Serikali fungeni shule na vyuo kuokoa maisha

Serikali fungeni shule na vyuo kuokoa maisha

Haya yote hayasaidii kwani nchi za wenzetu hawakufanya haya??? Korona imepungua??? Tuache kutishana bure kama ni kufa utakufa tu sio kwa korona hata malaria yatakuua tu! Tuache kujitoa ufahamu
 
Kufunga shule haitasaidia kitu, maana bado mishe mishe za maisha zitabaki vile vile. Napendekeza, barakoa kila mahali, kusiwe na mikusanyiko yoyote, daladala hakuna kusimamisha abiria, watu wapeane distance wanapopata huduma kama za kibenki.
Benki zile alama za viatu si zipo ila watu hawahangaiki nazo sikuhizi
 
Kufunga shule ili iweje. Serikali itoe chanjo bac. Ianze na watoa huduma za afya, iende kwa wazee, then vijana na imalizie na waatoto.
 
Kufikiri kufunga shule na vyuo kwa ugonjwa ambao hujui hatima yake ni ufinyu wa kufikiri. Wewe una kazi nzuri na una uhakika na kesho yako jua kwamba hizo ni ajira za watu! Kuna watu wanalisha familia zao kwa hizo ajira, toka corona ilivyoanza mwaka 2019 decemba duniani kote, mpaka leo nchi zilizofunga shule na vyuo Hawajui nini hatima yake, kwa hiyo wewe endelea kujikinga kivyako sio kuhamasisha wenzako wapoteze ajira.
Comment ya kijinga tokea Tanzania ipate uhuru
 
Tunazidi kupoteza nguvu kazi ya taifa! Hii siyo habari njema hata kidogo! Wizara ya afya, funga shule na vyuo. Watoto na vijana wanapata sana covid lakini, haina madhara makubwa kwao!

Covid haina madhara makubwa kwa vijana na watoto, wanaugua na kupona tena bila dawa za maana. Tatizo ni kuwa, wanaambukizana na kuileta majumbani na kuwaambukiza wazazi na watu wenye umri mkubwa nyumbani.

Hii ndo balaa! Kama tutaweza kudhibi maambukizi kwa watoto na vijana, tutakuwa tumefanikiwa sana kuokoa maisha ya watu wazima wanaojikinga katika familia. Shule na vyuo wafunge mwezi mmoja tu, maambukizi yatapungua.
Hivi umewahi kuwaza sisi wa Manzese, Kwa Mtogole, Mpitimbi, na Nyakanazi watoto wakiwa shule ndiyo wanakuwa salama zaidi kuliko nyumbqni?

Ni watanzania wangapi wanaweza kuwazuia watto wao wasichanganyijane na wengine?
 
1. Waanze kutangaza cases daily na wapi zimepatikana. Wataalamu wa kupambana na magonjwa ya milipuko wapewe confidence na uhuru wa kufanya kazi zao bila kusubiri ruhusa kutoka kwa wanasiasa
2. Weka bylaws kila mtu avae barakoa kwenye public. Mkaidi akamatwe na kulipa faini
3. Wageni kutoka nje wote waje na negative certificate za COVID with immediate effect. Ambae hana arudishwe na ngege aliyokuja nayo
4. Wafanyakazi waanze kuingia ofisini kwa shift na wengine wafanyie home ili kupunguza mikusanyiko. Hakuna haja ya kujazana ofisini
5. Public transport zianze kubeba watu nusu ya uwezo wake
6. Funga clubs kwa mwezi mmoja

Kuna mengi ya kufanya ila kiburi cha Magufuli ni tatizo. Sasa katwaliwa Eng. Kijazi. Who next?
Namba 2 TRA hawajaiona? Chanzo cha mapato hicho
 
Kufikiri kufunga shule na vyuo kwa ugonjwa ambao hujui hatima yake ni ufinyu wa kufikiri. Wewe una kazi nzuri na una uhakika na kesho yako jua kwamba hizo ni ajira za watu! Kuna watu wanalisha familia zao kwa hizo ajira, toka corona ilivyoanza mwaka 2019 decemba duniani kote, mpaka leo nchi zilizofunga shule na vyuo Hawajui nini hatima yake, kwa hiyo wewe endelea kujikinga kivyako sio kuhamasisha wenzako wapoteze ajira.
... watabaki mayatima wengi sana! Serikali itawahudumia? Shule zifungwe kwa muda sote (wazazi na watoto) tuwe salama au nchi ibaki na maelfu ya mayatima? Au unawaza usawa wa pua?
 
Unawezafikiri unawaza jema kuhusu kufunga shule, Kenya walifunga shule toka mwaka Jana kaulize madhara yake kwa taifa. Inawezekana wewe ni mfanyakazi wa serikali unayekula pesa yetu, hebu jaribu kuwafikiria na ndugu zako wanaoishi kupitia hizi shule mwisho wao utakuwa nini.

Kungekuwa na uwezekano raisi afunge shule lakini pia asimamishe mishahara yenu mpaka shule zitakapofunguliwa ili tuzungumze lugha moja huku mtaani. We are too selfish. Mwacheni raisi wetu ana mengi ya kufikiri juu ya taifa hili.

Na nyinyi walinzi tunaomba mumlinda sana raisi wetu maana kuna watu wakisikia anaumwa hata Mafua watashangilia sana.
 
Huu ugonjwa itabidi watu wawe tayari kufa, kufa na kufa tena maana tunaona wateule wa Jiwe wanaona aibu kuvaa barakoa huku wakiwa wengi ni wazee wenye kisukari,pressure & ukimwi
 
Kufikiri kufunga shule na vyuo kwa ugonjwa ambao hujui hatima yake ni ufinyu wa kufikiri. Wewe una kazi nzuri na una uhakika na kesho yako jua kwamba hizo ni ajira za watu! Kuna watu wanalisha familia zao kwa hizo ajira, toka corona ilivyoanza mwaka 2019 decemba duniani kote, mpaka leo nchi zilizofunga shule na vyuo Hawajui nini hatima yake, kwa hiyo wewe endelea kujikinga kivyako sio kuhamasisha wenzako wapoteze ajira.
Ila jamaa kasema kwa mwezi mmoja kama umemsoma vema, nafikiri ili kujipanga.
 
Kwa nini wote mna ushauri wa kukurupuka.
Kufunga shule wengi wataumia.

Hapa walete chanjo. Wazee na watu wa afya wapigwe chanjo
Chanjo ipo na ishaanza kutumika.

Upumbavu wa meko ni mzigo.
Mutant ya sA inatakiwa impige maana kawa kama farao
 
Kufikiri kufunga shule na vyuo kwa ugonjwa ambao hujui hatima yake ni ufinyu wa kufikiri. Wewe una kazi nzuri na una uhakika na kesho yako jua kwamba hizo ni ajira za watu! Kuna watu wanalisha familia zao kwa hizo ajira, toka corona ilivyoanza mwaka 2019 decemba duniani kote, mpaka leo nchi zilizofunga shule na vyuo Hawajui nini hatima yake, kwa hiyo wewe endelea kujikinga kivyako sio kuhamasisha wenzako wapoteze ajira.
Hao wachache wakiwa sucriface kwa ajili ya kuokoa Taifa au wengi sio tatizo,acha ubinafsi wa kijinga.

By the way ni wajibu wa serikali kuangalia Hali zao na kusaidia
 
Tunazidi kupoteza nguvu kazi ya taifa! Hii siyo habari njema hata kidogo! Wizara ya afya, funga shule na vyuo. Watoto na vijana wanapata sana covid lakini, haina madhara makubwa kwao!

Covid haina madhara makubwa kwa vijana na watoto, wanaugua na kupona tena bila dawa za maana. Tatizo ni kuwa, wanaambukizana na kuileta majumbani na kuwaambukiza wazazi na watu wenye umri mkubwa nyumbani.

Hii ndo balaa! Kama tutaweza kudhibi maambukizi kwa watoto na vijana, tutakuwa tumefanikiwa sana kuokoa maisha ya watu wazima wanaojikinga katika familia. Shule na vyuo wafunge mwezi mmoja tu, maambukizi yatapungua.
Mkuu kwa upanda wangu shuluisho hapa siyo kufunga shule na vyuo,
Sema serikali iweke mikakati dhabiti ya kuandaa mazgr. kwa kila taasisi kuwa na tahadhiri effectively
Kwa maana wizara ya Afya watoe semina na mafunzo namna gani wanavyo weza kupamvana na viral disease
 
Back
Top Bottom