Mtutuwandei
JF-Expert Member
- Jun 28, 2022
- 1,317
- 1,817
Joined Feb 3 2008. Bado ananufaika na bima ya wazazi.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Gharama zao ni sawa na za NHIF na baadhi yao gharama zipo chini ukilingansha na NHIF. Kwa bima nyingine, mwanachama ana haki ya kumuandikisha yeyote yule bila kupangiwa.Hivi swali la gharama za bima nyengine limejibiwa? Na kuhusu ukomo wa umri kumekaaje huko. Na uwezo wa kuwabeba wazazi na wakwe?
Je wajua hyo mifuko mingine ulioitaji hata kufikika ni kazi na ofs zao hazijulikani na ada zao huenda zikawa ghali sana hata kufikikaKatika siku za karibuni Bima ya Afya ya Taifa imekuwa gumzo kila kona, hasa inapodaiwa kwamba mfuko huu wa bima unaotoa matibabu kwa watumishi wa umma na familia zao, unakaribia kukata roho. Naomba kutangaza masilahi (declare interest) kwamba mimi ni mnufaika wa mfuko huu kupitia wazazi wangu ambao ni watumishi wa umma.
Mbali na NHIF kuna mifuko mingine mingi inayotoa huduma nzuri zaidi hapa nchini ukilinganisha na mfuko huu ambao kila kukicha umekuwa ukiwafanyia vitimbi wananchama wake na kuwakosesha huduma za matibabu kwa sababu ambazo hazina kichwa wala miguu. Nasema haya kwa ushahidi mubashara. Uongozi wa NHIF umekuwa ukiwabania wanachama wake dawa nzuri na zinazotibu barabara kwa kuhofia wananchama wao kuwa na afya mujarabu. Lengo la kufanya hila zote hizi wanazijua viongozi waliopewa dhamana ya kusimamia mfuko. Vitimbi vya karibuni kabisa kufanywa na NHIF ni kufuta fao la Toto Afya Card na kuwapangia wanachama kiasi cha kuumwa – kwamba kila mwanachama aumwe mara 4 tu kwa mwezi!
Kuna bima lukuki hapa nchini zinazotoa huduma nzuri bila unyanyapaa wala vitimbi kwa wananchama. Nimewahi kuwa mwanachama wa bima za afya Medex na AAR. Mifuko hii haina ujinga kama huu tunaoshuhudia NHIF. Wanajali zaidi uhai wa mwanachama tofauti na NHIF wanaojali matumbo yao na kuwaacha wanachama wajifie kifo cha mende. Ukiwa ndani ya AAR au Medex ni raha tupu. Hata ukiumwa ugonjwa mkubwa ulioshindikana kutibika hapa nchini, unasafirishwa nje ya nchi kwenda kutibiwa. Kupitia mifuko hii, wagonjwa wengi tu wametibiwa Uingereza, Ujerumani, Ufaransa, Afrika Kusini India na mataifa mengine ya nje yenye huduma nzuri za afya. Lakini kwa NHIF, ugonjwa wako ukishindikana kutibiwa hapa nchini, unaachwa ujifie kama mbwa. Inauma sana.
Baada ya kutoa dokezo hiili, naomba sasa nitoe ushauri wangu wa mwisho jinsi ya kuboresha huduma za NHIF. Kwanza ni kuondoa ukiritimba na figisu kwa wanachama. Nashauri wanachama wapewe uhuru wa kuchagua mfuko wa matibabu tofauti na sasa ambapo watumishi wote wa umma hulazimishwa kukatwa pesa na kutibiwa na NHIF watake wasitake. Wanachama wengi, ambao ni watumishi wa umma, wamechoshwa na vituko vya NHIF. Wanatamani wafunguliwe minyonyororo ya utumwa waliyofungwa kwa muda mrefu ndani ya NHIF wakatafute huduma nzuri kwenye mifuko mingine inayotoa bima za matibabu kama vile AAR, Momentum, Strategies, NMB, NSSF na mingine mingi tu iliyotapakaa hapa nchini.
Kwanini watu wanyimwe uhuru wa kujiunga na mifuko mingine ilhai kila siku NHIF inalalamika kuwa na hali mbaya ya kiuchumi? Ukiona hivyo ujue kuna manufaa ambayo serikali na watumishi wa NHIF wanayapata ambayo wakiruhusu watu waondoke, wanaweza kuyakosa. Kwa maana hiyo kumbe NHIF haipo kwa ajili ya maslahi ya wanachama bali ni kwa ajili ya maslahi ya serikali na wachumiatumbo wachache wasiopenda kuona watanzania wanakuwa na siha njema. Huu ni zaidi ya uhaini na uhujumu uchumi. Naomba TAKUKURU wafanye uchunguzi wa kina.
Ili NHIF iondokane na malalamiko ya gharama kubwa za matibabu kwa wanacham wake na kuhofia kufilisika, basi iwaachie wanachama waondoke mmoja mmoja waende wakatafute matibabu kupitia bima nyingine za afya. Wakibaki wanachama wachache inaweza kuwahudumia vizuri zaidi. Na hata hao wachache wakiamua kuhama, waachiwe waondoke. Wanachama wote wakishaondoka NHIF ifunge ofisi zake zote nchini na serikali iwapangie kazi nyingine waliokuwa waajiriwa wa NHIF. Kufikia hapo tatizo litakuwa limepata ufumbuzi wa kudumu. Huwezi kung’ang’ania jambo linakuuumiza kichwa wakati kuna ufumbuzi wa kudumu usiohitaji gharama yoyote.
Ikiwa serikali itafuata ushauri huu, itajiondoa jumla kwenye lawama za watanzania wanaokufa kila siku kwa sababu ya ubovu wa huduama za NHIF inayolalamika kutokuwa na fedha za kutosha kugharamia matibabu ya wanachama wake hadi kufikia hatua ya kufuta fao la Toto Afya Card na kuanzisha masharti ya kipuuzi kwa wananchma ambayo hayatekelezeki.
Nawasilisha.
Gharama zao ni sawa na za NHIF na baadhi yao gharama zipo chini ukilingansha na NHIF. Kwa bima nyingine, mwanachama ana haki ya kumuandikisha yeyote yule bila kupangiwa.
NHIF wanawapangia wanachama aina ya wanufaika.....wanataka mke/mume na watoto tu. Bima nyingine unamuingiza shangazi, mjomba, housegirl, jirani au mtu yeyote bila kubaguliwa ilmradi idadi ya wanachama izingatiwe.
Mkuu, vitabu vyote navifahamu vizur sana, kuna NHIF pricing, na NHIF ICD codes, nachokwambia sibahatishi, NHIF wanataka mtoa huduma afuate taratibu matibabu kwa mujibu wa standard treatment guidelines ( STG) wakati wateja wao wanataka wanabagua dawa, mfano mzuri ni kwenye UTI , unakuta mteja anataka azithromycin ( Azuma) lakini STG imeelekeza toa amoxycillin au nitrofurantoin au ciprofloxacin katika level ya zahanat, lakini health centre na hospital imeelekeza toa Amoxy clav, AMA kwa msaada wa culture and sensitivity toa powercef.Watoa huduma wanakuwa na kitabu cha amaelekezo kutoka NHIF kinachoelekeza aina ya dawa za kuwapa wanachama na nyingi ya hizi dawa hazina ubora. Kama hujawahi kukiona kitabu hicho nenda hospitali yoyote inayotoa huduma za NHIF ukiombe utapewa. Kina orodha ya dawa za NHIF. Wale wanaolipia cash wanapata aina yoyote ya dawa nzuri lakini wa NHIF wanabaguliwa.
Wanaabdikisha watoto kupitia shule, so kama una mtoto yuko shule , gharama ni ndogo sana tsh. 50400/=per yearMkuu kwa ambao tunataka kuandikisha watoto tu, inawezekana?
Strategies wako mikoa mingi sana, ila ada ya kuchangia malipo ya uanachama yako juu sana kuliko watu wanavyofikiria, NHIF wana gharama ndogo sana kulinganisha na hao wengineJe wajua hyo mifuko mingine ulioitaji hata kufikika ni kazi na ofs zao hazijulikani na ada zao huenda zikawa ghali sana hata kufikika
Mfano ofs za STRATEGIES OR MOMENTUM MIE SIJAWAHI KUZIONA NA SIJUI WAKO WAPO HUENDA WAPO DAR TU HATA SIMU ZAO NAMBA ZAO HAZIJULIKANI naaomba kujua wako wap msaaada
Mkuu, vitabu vyote navifahamu vizur sana, kuna NHIF pricing, na NHIF ICD codes, nachokwambia sibahatishi, NHIF wanataka mtoa huduma afuate taratibu matibabu kwa mujibu wa standard treatment guidelines ( STG) wakati wateja wao wanataka wanabagua dawa, mfano mzuri ni kwenye UTI , unakuta mteja anataka azithromycin ( Azuma) lakini STG imeelekeza toa amoxycillin au nitrofurantoin au ciprofloxacin katika level ya zahanat, lakini health centre na hospital imeelekeza toa Amoxy clav, AMA kwa msaada wa culture and sensitivity toa powercef.
Kifupi huoni mahala pameandikwa toa azuma, hapa ndipo ulipo mkanganyiko kati ya wanachama na NHIF kuona wanaonewa sana, ila taratibu za matibabu zinatakaje?
Hili linafanyika kuondoa risk ya usugu wa dawa
ingekuwa poa sana ningekuwa nafanya kazi NHIF, ila hata fikra hizo hazipo, nimegombana nao sana kwa nyakati tofauti tofauti, nawafahamu sana, changamoto zao ni financial management kama Dulu zisemavyo wanajipigia hela za wanachama, ila upande wa huduma tusiwaonee hivyo, watu wanafanyiwa dialysis, operative procedures na major surgeries mbalimbali, Jamani Mnyonge Mnyongeni haki yake mpeniMkuu utakuwa wewe ni Mfanyakazi wa NHIF nina mtu anafanyia kazi NHIF tena anacheo aliyosema jamaa ni kweli kabisa labda wewe unatetea ugali wako.
Huyo atakua mnufaika,maana ata utetezi wake ni hovyo hovyo tu.Mkuu mbona wewe unawatetea sana hawa wezi? Kwanini lakini?
Serikali ndiyo iliyoshindwa.kwasababu serikali ndiyo iliyoshindwa kuwasimamia hao waliowapa hiyo dhamana yajufanya hiyo kazi.Wananchi tumeiajiri serikali kwahiyo lawama lazima ziende kwa tuliyemuajiri.Serikali ingekua inachujua hatua hayo maujinga yasingekuwepo.Ila haiwezi kwasababu yenyewe ni sehemu ya tatizo.Hapana mkuu, kuilaumu serikali moja kwa moja is unfair, Serikali inapowapa taasisi watu waisimamie maanake imewapa dhamana kubwa, wakifail haimaanishi serikali imefail ila watu hao, cha msingi ni reformation tu
Ushauri wangu.Katika siku za karibuni Bima ya Afya ya Taifa imekuwa gumzo kila kona, hasa inapodaiwa kwamba mfuko huu wa bima unaotoa matibabu kwa watumishi wa umma na familia zao, unakaribia kukata roho. Naomba kutangaza masilahi (declare interest) kwamba mimi ni mnufaika wa mfuko huu kupitia wazazi wangu ambao ni watumishi wa umma.
Mbali na NHIF kuna mifuko mingine mingi inayotoa huduma nzuri zaidi hapa nchini ukilinganisha na mfuko huu ambao kila kukicha umekuwa ukiwafanyia vitimbi wananchama wake na kuwakosesha huduma za matibabu kwa sababu ambazo hazina kichwa wala miguu. Nasema haya kwa ushahidi mubashara. Uongozi wa NHIF umekuwa ukiwabania wanachama wake dawa nzuri na zinazotibu barabara kwa kuhofia wananchama wao kuwa na afya mujarabu. Lengo la kufanya hila zote hizi wanazijua viongozi waliopewa dhamana ya kusimamia mfuko. Vitimbi vya karibuni kabisa kufanywa na NHIF ni kufuta fao la Toto Afya Card na kuwapangia wanachama kiasi cha kuumwa – kwamba kila mwanachama aumwe mara 4 tu kwa mwezi!
Kuna bima lukuki hapa nchini zinazotoa huduma nzuri bila unyanyapaa wala vitimbi kwa wananchama. Nimewahi kuwa mwanachama wa bima za afya Medex na AAR. Mifuko hii haina ujinga kama huu tunaoshuhudia NHIF. Wanajali zaidi uhai wa mwanachama tofauti na NHIF wanaojali matumbo yao na kuwaacha wanachama wajifie kifo cha mende. Ukiwa ndani ya AAR au Medex ni raha tupu. Hata ukiumwa ugonjwa mkubwa ulioshindikana kutibika hapa nchini, unasafirishwa nje ya nchi kwenda kutibiwa. Kupitia mifuko hii, wagonjwa wengi tu wametibiwa Uingereza, Ujerumani, Ufaransa, Afrika Kusini India na mataifa mengine ya nje yenye huduma nzuri za afya. Lakini kwa NHIF, ugonjwa wako ukishindikana kutibiwa hapa nchini, unaachwa ujifie kama mbwa. Inauma sana.
Baada ya kutoa dokezo hiili, naomba sasa nitoe ushauri wangu wa mwisho jinsi ya kuboresha huduma za NHIF. Kwanza ni kuondoa ukiritimba na figisu kwa wanachama. Nashauri wanachama wapewe uhuru wa kuchagua mfuko wa matibabu tofauti na sasa ambapo watumishi wote wa umma hulazimishwa kukatwa pesa na kutibiwa na NHIF watake wasitake. Wanachama wengi, ambao ni watumishi wa umma, wamechoshwa na vituko vya NHIF. Wanatamani wafunguliwe minyonyororo ya utumwa waliyofungwa kwa muda mrefu ndani ya NHIF wakatafute huduma nzuri kwenye mifuko mingine inayotoa bima za matibabu kama vile AAR, Momentum, Strategies, NMB, NSSF na mingine mingi tu iliyotapakaa hapa nchini.
Kwanini watu wanyimwe uhuru wa kujiunga na mifuko mingine ilhai kila siku NHIF inalalamika kuwa na hali mbaya ya kiuchumi? Ukiona hivyo ujue kuna manufaa ambayo serikali na watumishi wa NHIF wanayapata ambayo wakiruhusu watu waondoke, wanaweza kuyakosa. Kwa maana hiyo kumbe NHIF haipo kwa ajili ya maslahi ya wanachama bali ni kwa ajili ya maslahi ya serikali na wachumiatumbo wachache wasiopenda kuona watanzania wanakuwa na siha njema. Huu ni zaidi ya uhaini na uhujumu uchumi. Naomba TAKUKURU wafanye uchunguzi wa kina.
Ili NHIF iondokane na malalamiko ya gharama kubwa za matibabu kwa wanacham wake na kuhofia kufilisika, basi iwaachie wanachama waondoke mmoja mmoja waende wakatafute matibabu kupitia bima nyingine za afya. Wakibaki wanachama wachache inaweza kuwahudumia vizuri zaidi. Na hata hao wachache wakiamua kuhama, waachiwe waondoke. Wanachama wote wakishaondoka NHIF ifunge ofisi zake zote nchini na serikali iwapangie kazi nyingine waliokuwa waajiriwa wa NHIF. Kufikia hapo tatizo litakuwa limepata ufumbuzi wa kudumu. Huwezi kung’ang’ania jambo linakuuumiza kichwa wakati kuna ufumbuzi wa kudumu usiohitaji gharama yoyote.
Ikiwa serikali itafuata ushauri huu, itajiondoa jumla kwenye lawama za watanzania wanaokufa kila siku kwa sababu ya ubovu wa huduama za NHIF inayolalamika kutokuwa na fedha za kutosha kugharamia matibabu ya wanachama wake hadi kufikia hatua ya kufuta fao la Toto Afya Card na kuanzisha masharti ya kipuuzi kwa wananchma ambayo hayatekelezeki.
Nawasilisha.
Mkuu kwani ugonjwa unapokuja unaagalia kama mgonjwa hana access ya kituo cha kutolea huduma chenye level ya kutoa dawa nzuri. Mimi nakuambia dawa fulani hainitibu afu wewe unanilazimisha uniandikie dawa hiyo nikafanyie nini? Huoni kwamba huo ni ukiritimba usioikuwa na sababu zozote za msingi?mfano mzuri ni kwenye UTI , unakuta mteja anataka azithromycin ( Azuma) lakini STG imeelekeza toa amoxycillin au nitrofurantoin au ciprofloxacin katika level ya zahanat, lakini health centre na hospital imeelekeza toa Amoxy clav, AMA kwa msaada wa culture and sensitivity toa powercef.
Huyo atakuwa anatetea mpunga bila kujali kwamba hata ndugu zake nao wanahitaji matibabu. Jamaa mbinafsi sana aisee!Mkuu utakuwa wewe ni Mfanyakazi wa NHIF nina mtu anafanyia kazi NHIF tena anacheo aliyosema jamaa ni kweli kabisa labda wewe unatetea ugali wako.
Wakuu kama taifa kila mmoja anaweza kuona makosa,Katika siku za karibuni Bima ya Afya ya Taifa imekuwa gumzo kila kona, hasa inapodaiwa kwamba mfuko huu wa bima unaotoa matibabu kwa watumishi wa umma na familia zao, unakaribia kukata roho. Naomba kutangaza masilahi (declare interest) kwamba mimi ni mnufaika wa mfuko huu kupitia wazazi wangu ambao ni watumishi wa umma.
Mbali na NHIF kuna mifuko mingine mingi inayotoa huduma nzuri zaidi hapa nchini ukilinganisha na mfuko huu ambao kila kukicha umekuwa ukiwafanyia vitimbi wananchama wake na kuwakosesha huduma za matibabu kwa sababu ambazo hazina kichwa wala miguu. Nasema haya kwa ushahidi mubashara. Uongozi wa NHIF umekuwa ukiwabania wanachama wake dawa nzuri na zinazotibu barabara kwa kuhofia wananchama wao kuwa na afya mujarabu. Lengo la kufanya hila zote hizi wanazijua viongozi waliopewa dhamana ya kusimamia mfuko. Vitimbi vya karibuni kabisa kufanywa na NHIF ni kufuta fao la Toto Afya Card na kuwapangia wanachama kiasi cha kuumwa – kwamba kila mwanachama aumwe mara 4 tu kwa mwezi!
Kuna bima lukuki hapa nchini zinazotoa huduma nzuri bila unyanyapaa wala vitimbi kwa wananchama. Nimewahi kuwa mwanachama wa bima za afya Medex na AAR. Mifuko hii haina ujinga kama huu tunaoshuhudia NHIF. Wanajali zaidi uhai wa mwanachama tofauti na NHIF wanaojali matumbo yao na kuwaacha wanachama wajifie kifo cha mende. Ukiwa ndani ya AAR au Medex ni raha tupu. Hata ukiumwa ugonjwa mkubwa ulioshindikana kutibika hapa nchini, unasafirishwa nje ya nchi kwenda kutibiwa. Kupitia mifuko hii, wagonjwa wengi tu wametibiwa Uingereza, Ujerumani, Ufaransa, Afrika Kusini India na mataifa mengine ya nje yenye huduma nzuri za afya. Lakini kwa NHIF, ugonjwa wako ukishindikana kutibiwa hapa nchini, unaachwa ujifie kama mbwa. Inauma sana.
Baada ya kutoa dokezo hiili, naomba sasa nitoe ushauri wangu wa mwisho jinsi ya kuboresha huduma za NHIF. Kwanza ni kuondoa ukiritimba na figisu kwa wanachama. Nashauri wanachama wapewe uhuru wa kuchagua mfuko wa matibabu tofauti na sasa ambapo watumishi wote wa umma hulazimishwa kukatwa pesa na kutibiwa na NHIF watake wasitake. Wanachama wengi, ambao ni watumishi wa umma, wamechoshwa na vituko vya NHIF. Wanatamani wafunguliwe minyonyororo ya utumwa waliyofungwa kwa muda mrefu ndani ya NHIF wakatafute huduma nzuri kwenye mifuko mingine inayotoa bima za matibabu kama vile AAR, Momentum, Strategies, NMB, NSSF na mingine mingi tu iliyotapakaa hapa nchini.
Kwanini watu wanyimwe uhuru wa kujiunga na mifuko mingine ilhai kila siku NHIF inalalamika kuwa na hali mbaya ya kiuchumi? Ukiona hivyo ujue kuna manufaa ambayo serikali na watumishi wa NHIF wanayapata ambayo wakiruhusu watu waondoke, wanaweza kuyakosa. Kwa maana hiyo kumbe NHIF haipo kwa ajili ya maslahi ya wanachama bali ni kwa ajili ya maslahi ya serikali na wachumiatumbo wachache wasiopenda kuona watanzania wanakuwa na siha njema. Huu ni zaidi ya uhaini na uhujumu uchumi. Naomba TAKUKURU wafanye uchunguzi wa kina.
Ili NHIF iondokane na malalamiko ya gharama kubwa za matibabu kwa wanacham wake na kuhofia kufilisika, basi iwaachie wanachama waondoke mmoja mmoja waende wakatafute matibabu kupitia bima nyingine za afya. Wakibaki wanachama wachache inaweza kuwahudumia vizuri zaidi. Na hata hao wachache wakiamua kuhama, waachiwe waondoke. Wanachama wote wakishaondoka NHIF ifunge ofisi zake zote nchini na serikali iwapangie kazi nyingine waliokuwa waajiriwa wa NHIF. Kufikia hapo tatizo litakuwa limepata ufumbuzi wa kudumu. Huwezi kung’ang’ania jambo linakuuumiza kichwa wakati kuna ufumbuzi wa kudumu usiohitaji gharama yoyote.
Ikiwa serikali itafuata ushauri huu, itajiondoa jumla kwenye lawama za watanzania wanaokufa kila siku kwa sababu ya ubovu wa huduama za NHIF inayolalamika kutokuwa na fedha za kutosha kugharamia matibabu ya wanachama wake hadi kufikia hatua ya kufuta fao la Toto Afya Card na kuanzisha masharti ya kipuuzi kwa wananchma ambayo hayatekelezeki.
Nawasilisha.
Ilikuwa ni jukumu la serikali kumtibu mtumishi wa uma, ila ufisadi wa Mkapa akafuta akaanzisha haya mavi yanaitwa NHIF!Kuna tetesi kuwa serikali ilichota fedha NHIF na kupelekea mfuko kuwa taaban. Sasa hivi Nhif ni usumbufu mkubwa kila ukienda kutibiwa unakuta kuna foleni nyingine ya kuhakikiwa.