Pre GE2025 Serikali, Bunge, Ziheshimu Mahakama! Kwanini Serikali na Bunge Hazijatekeleza Hukumu ya Mahakama kuhusu Ubatili wa Katiba na Sheria ya Uchaguzi?

Pre GE2025 Serikali, Bunge, Ziheshimu Mahakama! Kwanini Serikali na Bunge Hazijatekeleza Hukumu ya Mahakama kuhusu Ubatili wa Katiba na Sheria ya Uchaguzi?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Serikali Bunge na Mahakama, zina wajibu wa kuheshimiana, mahakama ikitoa hukumu, bunge na serikali zinapaswa kwanza kutekeleza hukumu husika, ndipo taratibu za kukata rufaa ziendelee, lakini kwa mujibu wa katiba ya JMT ya mwaka 1977, dhima ya mtunga katiba ni sheria yoyote batili, sio sheria, kwa lugha ya kisheria ni "void ab initio", yaani haipo!.
Thanks pascal
 
Vigezo vya Urais ndio vitawaengua,
  • ili kugombea urais, unapaswa kupata wadhamini 1000, katika mikoa 15 ya Tanzania ikiwemo mikoa 2 ya Zanzibar, na mmoja Pemba.
  • Uwe na elimu ya Masters ya Chuo Kikuu
  • Uwe na shughuli ya kueleweka inakuingizia kipato cha zaidi ya TZS. 10,000,000 kwa mwezi
  • Utawasilisha dhamana ya TZS. 100,000,000
  • Utawasilisha list ya wafadhili na gharama za kampeni.
  • Utawasilisha ilani yako ya uchaguzi.
individuals hawawezi.

Vigezo vya Ubunge
  • ili kugombea ubunge, unapaswa kupata wadhamini 100, katika jimbo husika ambao wamejiandikisha kupiga kura.
  • Uwe na elimu ya Chuo Kikuu
  • Uwe na shughuli ya kueleweka inakuingizia kipato cha zaidi ya TZS. 1,000,000 kwa mwezi
  • Utawasilisha dhamana ya TZS. 10,000,000
  • Utawasilisha list ya wafadhili na gharama za kampeni.
  • Utawasilisha ilani yako ya uchaguzi.
Vigezo vya Udiwani
  • ili kugombea udiwani, unapaswa kupata wadhamini 100, katika kata husika ambao wamejiandikisha kupiga kura.
  • Uwe na elimu ya Sekondari
  • Uwe na shughuli ya kueleweka inakuingizia kipato cha zaidi ya TZS. 500,000 kwa mwezi
  • Utawasilisha dhamana ya TZS. 1,000,000
  • Utawasilisha list ya wafadhili na gharama za kampeni.
  • Utawasilisha ilani yako ya uchaguzi.
Serikali ya Mtaa
  • ili kugombea serikali ya mtaa, unapaswa kupata wadhamini 100, katika mtaa husika ambao wamejiandikisha kupiga kura.
  • Uwe na elimu ya kujua kusoma na kuandika
  • Uwe na shughuli ya kueleweka inakuingizia kipato cha zaidi ya TZS. 100,000 kwa mwezi
  • Utawasilisha dhamana ya TZS. 100,000
  • Utawasilisha list ya wafadhili na gharama za kampeni.
  • Utawasilisha ilani yako ya uchaguzi.
P
Vigezo vya u-Rais napinga hiyo milioni 100 pamoja elimu ya masters, degree inatosha na kipato cha milioni 1 kwa mwezi kinatosha na dhamana milioni 10
 
Ni serekali ipi ya kutii hiyo mahakama ambayo hakimu au jaji akipigiwa simu Moja tu anatoa hukumu kuendana na maagizo? Niliidharau sana mahakama wakati wa kesi ya kutungwa ya Mbowe ya ugaidi. Yaani upande wa serekali ulikuwa unatoa ushahidi batili kabisa, na hakimu anaona ni ushahidi wenye mashiko! Mahakama ya kipuuzi hivyo unawezaje kuitii ukiwa na Nia ovu?

Mahakama za Kenya wangalau zinajitambua. Ukitaka kujua mahakama hapa kwetu ni kanyaboya, hata ww mwenye elimu ya Sheria unaishia kuweka mabandiko marefu marefu huku kwenye social media na huendi huko mahakamani, maana unajua ni kupoteza muda.
Hakuna mahakama hapo haya ni matawi ya CCM
 
Back
Top Bottom