Inasikitisha sana, hii tabia ya Waafrika kujiliza ifike mwisho sasa.
Mbaya tunangangania tupendwe na jamii nyingine, wapi umeona raia wa Japan, America, India, Germany, Uruguay n.k wakililia wapendwe iwe katika siasa zao, imani zao za kidini, kibiashara n.k Wao hufanya yao mazuri na kizuri chajiuza wakati kibaya chajitembeza kwa kulialia.
Wamatumbi tuache kulialia fursa zipo kibao na tubadili mifumo yetu ya kimaisha ili tuondokane na minyororo ya umasikini wa kujitakia. Tuache kupoteza muda ktk shughuli za harusi, misiba, kujenga majumba ya mabilioni kwa ajili ya kuishi wakati ndiyo mtaji wenyewe, kuendesha magari kwa ajili ya starehe badala ya kutumika kama nyenzo ya kufuatilia biasha zako, kushinda ktk majumba ya imani za kidini za kuja n.k mambo ambayo yanatugharimu ktk jamii pakubwa kiiuchumi.CHEMA CHAJIUZA KIBAYA CHAJITEMBEZA. kitu kizuri hakihitaji lebo wala nembo
Wenzetu hata baiskeli huwa inatumika ktk shughuli za kiuchumi. Mambo ya kibiashara yakikua hununua pikipiki ya bei nafuu kuzidi kutumika kupanua biashara. Baada ya hapo biashara hiyo ikizidi kukua , hununua gari la bei ndogo na anaendelea kwa mtindo huo hadi kufikia ngazi ya gari la gharama kubwa kufuatana na mabilioni ya faida ktk biashara yake. Sisi wamatumbi tunaruka hatua hizo na kujitumbikiza katika matatizo makubwa ya kifedha na kiuchumi kwa kujiingiza ktk madaraja ambayo bado hatujafikia .
Kwa kifupi ukitaka kujua kama baiskeli au gari inakufaa kwa shughuli zake halali zinazokuingizia kipato basi fanya hesabu je nikipewa mkopo wa baiskeli au pikipiki kwa ajili ya usafiri kwenda kwenye shughuli zako utaweza kulipia mkopo huo kila mwezi, pia kipato chako halali kitaweza kununua chakula, mavazi, karo za shule kama una familia, pango / kodi la/ ya nyumba ? Kama ni hapana achana na hiyo baiskeli au gari tumia usafiri wa umma ndivyo wenzetu wanavyofanya ktk nidhamu ya fedha na kujijengea mtaji / capital.