Sensa ya watu na makazi: Maswali ambayo hayakupaswa kuwepo kwenye dodoso

Kumbe upo mtupu hivi!!! Sikujua
Utupu uko wapi hapo? Uki calculate Human development index/Poverty Index kwenye research/Survey au Sensa tofauti Yao ni ipi?? Tofauti ni sampling tu kwamba sensa umechukua wote ila survey umechukua sample tu.

In fact kwenye research kama unafanya survey kwenye general population inaitwa SENSA. Sasa kama Una jibu tofauti na Hilo njoo unieleze utupu uko wapi hapo.

Tujifunze kujibu kwa hoja, matusi hayasaidii.
 
Hujui kitu, uliza tukupe darasa! Upo mtupu kijana. Panua ubongo kidogo, kama survey ni sawa na census! Kwanini nchi zote zifanye census wakati kila wakati wanafanya surveys ambazo gharama zake ni 0.1 ya gharama za sensa moja. Inaonesha hujui tofauti kati ya sample na population kitakwimu. Dogo kumbe Upo mtupu!
 
Hapa tunaongelea dodoso, nimeshasema dodoso la survey na sensa yote yanakua coded sawa, dummy variables zinatengezwa sawa hata reliability na validity ya hayo madodoso yanapimwa sawa tu.

2. Nimeshasema tofauti ya sensa na survey ni SAMPLE tu. Yaani ukihoji units zote kwenye population inaitwa SENSA ila ukiamua kuhoji representative sample ya population kama wanavyofanya TWAWEZA, au REDET n.k hiyo Inakua SURVEY. So tofauti ni hiyo tu ila mambo mengine yote ni same.

3. Hoja inasema maswali ya Brenda, Feni n.k ni ujinga na ndio mzizi wa mada. Nikaeleza kwamba Kupima Poverty Index au Human Development Index Kila swali pale linakua na value kulingana na code yake, yaani ukibonyeza kitufe cha YES or NO kule haziingii YES/NO zinaingia value kama ni 1 to 10. So mtu akisema anamilikia nyumba kule inatick 10/10, akisema Brenda inatiki say 3/10 so baadae inapigwa average kujua ratio ya umaskini/Utajiri wa mtu kulingana na Umiliki/access wa vitu kadhaa.

Sasa hizo index zinapigwa hesabu same kwenye survey na sensa zinapigwa hivyo hivyo ndio kitu nilichoeleza hapa in that sense DODOSO LA SENSA NA SURVEY YANAFANANA.

Mimi nafanya shughuli za Research na nimeandaa, sambaza, kusanya, na kuanalyse madodoso sana tu so naongea kama practitioner so elewa nachokwambia. Kuleta ujuaji wakati mtu hujafanya hizi kazi uta mislead watu humu!!
 

Hujui kitu wewe! Tukufundishe Sampling errors! Unalingalisha population na samples wewe kiazi. Unajua a true representative sample wewe. Je kuna true representative hapa duniani wewe? Unadhani wewe unanashabihiana 100% na mtu mwingine? Unajua uniqueness. After all hujui probability sampling hivyo unadakia tu! Mtu anayefananisha data ya sensa na data ya survey ni kiazi tu
 
Hakika, kuna maswali mengine yakuchoshana tu...

Unashindaga wapi... Hua nashindaga kwa @Beesmom
Hakika yamechosha Sana,nilichoka pale walipouliza Smart911 akishinda kwako huwa mnafanya nn......nami nikawajibu yeye ni mwanaume Mimi mwanamke Ivo hatufanyi kitu🙄 nikasahau Kumbe hata ingekuwa mwanaume Kwa mwanaume bado wanaweza fanya kitu 😜
 
Jirani umenichekesha sana...
 
Kama kiingereza tu kinakushinda hizo "sampling errors" utaweza nifundisha? Tuheshimiane kijana, huna Elimu Wala ujuzi wowote wa kunifundisha kuhusu research!!

Nmeshakuambia tofauti ya sensa na survey ni SAMPLE sasa unaruka ruka mada za nini? Kutaja terminology za sampling ulizokariri form 1 basi unadhani ndio ntakuona Unajua research?

Nyie ndio mnashusha hadhi ya JF, mnaleta ujuaji wakati shule hamna, kajifunze kwanza lugha ndio urudi kujadili mada za kitaaluma.
 

Source: EU
 
Mbona sikuulizwa swali la waliokufa maana kama wangeuliza lazima la lini walikufa lingefuata.
Mimi nakumbuka walikuwa wanauliza vifo vya watoto waliozaliwa wafu na hili swali lilimlenga mwanamke iwapo alishapoteza mtoto wakati wa kuzaa.

Kuna Data nyingi za mtu zinaweza kupatikana NIDA hivyo tunategemea kwa kuingiza namba ya NIDA katika mfumo data nyingi zinaweza kuunganishwa NBS kupunguza maswali.
 
Huoni hapo kuwa wewe ni kiazi. An estimation (introducing a factor) is just an estimation young man!!!! Huwezi kuilinganisha na actual (census data). Umeelezwa survey data (using part of the population-sample) si sawa na kutumia actual population. Wewe ni kiazi tu, haya mambo unayasikia wakati sie tumebobea dogo
 
Tatizo lugha mkuu inakupa shida, nimekuwekea hapo uone kwamba tofauti ya sensa na survey ni SAMPLE sio kingine. Ukichukua data kwa SAMPLE ya watu wachache kwenye population inaitwa SURVEY ila ulichukua data kutoka Kwa watu WOTE kwenye population husika inaitwa CENSUS.

Sasa wewe unataka kupotosha kitu Gani hapa? Questionnaire ya census na survey Zina tofauti Gani? Ku-code maswali ya questionnaire na Census Yana tofauti Gani? Ku calculate poverty index kwenye survey na census Ina tofauti Gani?

Alafu census haimaanishi watu hapana hata ukihoji makampuni yote ya Mabasi unaita CENSUS sio SAMPLE!!
 
Tatizo ndo liko hapo. Kuchanganya nazaria na hali halisi. Kama una deal na population, sample iwe representative au la, ya nini? Hiyo sensa si ingetoa majibu yote kwa usahihi zaidi? Magharama si yangepungua? Unafanya sensa wk 1 na inayofuata unakuja na hiyo survey, kweli! Ni kweli takwimu sio ugali kwamba kila mtu anakula lkn pia kusomea takwimu haikufanyi kujua jinsi ya kupanga, inakufndisha kutafsiri takwimu. Unaulizia baskeli, sio bodaboda, namba ya luku sio ya mita ya maji, ekari ngapi sio kampuni ngapi! Kujua sampling technique sawa, lkn maswali mengne kama vile ya kitoto! Yanatuongezea tozo. Kila la heri mtaalam wetu
 
Sensa mbona fresh tu mi walipokuja niliwaambia nina muda mfupi basi walinihoji kwa ten minutes tu hayo maswali mia wanayodai raia sikuulizwa na binafsi sioni faida ya Sensa ikiwa hakuna uwiano mzuri wa revenue collected kupitia matozo yaliyotuzidi uwezo wa kuyalipa katika matumizi ya maendeleo (miundombinu) na matumizi ya sirikali (ununuzi wa V8 za viongozi )

Sorry guys mi kwangu sensa haina faida. Wananchi wengi ni maskini tangu uhuru , ajira hakuna kwa vijana tangu uhuru, vijana kukamatwa uzururaji tangu uhuru, barabara za vumbi tangu uhuru, huduma mbovu za afya tangu uhuru, maji hakuna tangu uhuru, umeme sijui mgao tangu uhuru miaka sijui mingapi nchi nyingi maskini zimeipiku bongo, mi kwangu naona wananipigia makelele tu fedha wanayokusanya hainisaidii, elimu duni tangu uhuru , tuondoleeni sijui Ujamaa my foot, weka English as medium of instruction kuanzia primary school ndo nitawalewa!maana tutaongeza wawekezaji kutoka nje na nchi itapaa kiuchumi fasta!

Kuna kitu kinaitwa "Social contract theory" huko duniani uzunguni ni kitu cha kawaida mtaani kila mtu anajua, siku wabongo wakijua hilo hapatakalika, yani ni hivi kwanza hakuna mikutano ya kampeni za uchaguzi , kura ni mkataba tunafunga nione lami sio V8 , nisipoona lami uchaguzi ujao napigia kura chama kingine hiyo ndo iko ulaya watu hawacheki , kwenye kampeni mtaani wanakuwekea meza ina matunda uchague Karoti au Apple! unachochukua kula ndo chama utakachopigia kura, watu wako serious miaka mitano wanafuatilia matumizi ya tozo zao na ukizingua uchaguzi ukifika wanaambiana wanakula kichwa!

Viongozi wa bongo Mungu amewapenda sana amewapa nafasi ya kutawala raia maskini, raia waoga, raia wasiojua haki zao, raia wasio na elimu ya uraia wala tozo, hongera sana kwao Matozo Government!

naunga mkono hoja wanatusumbua tu!
 
Hujui kitu. Nikueleweshe! Utafiti uliotimilika ni sensa ambayo inapata data kutoka kwa watu au vitu vyote unavyotafiti. Sababu kuu ya mfano kupata data za watu wote au vitu vyote ni kwa vile hatufanani (we are not homogeneous in nature). Lakini njia hii ni ya gharama sana kama ulivyoona katika sensa ya watu na makazi au hii inayoendelea ya Majengo. Mfano Twaweza katika utafiti wao ingefaa kama wangeliuza watanzania wote kuhusu Tozo, tungepata jibu la uhakika, ila kuuliza watu wote ni ghali na hizo pesa hawana. Hivyo wanajaribu kupata wawakilishi ili majibu ya hao wawakilishi yawe kama representative ya watu wote. Hapo ndipo siye watakwimu tunaingia (sampler)!

Turudi katika hoja ya msingi, huwezi aminisha watu kuwa sensa ni sawa na survey! La hasha maana survey unatumia uwakilishi na katika hali ya kawaida uwakilishi haupo. Mfano tunaambiwa wabunge ni wawakilishi wetu, Hivi ni kweli wanayoongea bungeni huwa tunawatuma au wanatumia vichwa vyao! Aidha Faida kuu ya sensa ni kupata idadi ya watu (enumeration) ili itumike kama denominator ya kila calculation inayotumika. Mfano katika kutafuta asilimia au uwiano. Tukisema ni asilimia kadhaa ya Watoto wamechanjwa, numerator (ile namba ya juu) itapatikana kwa mchanjaji na ya chini ambayo ni denominator inatoka katika data za sensa. Pahala ambapo hakuna data za sensa utasikia wamechanjwa asilimia Mia moja na kumi (Upuuzi mtupu) ni kutumia maoteo ya survey yanapotosha.! Una la ziada?
 
Kizuri (perfection) ni gharama! Kuna gharama huwezi kukwepa.
 
Hivi ile,kama nyumba ni yako..unaweza kuiuza kwa kiasi gani,hilo ndo limenishangaza sana.

Wameomba hadi meter number.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…