Send off nzuri sana imefanyika ya binti anayejielewa kutoka familia inayojitambua. Hakuna kusumbua watu Michango

Sie tunaobebwaga na kadi za familia tumekutwa na jambo....yaani hakuna pa kujifichia!!
 
Mambo ya Fatma tumuachie yeye na familia yake...
 
Safi kabisa angalau naanza kuona mambo ninayoyapenda na mimi nitafunga ndoa na watu 20 tu nitaalika .
Ni uchoyo na ndoa yako haitapendeza itakuwa tu kama chakula cha jioni,
 
Jambo la ndoa na msiba ni swala la kifamilia hata zamani ilikuwa hivyo. Siyo mbwembwe kwa sababu hakuna hata mahali watanzania walivyo hodari wa kuiga,wameiga
Watu hulipa uzito usiostahili, sherehe za ndoa Sasa hivi hazitakiwi kuwa jambo kubwa sana. Wazazi au walezi wawaandae vijana wao na maisha halisi ya ndoa, siku hizi furaha ni kwenye sherehe tu ila wakishaoana baada ya mwaka vurugu huanza na mashtaka kibao, hivyo vijana waandaliwe kwenye maisha halisi ya ndoa.
 
Sherehe nyingi hazina uhalisia na kipato cha wahusika,ni michango ya watu,siyo jambo jema.Binti yetu alidumu kwenye ndoa miezi mitatu tu,kwa kweli ni aibu kubwa.
 
Tusiige mambo ya Wazungu, wao hufanya hivyo kwani kule watu hawana time na pia hakuna cha mambo ya shangazi, mjomba, jirani, nk, huku kwetu extended familu ipo na kuna watu wengi tu watakuwa wanajiona wametengwa.
Fanya ambacho kipo ndani ya uwezo wako hakuna haja ya kujiumiza au kusumbua watu na habari za michango
 
Mbona jina langu silioni hapo, na nilialikwa pia kuchangia?
Aaaah wee!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…