Serikali hii ya Magufuli itakuwa na ubavu wa kugomea masharti magumu ya Wachina ilhali wanataka kukamilisha miradi hii ndani ya miaka mitano?

Nimeipenda hii sana mkuu, tatizo nchi kwa sasa hakuna usikivu, ni maamuzi kutoka juu tu.
 
Akili kusoda, like father like son
 
Naona ni uzi wa kupiga ramli huu.
 
Hukunielewa nasema ukileta ufisadi kwa mchina yeye hajali masuala ya haki za binadamu. Kama kusingalikuwa na uhitaji wa maini wafungwa wasingetolewa hayo maini.

SGR ya kenya ni akina Kenyatta kulangua ardhi kwao, je utalaumu Wachina au Viongozi wa Kenya kwa ufisadi? Always demand ndiyo inasababisha supply
 
Magufuli hana rafiki; kwa hiyo hashindwi kabisa kuwakatalia Wachina papo kwa papo wakileta masharti asiyokubaliana nayo.
Hapo hapahitaji "urafiki"

Sio kweli "hashindwi kabisa kuwakatalia...". Mbona historia ya utumishi wake inaonyesha ku'capitulate' akikataliwa na wakubwa. Ghorofa la Tanesco halikuvunjwa.

Usidhani mfano huo hauendani na hali anayoikabili sasa hivi kuhusu miradi hiyo.
 
Ccm na wachina ni damu damu mwenyekiti alidhani angeweza watenga amerealize mwenyewe.akaja tofauti SGR mturuki stiglers Egypt soon mradi wa Bandari bagamoyo tutaambiwa una tija.
 
Laiti Kama KILA mlipa Kodi angeshirikishwa juu ya vipaumbele vya matumizi ya Kodi yake tungekuwa mbali Sana.
 
Mkuu kwanza hakuna makubaliano au mkataba hadi sasa.
Pili Magufuli huyu huyu ndie alikataa ujenzi wa bandari ya Bagamoyo baada ya kugundua mapungufu wa mradi.Kwa mantiki hiyo hataingia kijinga kama watangulizi wake.
Tatu China analipa fadhila za Tanzania kumuweza kurudishwa Umoja wa Mataifa, labda ndio tofauti China anavyozichukulia nchi nyingine.
Nne China ameichukulia Tanzania kuwa taifa linalozungukwa na mataifa mengi sana kama mlango wa biashara na usalama wa mataifa hayo.
Lakini pammoja na hayo China ndie nchi yenye miradi yenye wakandarasi wengi sana kwa miradi mikubwa hadi midogo kuliko taifa lolote hapa Bongo.Hivyo kumpa msaada Tanzania ni jambo lilio wazi.
Hata hivyo maliasili, madini yanayopatikana Tanzania yanahitajika China kwa wingi.
Pamoja na hayo Tanzania isibweteke na maneno mazuri ya China.Yawezekana ni mbinu za ukoloni mamboleo.
 
we kibaraka wa wachina zama za kuwategemea wafadhili wa kichina zimepitwa na wakati sasa mfadhili mkuu ni kodi zetu only
 
Manyumbu bana...mnajiuliza na kujijibu wenyewr...tulieni dawa iwaingie...acheni maneno ya kijiweni
 
Mzee wala usitumie nguvu nyingi kujibishana na hawa nyumbu wako hapa kama fisi wanasubiri mkono udondoke...wanavyoongelea utadhani hii miradi haiwahusu wao..all in all sema vyote kuhusu China Ila ndo nchi pekee iliyosaidia kufanya uwekezaji mkubwa kwenye nchi maskini..hayo mengine kunyonywa ni maamuzi binafsi kwani mikataba inasainiwa na watu wanaojielewa...wanamsema mchina wakati mzungu yeye anawekeza kwenye condom na vita tu...miundombinu kakaa pembeni..tufanye kazi aisee
 
kurahisisha usafiri wa kwenda burigi- chato
 
Naona point kwenye uzii huu, ngoja nifikiri kidogo nitarejea baadae. Linanikumbusha tricks za negotiations if you are compromised you stand a good chance of losing ground.
 
Japo sijaona polisi wa kihindi au kiarabu Tanzania lakini nauliza je mchina hawezi kuwa raia wa Zambia na akapatiwa fursa yoyote ile?

Kuna kazi nyeti hawapewi raia wa “kusajiliwa”.

Kuna Watanzania wenye asili ya kihindi na kiarabu wengi ambao ni uzao wa 3 na zaidi wa wahamiaji. Zamani walikuwemo kwenye majeshi yetu kabla “siasa za uswahili” hazijakolea majeshini na viwango kuathiriwa.
 
kama tuliwagomea mabeberu,mchina hawezi kutuyumbisha,ni sisi ndio tunapanga masharti ya kukopa
unafahamu kwamba SGR ilikua apewe mchina?pesa ilikua tayari ya kumaliza mradi wote kwa 100%,lakin kwa uzalendo wetu tukakataa gharama zilikua kubwa mno
 
kama tuliwagomea mabeberu,mchina hawezi kutuyumbisha,ni sisi ndio tunapanga masharti ya kukopa
unafahamu kwamba SGR ilikua apewe mchina?pesa ilikua tayari ya kumaliza mradi wote kwa 100%,lakin kwa uzalendo wetu tukakataa gharama zilikua kubwa mno
Kabombe: unazungumza ukweli? au utani?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…