Serikali: Hatujasaini EPA, Msimamo wetu uko palepale

Serikali: Hatujasaini EPA, Msimamo wetu uko palepale

OLS

JF-Expert Member
Joined
Oct 12, 2019
Posts
426
Reaction score
685
Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara imekanusha suala linaloendelea mtandaoni kuwa serikali imepitisha Economic Partnership Agreement(EPA) ambayo imetajwa na wasomi wengi kuwa itasababisha Tanzania kupoteza mapato yanayotokana na Importations kwa takribani 71% in the long run

Wizara imesema mijadala inayoendelea mitandaoni kuhusu suala hilo halina ukweli bali bado Tanzania inaendelea kuwa na msimamo wa kukataa makubaliano hayo ambayo yalipingwa vikali na Rais Mkapa mwaka 2015 katika moja ya andiko lake, ambapo pia rais Magufuli aliyakataa suala hilo.

Serikali imesema inaendelea kufanya mambo yenye manufaa kwa nchi na Jumuiya ya Afrika mashariki na kuwataka wananchi kupuuza taarifa zinazoenea mtandaoni.

MIJADALA KUHUSU EPA
EPA ni makubaliano yanayotaka kuweka biashara huria kati ya nchi za Afrika na Ulaya, kwa kuondoa vikwazo vya kuingiza na kutoa bidhaa. Yaani Ulaya watakakuwa wanaingiza bidhaa zao nchini bila kodi na tozo, hali ambayo imeonekana itashusha mapato ya nchi yanayotokana na importations. Aidha kutokana na uchanga wa viwanda vilivyopo, makubaliano haya yametajwa kuua viwanda vya ndani. Ambapo rais Mkapa alisema kuwa yataifanya makubaliano yataifanya Afrika kuwa Dampo.

Katika nchi za Afrika mashariki, Kenya wameshakubaliana na EPA na wameanza kutekeleza huku Tanzania, Uganda na Burundi zikiwa bado hazijakubaliana na habari hiyo.

Tanzania kama nchi inayoendelea inafaidi kupeleka bidhaa katika nchi za Jumuiya ya Ulaya bila kutozwa kodi kutokana na makubaliano ya Everything But Arms(EBA) ambao uliingiwa mwaka 2001 ikiwa na nia ya kukuza viwanda vya nchi zinazoendelea.

Kuingia katika makubaliano ya EPA kutaifanya Tanzania isiweze kufanya protectionism. Na makubaliano haya yanakuwa kama EU nao wanataka kufaidi kile ambacho nchi zinazoendelea zinafaidi kupitia EBA.

HALI ILIVYOKUWA
Hivi karibuni kumekuwa na tetesi kuwa serikali ilikuwabaliana na suala hilo na kukawa na mijadala mtandaoni ikiwa nchi imefanya study ya kujua madhara ya suala hilo. Swali kubwa lilikuwa, kama nchi inafaidika kwa EBA kuna haja gani ya kujiunga na EPA?

Lakini kwa kanusho hili la Serikali limeleta unafuu na ahueni kwa kuona kumbe tuko makini


Signed
OEDIPUS

Pia, soma;

Thread 'Rais Samia kusaini EPA huko Brussels?' Rais Samia kusaini EPA huko Brussels?

1.jpg
 
Tanzania position on ratification of the East African Community (EAC) and European
Union (EU) Economic Partnership Agreement (EPA) has not changed!

8EF37ED2-05C0-4A44-B076-8FEECF12E488.jpeg
 
Afadhali angeandika kiswahili tu. Kwa vile Zuhura aliandika "Press Release" kwa kiingereza, na Suzan naye anajikwamua na kuandika ya kwake kwa "kiingereza cha mtaani". Yaani alipanga mawazo katika kiswahili, halafu akayatafsiri kutoka kiswahili kuwa kiingereza.
 
Haya ni maamuzi ya hovyo kabisa. Sasa sisi Tanzania tuna nini cha kusema tunalinda cha ndani? Tulichonacho hakina hadhi ya kulindwa.

Economic advantage yetu ni vitu raw, i.e unprocessed, mfano mbao, maparachichi, maua, nk.

kwa upande mmoja sisi tuna ardhi ya kutosha inayoweza kutumiwa na wajasiriamali kuzalisha raw products. Kwa upande wa pili, wazungu wao wana teknolojia muhimu tunazozihitaji.

Hapa unapata win-win situation.
 
Haya ni maamuzi ya hovyo kabisa. Sasa sisi Tanzania tuna nini cha kusema tunalinda cha ndani? Tulichonacho hakina hadhi ya kulindwa...
Hiyo advantage unayoitaja unaipata kwenye EBA ambapo vitu vyote hivyo huingia EU bila kodi mkataba ulisainiwa 2001, nia ikiwa ni kukuza uchumi wetu. Hili suala la EPA ni suala la EU kuingiza bidhaa nchini bila kodi. Elewa kipengele hicho kwanza
 
Yaani mnalinda bidhaa zenu za ndani mfano, sukari yenu kutoka moshi inauzwa arusha shs 2900/= na sukari iliyopamda meli kutoka Brazil inauzwa arusha shs 2050/=

Nchi jirani ya Zanzibar wanaruhusu biashara huria wananchi wanafaidika na bidhaa za nje kwa bei ya chee nyie mnalinda vya ndani huku wananchi wanaumia kwa bei za juu.

Bora msaini tu viwanda vyetu vipumue, kuliko kutosaini alafu bado bei kwa inside product inazidi ya nje kwa 50%
 
Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara imekanusha suala linaloendelea mtandaoni kuwa serikali imepitisha Economic Partnership Agreement(EPA) ambayo imetajwa na wasomi wengi kuwa itasababisha Tanzania kupoteza mapato yanayotokana na Importations kwa takribani 71% in the long run

Wizara imesema mijadala inayoendelea mitandaoni kuhusu suala hilo halina ukweli bali bado Tanzania inaendelea kuwa na msimamo wa kukataa
Tuwe makini, hawa watu watakuja ku import vitu vya ajabu hata vya kudhuru raia. The economic war is real. Kueni makini
 
Rais samia anaelekea kukubali kutia sahihi mkataba wa nchi za ulaya na nchi za kiafrika EPA. Mkataba huo umekataliwa na watangulizi wake kwani unaziweka nchi za kiafrika kubakia soko tu na kuzuia jitihada za kujitegemea kwa kuendeleza viwanda.

Nchi ya tanzania ina fulsa kuendelea kiviwanda kutokana na ukubwa wake idadi ya wananchi na mali asili yake kama madini na ardhi kubwa. Mkataba wenye masharti kama yale ya epa itaibana nchi yetu kujenga viwanda ambavyo vitatoa ajira kwa wananchi na wasomi badala yake wasomi kubakia na umachinga wa bidhaa za ulaya.

Watanzania tukae chonjo na rais wa kupapatikia chochote anachoshauriwa na wazungu kama kina tony blair. Tusiache spirit ya kujenga kujitegemea na kupinga unyonyaji iwe kwa mtu na mtu au kunyonywa kama nchi na mabebetu.
 
Back
Top Bottom