Uchaguzi 2020 Sera ya majimbo itaua utaifa na uzalendo

Uchaguzi 2020 Sera ya majimbo itaua utaifa na uzalendo

Sera ya Majimbo mimi kwa uelewa wangu ni sawa na familia ya baba na mama ambao wamefanikiwa kuwa na watoto na wajukuu... Ishara na kitovu cha ugatuzi wa madaraka!

Kila mtoto/mjukuu atakua nae ataanzisha familia yake "jimbo lake".
Serikali kuu kama baba na mama... Serikali za majimbo kama uzao wao...!! Na uhusiano/ushirikiano unaendelea vizuri tu!
Kuna mambo mengi muhimu tu ya kuendelea kutegemea kutoka kwa baba na mama... Lakini kuna mengine mengi tu ambayo kila jimbo linatakiwa liwajibike kuyamaliza...

Common sense inaelekeza kuwa mtu mzima kuendelea kumtegemea baba na mama kwa kila jambo ni udumavu wa akili na maendeleo...!! Ebu fikiria kama inaingia akilini baba na mama ndo wakupangie ama wakuamulie kila kitu kwenye maisha yako ndani ya jimbo lako...

Kama binadamu walivyo na changamoto; mfumo wa majimbo nayo lazima utakuwa na changamoto zake... Jukumu letu ni kuzibaini changamoto na kuzitatua ipasavyo...

Itoshe tu kusema kuwa faida za majimbo kwa "linchi likubwa" kama Tanzania ni kubwa kuliko hasara zake...!
Mfumo wa sasa ni wa kikoloni na kinyonyaji! Ebu fikiria juzi kwenye kampeni JPM kafika eneo fulani alafu anampigia Jafo simu atume pesa ili ikafanye kazi ya kukamilisha barabara...!! Ni wazi kuwa wale wananchi wangelimaliza lile tatizo wenyewe Kama lingekuwa ndani ya uwezo wao bila kumsumbua Jafo/JPM ambao hakuona umuhimu wa kulimaliza kabla...

Yaani uzalishaji tufanye sisi... kodi tulipe sisi alafu maji ya matope tunywe sisi...na wewe hadi ujisikie ndo utupatie ufumbuzi... Kwingineko tunaambiwa kuwa tutaendelea kukosa maendeleo kisa hatuchagui kama unavyotaka wewe...

Yaani viongozi wote uwalete wewe.... Why tukaliwe kiasi hiki...!!

Woga wetu ndo kikwazo cha maendeleo yetu...!!!
 
Acha kubisha kitu usichokifahamu mkuu tafuta habari ziko mtandaoni, AU haina jeshi rasmi, ila ukitokea mzozo wa kundi fulani kugawa nchi, kila mwanachama wa AU atatoa wanajeshi wake kwenda kupambana na kundi la uasi!
Wewe ndio huelewi unadandia manbo juu juu. Yale majeshi ya Tanzania yaliyoko Kongo nani anagharamia? Kule Somalia nani anagharamia yale majeshi ya Afrika? Au unafikiri ni suala la kuchanga majeshi tu? Africa nzima haina uwezo wa kuendesha operesheni yeyote kijeshi bila kugharimiwa na mataifa nje ya Afrika financially, logistically na kwa vifaa.

Soma vizuri hoja yangu halafu ndio ujibu.
 
Mfumo wa Majimbo utakuwa na athari hasi kwa Muungano wetu tuwe makini
 
Sera ya Majimbo mimi kwa uelewa wangu ni sawa na familia ya baba na mama ambao wamefanikiwa kuwa na watoto na wajukuu... Ishara na kitovu cha ugatuzi wa madaraka!
Kila mtoto/mjukuu atakua nae ataanzisha familia yake "jimbo lake".
Serikali kuu kama baba na mama... Serikali za majimbo kama uzao wao...!! Na uhusiano/ushirikiano unaendelea vizuri tu!
Kuna mambo mengi muhimu tu ya kuendelea kutegemea kutoka kwa baba na mama... Lakini kuna mengine mengi tu ambayo kila jimbo linatakiwa liwajibike kuyamaliza...
Common sense inaelekeza kuwa mtu mzima kuendelea kumtegemea baba na mama kwa kila jambo ni udumavu wa akili na maendeleo...!! Ebu fikiria kama inaingia akilini baba na mama ndo wakupangie ama wakuamulie kila kitu kwenye maisha yako ndani ya jimbo lako...
Kama binadamu walivyo na changamoto; mfumo wa majimbo nayo lazima utakuwa na changamoto zake... Jukumu letu ni kuzibaini changamoto na kuzitatua ipasavyo...

Itoshe tu kusema kuwa faida za majimbo kwa "linchi likubwa" kama Tanzania ni kubwa kuliko hasara zake...!
Mfumo wa sasa ni wa kikoloni na kinyonyaji! Ebu fikiria juzi kwenye kampeni JPM kafika eneo fulani alafu anampigia Jafo simu atume pesa ili ikafanye kazi ya kukamilisha barabara...!! Ni wazi kuwa wale wananchi wangelimaliza lile tatizo wenyewe Kama lingekuwa ndani ya uwezo wao bila kumsumbua Jafo/JPM ambao hakuona umuhimu wa kulimaliza kabla...
Yaani uzalishaji tufanye sisi... kodi tulipe sisi alafu maji ya matope tunywe sisi...na wewe hadi ujisikie ndo utupatie ufumbuzi... Kwingineko tunaambiwa kuwa tutaendelea kukosa maendeleo kisa hatuchagui kama unavyotaka wewe...
Yaani viongozi wote uwalete wewe.... Why tukaliwe kiasi hiki...!!

Woga wetu ndo kikwazo cha maendeleo yetu...!!!
Tayari mmechafuka kwa hiii sera ya majimbo, bora mjitoe tu uchaguzi hamtaaminiwa tena. Mmeatamia jiko la moto, ukiatamia jiko la moto litakuunguza tuuu, hata lisipokuunguza kama halina moto litakuchafua kwa majivu.Poleni wana chadema siasa ndiyo hiyo. JIANDAENI NA UTETEZI MWINGINE KWA SERA YENU YA KUWEKA DHAMANA MALI ZA NCHI ILI MUWEZE KUKOPA.Hahahahahaha mwaka huu mnalo.

Sasa hivi ccm wanawabomoa kwa sera zenu mlizotunga wenyewe.Inaonekana zilitengezwa na wazungu mkapewa kwenye bahasha bila ku proof read. Yaani ccm sasa hivi wanabonyeza kitufe cha sera za chadematu kitu kinalipuka
 
Tunaomba aliye na ilani ya chadema aiweke humu, mgombea wa ccm ndugu Magufuli katushauri tuisome tushangae yaliyomo
 
Tayari mmechafuka kwa hiii sera ya majimbo, bora mjitoe tu uchaguzi hamtaaminiwa tena. Mmeatamia jiko la moto, ukiatamia jiko la moto litakuunguza tuuu, hata lisipokuunguza kama halina moto litakuchafua kwa majivu.Poleni wana chadema siasa ndiyo hiyo. JIANDAENI NA UTETEZI MWINGINE KWA SERA YENU YA KUWEKA DHAMANA MALI ZA NCHI ILI MUWEZE KUKOPA.Hahahahahaha mwaka huu mnalo.

Sasa hivi ccm wanawabomoa kwa sera zenu mlizotunga wenyewe.Inaonekana zilitengezwa na wazungu mkapewa kwenye bahasha bila ku proof read. Yaani ccm sasa hivi wanabonyeza kitufe cha sera za chadematu kitu kinalipuka
Tumechafukwa kivipi wakati watanzania wanaiunga mkono sana???
 
Kwahiyo Wamarekani hawana utaifa wala uzalendo au?
China Japan South Africa Uk kote wanatumia mfumo wa majimbo ambao ni vigumu Serikali kuu kuchukua pesa za jimbo kienyeji kufanya mambo yasiyo na tija kama CCM walivyofanya kununua Ndege kujenga chato Airport kienyeji pasipo idhini ya bunge
 
Kwahiyo Wamarekani hawana utaifa wala uzalendo au?
Jimbo moja tu la Texas lina ukubwa sawa na Tanzania.

Atakayekuja na wazo la kuiunganisha afrika ikawa ni nchi moja yenye sarafu moja, huyo atakuwa na nia ya kuigeuza Tanzania ikawa ni jimbo mojawapo kati ya majimbo ya Afrika.
 
China Japan South Africa Uk kote wanatumia mfumo wa majimbo ambao ni vigumu Serikali kuu kuchukua pesa za jimbo kienyeji kufanya mambo yasiyo na tija kama CCM walivyofanya kununua Ndege kujenga chato Airport kienyeji pasipo idhini ya bunge

Kununua ndege ni jambo halina tija?..mkuu naona umechafukwa.

Hao uliowataja misingi ya mataifa yao haifanani na misingi ya kwetu. Wengine walipigana vita hivyo hayo majimbo yao hayakuibuka tu.
 
SWALI NI: JE, MFUMO WA MAJIMBO UTALETA UKABILA NA KUFANYA BAADHI YA SEHEMU TANZANIA KUTOKUWA NA MAENDELEO?

Amani iwe nanyi wadau!

Leo napenda kuwajibu wana CCM wanaosema mfumo wa Majimbo utachochea ukabila na kusababisha baadhi ya maeneo kutokuwa na maendeleo,

Ukweli ni kuwa kamwe mfumo wa majimbo hautaleta ukabila na kamwe hautoleta kudumaa kwa maendeleo kwenye baadhi ya sehemu kama propaganda za CCM zinavyosema! Hii ni kwa sababu zifuatazo;

1. Jimbo la Kati- Mikoa ya Dodoma, Singida na Tabora na Morogoro.
Mikoa hii ina utajiri mkubwa wa mazao kama Tumbaku, Zabibu, Alizeti, Karanga, Asali na Mtama, Mpunga,Ndizi na Mahindi(vya mkoa wa Morogoro) Haya mazao tukipata viongozi wenye akili sio hawa wa CCM yataendelezwa vizuri na kuingiza mapato makubwa kwenye jimbo hili la kati.

Kuna uhitaji mkubwa sana wa Karanga na Asali kwenye masoko ya Asia na Ulaya. Haya mazao yakiendelezwa kisasa na kibiashara jimbo hili litanyanyuka mno kiuchumi. Hata viwanda vya mvinyo tu Dodoma vikiendelezwa na kutangazwa vizuri na mvinyo ukitengenezwa mzuri mapato

Pia kwenye jimbo hili kuna maliasili mbalimbali za wanyama kutokana na mapori ya akiba kama swagaswaga, manyoni na mapori ya Tabora ambayo pia yana tembo wengi na mbao nyingi. Hivi vitu vikiendelezwa na kutangazwa vizuri vitakuwa source kubwa ya mapato kutokana na uwindaji na utalii. Haya pia ni mapato makubwa sana.

Mkoa wa Morogoro una mbuga za wanyama kama mikumi, udzungwa na nyingine nyingi ambazo pia zitaleta mapato ya utalii.

Pia Kuna madini Kama dhahabu mikoa ya Tabora na Singida na Morogoro ambayo yakiendelezwa vizuri yataketa mapato makubwa sana kwenye maeneo haya. Hapo sijaweka biashara za mifugo, wanyama na viwanda ambavyo navyo vipo na vitakuwepo kwenye jimbo hili.

Kwa hiyo dhana ya Jimbo la Kati kuwa masikini si kweli.

2. Jimbo la Mashariki- Mikoa ya Dar es Salaam, Tanga na Pwani
Jimbo hili chanzo kikuu cha Maputo kitakuwa Bandari, Viwanda na Biashara. Kodi nyingi itakusannywa kutoka maeneo haya na kwa kweli itaendeleza kweli jimbo hili.

3. Jimbo la Kusini- Mikoa ya LINDI, Mtwara na Ruvuma
Jimbo hili lina utajiri mkubwa wa gesi na mazao ya korosho na mbaazi bila kusahau viwanda, bandari na uvuvi. - Hili jimbo litakuwa na na mapato makubwa sana ambayo yatajenga shule bora, hospitali, madawa, kujenga barabara nzuri na makazi bora.

Pia jimbo hili litakuwa na mapato ya utalii kutokana na hifadhi ya Selous na mapori ya akiba ya mkoa wa Ruvuma.

4. Jimbo la Nyanda za Juu kusini- Mikoa ya Iringa, Njombe,Songwe na Mbeya
Jimbo hili ndo mzalishaji mkuu wa chakula kinacholisha Tanzania, Afrika ya kati na Afrika mashariki. Kilimo na Biashara ya Chakula kitaingiza mapato makubwa sana kwenye jimbo hili. Biashara pia ya mbao na utalii kutokana na hifadhi za kipengele, Ruaha, Kitulo na Rungwe vitaingiza mapato makubwa sana kwenye jimbo hili.

Mipaka ya Zambia na Malawi pia itaingiza mapato makubwa kutokana na biashara bila kusahau viwanda na kilimo cha mashamba makubwa ya mpunga, maparachichi, nyanya, chai na miti.

5. Jimbo la Magharibi- Mikoa ya Katavi, Rukwa, Kigoma na Kagera- Mikoa hii ina utajili wa kilimo hasa cha mazao ya mahindi, tumbaku, mawese, miwa pamoja na miti pia. Pia ina uvuvi wa maziwa ya Tanganyika na Victoria.

Mikoa hii pia ina utalii wa mbuga za wanyama kama hifadhi za Gombe, Kimisi, Katavi, Mto Maragarasi pamoja na biashara kubwa na kodi katika mipaka ya nchi za Congo( Bandari) , Burundi, Rwanda na Uganda! Itoshe tu kusema kuwa jimbo hili pia litakuwa na mapato mengi sana ambayo yataboresha miondombinu ya barabara, hospitali , mashule na huduma za Maji safi na salama!!

6. Jimbo la Kaskazini- Mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Manyara na Mara.
Jimbo hili litakuwa na na chanjo kikuu cha mapato ambacho ni utalii na pia madini ya mikoa ya Arusha, Manyara na Mara. Utalii wa mbuga za kilimanjaro, Ngorongoro, Serengeti na Manyara utaingiza pesa nyingi sana za kuboresha miondombinu na huduma za msingi

Biashara pia na kodi kwenye mipaka ya Kenya kwa sehemu za holili,Silali na Arusha italeta mapato mengi Sana. Na hapa hujaweka kilimo cha ndizi, tangawizi na mifugo bila kusahau viwanda.

7. Jimbo la Kanda ya Ziwa (Victoria)- Mikoa ya Simiyu, Geita, Shinyanga na Mwanza.
Jimbo hili ndo kitovu cha madini Tanzania. Pia lina mbuga na mapori ya akiba mengi bila kusahau viwanda na biashara ambavyo vitaingiza napata mengi sana na kuleta impact kubwa sana kwenye uchumi. Uvuvi pia utaleta mapato mengi sana.

Dhana ya ukabila haiwezi kupata nguvu kwenye mfumo huu kwa sababu Kuna mchanganyo mkubwa wa makabila kwenye majimbo haya!

Pia chini ya mfumo huu kila mwananchi atawajibika kufanya kazi halali na kujituma kwa sababu atajua bila kufanya kazi hawezi endelea na sehemu yake haiwezi kufanya vizuri katika huduma za msingi.

Chini ya mfumo huu pia hakutakuwa na unyanyasaji wa wananchi kwa sababu wananchi watakuwa wanajua kuwa Mapato yao ndio yatakayowaletea maendeleo!

Viongozi pia watawajibika moja kwa moja kwa wananchi na kamwe hawatofuja mali kwa wananchi wala kuwagawa kwa misingi ya kikabila au kichama kwenye maendeleo.
Mfumo wa majimbo ni bora zaidi ya mfumo tuliokuwa nao sasa wa kuwa na RC ambao ni mfumo wa hovyo usio na tija ndiyo maana mpaka sasa Tanzania ina miaka 59 haina maendeleo pesa zote za viwanda zinatumika kudhoofisha chadema kuua upinzani kuhujumu kukandamiza demokrasia badala ya maendeleo
 
Mfumo wa majimbo ni bora zaidi ya mfumo tuliokuwa nao sasa wa kuwa na RC ambao ni mfumo wa hovyo usio na tija ndiyo maana mpaka sasa Tanzania ina miaka 59 haina maendeleo pesa zote za viwanda zinatumika kudhoofisha chadema kuua upinzani kuhujumu kukandamiza demokrasia badala ya maendeleo
CCM wengi hata hawaelewi ukiwauliza mfumo wa majimbo ukoje Yaani wamekaririshwa tu na ukilaza wao. Wengine wanaamini Majimbo ya wabunge ndo yatakuwa majimbo wengine wanasema Eti Mkoa ndo utakuwa jimbo, yaaani ni vilaza watupu 😂😀😀
 
Kununua ndege ni jambo halina tija?..mkuu naona umechafukwa.

Hao uliowataja misingi ya mataifa yao haifanani na misingi ya kwetu. Wengine walipigana vita hivyo hayo majimbo yao hayakuibuka tu.
Ndege zikinunulia kwa mfumo bora kwa bei nafuu huleta tija lakini kununua Ndege kwa cash huku wajanja wachache wakiwa na 10% humo ni ufisadi na ununuzi wa Ndege wa aina hii hauna tija kwani Ndege hazitengenezi faida sana sana zimekuwa mziko kwa Taifa
 
CCM wengi hata hawaelewi ukiwauliza mfumo wa majimbo ukoje Yaani wamekaririshwa tu na ukilaza wao. Wengine wanaamini Majimbo ya wabunge ndo yatakuwa majimbo wengine wanasema Eti Mkoa ndo utakuwa jimbo, yaaani bi vilaza watupu 😂😀😀
Ha ha ha CCM watajifunza kupitia South Africa inatosha au wajifunzie kenya basi
 
Tayari mmechafuka kwa hiii sera ya majimbo, bora mjitoe tu uchaguzi hamtaaminiwa tena. Mmeatamia jiko la moto, ukiatamia jiko la moto litakuunguza tuuu, hata lisipokuunguza kama halina moto litakuchafua kwa majivu.Poleni wana chadema siasa ndiyo hiyo. JIANDAENI NA UTETEZI MWINGINE KWA SERA YENU YA KUWEKA DHAMANA MALI ZA NCHI ILI MUWEZE KUKOPA.Hahahahahaha mwaka huu mnalo.

Sasa hivi ccm wanawabomoa kwa sera zenu mlizotunga wenyewe.Inaonekana zilitengezwa na wazungu mkapewa kwenye bahasha bila ku proof read. Yaani ccm sasa hivi wanabonyeza kitufe cha sera za chadematu kitu kinalipuka

Yaani mshukuru kuwa waTanzania mmewafanya mazezeta waamini katika ahadi zenu hewa miaka nenda rudi hata katika yale yaliyo haki kwao...

Siku wakizinduka mtabaki historia...
Hizo Sera za CDM zinatekelezeka kuliko za zilizofeli tokea nchi ipate Uhuru... Ndo maana mnaahidi hiki mnatekeleza msiyoahidi...

Hao wazungu msiowataka kila leo mnawainamia na kuwasujudu wawasaidie...
Shame on you bigots; rubbish pits!
 
Usione vyaelea. Unajua imewagharimu kiasi gani kufika hapo walipo?.
Kwahiyo unataka rais aendelee kuwa ndiyo mgawa riziki ktk mikoa? Tunatka madaraka yarudi kwa wananchi.
 
Nimesikia chama kimoja kinazungumzia nchi kuigawa kwenye majimbo ya kiutawala na uendeshaji. Kwangu mimi kwa nchi ambayo imekuwa kwenye utawala wa mikoa kwa miaka zaidi ya 50 na kwa mfumo wa kugawana mapato kupitia serikali kuu na serikali za mitaa kwa baadhi ya mapato haileti mantiki kubadili mfumo kwenda kwenye majimbo ambayo yanaweza kuua utaifa na kuleta mfarakano. Mfumo wa sasa unaondoa u-mimi na maendeleo ya uchumi yanayopishana- Regional economic imbalances - ambao utaacha baadhi ya maeneo kwenye umasikini mkubwa. Baadhi ya athari zinazoweza kujitokeza ni pamoja na:

1. Maeneo yenye raslimali kidogo kuendelea kuwa maskini na maeneo mengine kuwa tajiri na hivyo kuwa na mchango mdogo wa GDP

2. Ajira ndogo kwenye baadhi ya maeneo yenye raslimali chache na hivyo ongezeko la idadi ya watu kwenye maeneo yenye utajiri wa raslimali

3. kila jimbo kuwa na sheria zake za kiutawala, bunge dogo, polisi nk hali inayoweza kujenga mwelekeo wa kujitenga. Rejea matatizo yakujitenga kwa Biafra Nigeria miaka ya nyuma.

4. Nchi zenye majimbo mf Msumbiji hazina hakikisho la maendeleo endelevu kuzidi ambazo hazina utaratibu huo ie Tanzania

5. Mfumo huo utakuwa na gharama kubwa kuuanzisha

Kimsingi hadi sasa mfumo uliopo hauna shida changamoto kubwa ni kuweka mifumo mizuri ya udhibiti matumizi na mapato ya serikali kwa kuyagawa kwa haki ili kila eneo la serikali liweze kunufaika. Na hususani kuimarisha mfumo wa Halmashauri uweze kukabiliana na changamoto za kiuchumi kwa kila eneo. Iwapo kuna changamoto za mgawanyo sawia basi tupitie upya sera na sheria zetu ndani ya mfumo uliopo tuboreshe.

6. Hata hivyo, Kwa maoni yangu badala ya utawala wa majimbo ni afadhali kuweka kanda za kiuzalishaji ili kuchochea uchumi wa kimaeneo kulingana na mazingira ya kiuchumi na uzalishaji kwa kila eneo.
Rais anateua wakuu wa mikoa,wakuu wa Wilaya, wakurugenzi wote wa Halmashauri,makstibu wakuu,mabalozi, mawaziri nk nk. Tunachotaka wakuu wa mikoa na wakuu wa Wilaya wagombea na kupigiwa kura Kama wabunge.
 
Salamu kwako Tundu Antiphas Lissu, Shalom,

Leo napenda kukwambia rasmi kuwa , Kura yangu iko kwako! Na hii ndo sababu yangu kuu ya kukupa kura!

Katika maisha yangu nimekuwa nikifanya utafiti sana juu ya dhana ya umasikini wa watanzania na Tanzania kwa ujumla, Moja ya sababu ambayo niligundua kwenye utafiti wangu ni kuwa Tanzania tuna mfumo mbovu sana wa utawala ambao vyovyote vile hatuwezi kuendelea kwa mfumo huu!

Mfumo huu ninaousema ni mfumo kuwa fedha zote za watanzania zinakusanywa na kuwekwa chini ya mtu mmoja( raisi ambayo yeye ndo anayeamua kuwa hizo fedha zigawanywe kivipi)

Madhara ya mfumo huu ni kuwa umeondoa uwajibikaji kwa wananchi na viongozi, umeondoa ubunifu kwa wananchi na viongozi na mwisho umepelekea tabia ya ombaomba na unafiki kwa wananchi na viongozi

Mfumo huu pia umechochea ufisadi wa kiwango kikubwa sana kwa wananchi na viongozi na kama Kuna mtu anabisha Leo hii aniambie maisha ya ukwasi wanayoishi maraisi wastaafu yametokana na nini???

Hapa Tanzania hakuna raisi mstaafu mwenye maisha ya utajiri wa kuwaida. Wengi wana utajiri mkubwa wa real estate, kilimo kikubwa na hata pia makampuni makubwa ya uzalishaji. Na kibaya ni kuwa vyote hivi huwa wanavipata wakiwa maraisi. Sababu ya haya yote ni kuwa tumekuwa na mfumo wa kuziweka fedha zote za nchi chini ya mtu mmoja.

Leo hii raisi ni kama Mungu hapa Tanzania. Kila aendapo watu ni kulia shida, awafanyie hiki na awaletee hiki, haya yote ni kwa sababu ya mfumo mbovu tulionao ambao umeondoa uwajibikaji na ubunifu kwa watanzania na viongozi wetu

Kwa nini Mfumo wa Majimbo ndo suluhisho wa haya yote?
1. Mfumo wa majimbo utafanya hela zote zinazokusanywa kwenye sehemu husika zitumike kwa matakwa ya wananchi wa sehemu husika mf. Kujenga barabara , hospitali, shule bora na huduma bora za Maji na umeme!! Hili litafanya wananchi wasiwe wajinga kwa viongozi wao na kamwe was iwe ombaomba na watu wa kujipendekeza kwa viongozi wao.

2. Mfumo wa majimbo utachochea ubunifu kwa wananchi kufanya shughuli mbalimbali bora za uzalishaji ili majimbo yao yakusanye fedha za kutosha kwa ajili ya maendeleo yao.

Kama jimbo husika linategemea kilimo basi wananchi wa hilo jimbo watafanya kilimo bora na watakifanya cha biashara ili wapate mapato mazuri ya kuendeleza jimbo lao kimiundombinu na Pia kimaendeleo. Hakuna sehemu watu watalala au kuwa wazembe na watakuwa wakali kwa viongozi wao kuwahamasisha wawe agressive kwenye kubuni miradi bora ya maendeleo kwa maendeleo yao.

Mfumo huu utatengeneza wananchi wanaojiamini na Kuwajibika kweli katika kutunza rasilimali zao ili ziwasaidie wao na uzao wao. Wananchi hawatakuwa wazembe na watawawajibisha kweli viongozi wasio wabunifu kwenye kutengeneza vyanzo vya mapato kwa sababu watakuwa wanajua bila vyanzo vya mapato bora na vya uhakika kwenye maeneo yao basi watakuwa nyuma kimaendeleo na hawataweza kunsurvive.

Mfumo wa majimbo utafanya kama sehemu Kuna mbuga za wanyama basi wananchi wa maeneo husika wazitunze rasilimali kweli kwa sababu watajua kweli bila mbuga hizo utalii utakufa na hawatapata mapato ya kulipa mishahara wafanyakazi wao, kujenga barabara na mitaa bora, kuhudumia Bima za afya na madawa hospitali. Kwa iyo Kama jimbo litategemea utalii basi watautunza na kuuthamini kweli utalii.

Kama jimbo linategemea viwanda au biashara basi jimbo hilo litatunga Sera bora ili kuhamasisha uwekezaji mkubwa wa viwanda na biashara kwa sababu wananchi wa sehemu husika watajua bila hivyo basi hawawezi pata mapato ya kununulia dawa, kupata Maji safi na salama na kujenga barabara nzuri!

Kama jimbo husika linategemea kilimo na migodi basi wananchi wa viongozi wa maeneo husika wataumiza kichwa kuweka Sera bora katika hayo maeneo ili kuhakikisha zinawapatia mapato makubwa ya kufanya miradi ya maendeleo. Watu watajiona kweli kuwa wao ni sehemu sahihi ya maendeleo husika.

Imefika wakati watanzania lazima tuseme kuwa mfumo wa utawala wa Chama cha mapinduzi, umechochea sana ufisadi, umasikini, kujipendekeza, uzembe, ubabaishaji na kutowajibika kweli kwa Watanzania!!!

Mfumo huu wa sasa umefanya watanzania tudharauliwe na viongozi na kuendeshwa Kama watoto wadogo kuwa tusipowachagua watu wao basi tusahau maendeleo kwa sababu wao ndo wanaamua hela zetu wazigawe vipi!! Hii sio sawa kabisa

Mfumo huu wa sasa umesababisha watu kuwa ombaomba na watumwa kwenye nchi yao kuwa kila wakimuona Raisi basi wamnyenyekee kama Mungu n kumuomba hiki na kile. Kama Raisi tunaomba Maji, barabara, umeme na shule bora

Kwa maendeleo ya kweli ni lazima Watanzania tuamue kwenye uchaguzi huu kumchagua Tundu Antiphas Lissu ili atubadirishie mfumo.

Hamasisha watu wengi zaidi kumchagua Lissu na Chadema kwa maendeleo ya kweli ya Tanzania na Watanzania!

Sambaza kwa watu wengi zaidi waelimike pia!!

Asanteni!
Lord denning.

Mnachosahau ni kwamba maendeleo halisi yanatofautiana kati ya mkoa mmoja na mwingine.

Ukianzisha majimbo umeanzisha aina fulani ya mashindano na dharau miongoni mwa watu wa majimbo hayo.

Leo hii hakuna majimbo unakuta watu wa kaskazini wanawadharau watu wa kanda ya kati, ukianzisha majimbo hizo dharau hazitapungua na zitaivunja nchi.

Sisi tuna utaifa wenye miaka mingi. Maury’s kaoa mnyakyusa, Mhaya kaoa mgogo, mmakonde kaoa mhaya.

Tangu mwanzo kabisa wa ujenzi wa nchi nguvu ilitumika kujenga utaifa, ukija na sera ya majimbo huo utaifa hautabaki salama.
 
Mnachosahau ni kwamba maendeleo halisi yanatofautiana kati ya mkoa mmoja na mwingine.

Ukianzisha majimbo umeanzisha aina fulani ya mashindano na dharau miongoni mwa watu wa majimbo hayo.

Leo hii hakuna majimbo unakuta watu wa kaskazini wanawadharau watu wa kanda ya kati, ukianzisha majimbo hizo dharau hazitapungua na zitaivunja nchi.

Sisi tuna utaifa wenye miaka mingi. Maury’s kaoa mnyakyusa, Mhaya kaoa mgogo, mmakonde kaoa mhaya.

Tangu mwanzo kabisa wa ujenzi wa nchi nguvu ilitumika kujenga utaifa, ukija na sera ya majimbo huo utaifa hautabaki salama.
Kwanza Embu tuambie unaelewaje ukisikia sera ya majimbo?
 
Mnachosahau ni kwamba maendeleo halisi yanatofautiana kati ya mkoa mmoja na mwingine.

Ukianzisha majimbo umeanzisha aina fulani ya mashindano na dharau miongoni mwa watu wa majimbo hayo.

Leo hii hakuna majimbo unakuta watu wa kaskazini wanawadharau watu wa kanda ya kati, ukianzisha majimbo hizo dharau hazitapungua na zitaivunja nchi.

Sisi tuna utaifa wenye miaka mingi. Maury’s kaoa mnyakyusa, Mhaya kaoa mgogo, mmakonde kaoa mhaya.

Tangu mwanzo kabisa wa ujenzi wa nchi nguvu ilitumika kujenga utaifa, ukija na sera ya majimbo huo utaifa hautabaki salama.
Kwani sera ya majimbo inasema hakuna kuoana??? China Mtu wa Shanghai hawezi kuoa Beijing??? Ndo unavyoelewa hivyo Sera za majimbo wewe kilaza wa Lumumba???
 
Back
Top Bottom