zake:"
Sema Harmo akiacha bangi atakuwa mkali sana😁😁

Kaisikilize sasa
Aendelee kuvuta jani korofi ndio linaleta burudani zote hizo+kipaji,,Jani likikukubali lina hisia tamu katika kile ufanyacho
 
Duh! Siyo nzuri hiyo ina haribu akili
Kila Kitu Ni Kwa Kiasi Na Kwa Wakati Mamito,,Vyote Tutumiavyo Ukizidisha Tu Ni Either Uharibu Akili,,,Mwili Au Nafsi Au Vyote Kwa Pamoja Au Kimojawapo Kati Hivyo Au Viwili Kati Ya Hivyo Vitadhurika,,,Tujifunze Kuwa Na Kiasi Na Kufanya Vitu Kwa Kuzingatia Wakti Utafurahi Na Roho Yako Kipenzi Changu
 
Back
Top Bottom