Serengeti beer, sticker label yenu mpya ni ya hovyo!

Niliwahi pia kulalamika humu. Huyu aliefanya Pack test alikosea sana. Lebel ni mbaya sana. Bora iridu ile black.
Yaani kila nikiiona napata hasira sana.
Kama Balimi kabisa
 
Tembo / Mnazi ambao haujazimuliwa baada ya kulala siku 3/4 ukinywa HUO tunakubeba kwenye Mtaro
Naijua iyo kitu kama sio mkongwe unakata moto kabisa, unakuja kuzinduka siku ya 3 upo mochwari unakuta ndugu ndio wanamalizia taratibu za mazishi yako. Hakafu hangover yake sasa ni wiki mbili
 
Naijua iyo kitu kama sio mkongwe unakata moto kabisa, unakuja kuzinduka siku ya 3 upo mochwari unakuta ndugu ndio wanamalizia taratibu za mazishi yako. Hakafu hangover yake sasa ni wiki mbili
Tembo / Mnazi imekosa vifungashio tu km ilivyo Chibuku Ila ni bonge moja ya koburudisho cha walevi wale wa hali ya Chini litre 1 ni 500 tu zungusha Komichi mwendo wa kupuliza nyuki kwenye Komichi pombe Ina ladha ya asali Dawa ya Figo na kibofu cha mkojo

Tembo / Mnazi ilibidi iwe km ilivyo Juice ya Miwa
 
Marketing manager amefeli. Packaging ni sehemu ya kumvuta mteja.

Inaonekana kama Ile Pilsner za mitambo kileee!
 
Kiukweli ni bia yangu ila mmefeli sana, kwanza label inaonekana ya bei chee, ikiwekwa kwenye friji ikiletwa label inazungukazunguka na gundi, lite imefanana na banana kabisa hadhi yake imepotea, nashauri warudishe label za zamani, yani inafanana na BALAA LIMEINGIA MIJINI (BALIMI) kiufupi nahamia safari lager mpaka warudishe uhalisia wake.
 
Mkuu hapa hujakosea, stika ya ovyo kinyama.... afu sijui wamechakachua kweli.... ladha yake siielewi kabisa
 
Afu kutuwekea rangi za CCM ndio nini sasa? Au kuna mdau wao katia mpunga huko? Ovyo kabisa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…