Serikali iangalie uwezekano wa kutoa mikopo kupitia halmashauri kwa mtu hata mmoja mmoja badala ya kulazimishwa kuwa katika kikundi

Serikali iangalie uwezekano wa kutoa mikopo kupitia halmashauri kwa mtu hata mmoja mmoja badala ya kulazimishwa kuwa katika kikundi

Huu ndio utakuwa mwanzo wa kufa kwa hiyo project.

Risk ya pesa kupotea kwa mtu mmoja ni kubwa kuliko kikundi.

Mtu mmoja anaweza kopa na kutokomea nazo ila kikundi ambacho members wote wapo verified atapatikana tu mmoja au baadhi yao kubeba mzigo in case of default.

Hili jambo lisifanyike.
 
Huu ndio utakuwa mwanzo wa kufa kwa hiyo project.

Risk ya pesa kupotea kwa mtu mmoja ni kubwa kuliko kikundi.

Mtu mmoja anaweza kopa na kutokomea nazo ila kikundi ambacho members wote wapo verified atapatikana tu mmoja au baadhi yao kubeba mzigo in case of default.

Hili jambo lisifanyike.
Nimetoa masharti na taratibu za kutoa mkopo kwa mtu mmoja,Soma Tena utaelewa namna ambavyo itakuwa ngumu kwa pesa kupotea bila kulipwa
 
Ndugu zangu watanzania,

Mfumo uliopo kwa Sasa juu ya pesa za halmashauri zinazotolewa Kama mkopo kwa vijana kutokana na makusanyo na mapato ya ndani unataka vijana au akina mama au watu wenye ulemavu kuweza kujiunga au kuunda kikundi cha kijasiriamali ili kuweza kupatiwa mkopo, ambapo hapa kuna taratibu za kufuata ili kukidhi vigezo Kama vile kutengeneza katiba, kuwa na akaunti ya kikundi, viongozi wa kikundi, mradi au wazo la mradi au biashara na mengineyo.

Ndugu zangu katika utolewaji wa pesa hizi hazitoi fursa kwa mtu mmoja mmoja kupatiwa mkopo, ukiwa kijana pekee huwezi ukapata mikopo hii hata Kama Ni muaminifu,una wazo zuri la biashara au mradi au una mradi au biashara ambayo ungependa uongeze na kukuza mtaji wako.

Hali hii inawanyima fursa vijana wengine ambao wanaona katika vikundi Kuna kuwa na baadhi ya changamoto Kama vile uaminifu mdogo kwa baadhi ya wanakikundi,kutofautiana kwa malengo, matumizi mabaya ya Fedha, uzembe wa baadhi ya wanakikundi, wengine kuchukua hela na kuishia kugawana pasipo kutumia katika malengo husika.

Kutokuwa na Elimu ya kutosha juu ya mradi au biashara tarajiwa na hivyo kuishia kupoteza mtaji wote kabla hata ya kurejesha, Haraka ya baadhi ya Wana kikundi au vijana kutaka utajiri wa haraka haraka na hivyo kuwekeza katika maeneo hatari wasio na uzoefu nayo au ujuzi nao zaidi ya habari za kusikia tu juu ya faida kubwa watakayoipata.

Hivyo nilikuwa naona Ni wakati wa serikali ya Rais wetu mpendwa mama Samia kuangalia uwezekano wa kutoa fursa ya mkopo kwa mtu hata mmoja mwenye kuhitaji mkopo huu huku wenye kuungana na kuwa kikundi nao waendelee kupewa Kama kawaida,hii itarahisisha na kusaidia vijana wengi Sana kuweza kupata mikopo na kuwasaidia vijana wengine hata kimawazo na kiushauri.

Vigezo vinavyoweza kutumika ni Kama vile uwepo wa Taarifa za kutosha juu ya mwenendo wa kiuadilifu, kiweledi, kimaadili, kiutendaji, kiuaminifu na kitabia kutoka katika uongozi wa serikali za mitaa.

Uwepo wa mdhamini anayeaminika na mwenye makazi ya kudumu katika eneo analotokea na kuishi kijana anayehitaji mkopo, mdhamini akubali kuwajibika endapo mhusika au kijana ataamua kukimbia au kutoroka kabla ya kurejesha pesa halmashauri.

Mdhamini asaiini fomu maalumu mbele ya mwanasheria wa serikali na kula kiapo cha kuwajibika juu ya Deni la anaye mdhamini na kopi ya fomu hiyo ibaki halmashauri ,nyingine kwa mwanasheria,nyingine kwa serikali ya mtaa ,nyingine kwa anayechukua mkopo na nyingine abaki nayo mdhamini.

Mdhamini awe na Mali zisizo hamishika na zenye hati inayotambulika kisheria,mdhamini awe Ni mzazi wa mhusika au mtu mwingine yeyote mwenye Mali zisizo hamishika na makazi ya kudumu eneo husika,Mdhamini akitaka kumdhamini mtu zaidi ya mmoja aruhusiwe mpaka pale tu itakapothibitika kuwa Mali za mdhamini Zina thamani kubwa ukilinganisha na mikopo au fedha inayotaka kuchukuliwa.

Hili Jambo litasaidia halmashauri kupata marejesho ya mikopo yote inayotolewa kwa vijana lakini pia itawasaidia vijana wengi kupata mikopo kwa urahisi bila mlolongo wa kutafutana na hata kuwalazimisha wengine ili wajiunge kwenye vikundi kusudi kutimiza lengo la kupata mkopo ambapo mwisho wa siku Hawa walio lazimishwa au kupachikwa kwenye kikundi kuweza kusaidia kupata mkopo wanakuwa hawana ule moyo au ufanisi mzuri na uwajibikaji mzuri na wanakuwa hawana mchango wowote ule katika kukuza ,kulinda na kuendeleza mtaji.

Naiomba Sana serikali iliangalie hili kwa jicho la kipekee kabisa, maana unakuta mtu unalima lakini unakosa hela ya pembejeo hasa mbolea kwa kuwa unawaza ukitaka mkopo wa kupanua kilimo chako inahitaji uende kwenye kikundi ambacho unajikuta nacho kina malengo mengine kabisa Kama vile ufugaji wa kuku wa mayai au ng'ombe wa maziwa ambapo unaona wewe huwezi ukapata hata nafasi ya kwenda kukatia ng'ombe majani au kuwawekea maji kuku kwa kuwa wewe shughuli zako Ni shambani muda mwingi na ndio Jambo unalolipenda kuliko ufugaji wa kuku wa mayai au nyama au ng'ombe wa maziwa.

Unakuta kikundi kimeundwa na kuomba mkopo wa Jambo fulani lakini Wana kikundi kila mmoja ana malengo yake kichwani juu ya hela ikiwa mkononi mwao, hivyo kupelekea mradi uliolengwa kukosa nguvu ya pamoja ya wanakikundi.

Kazi Iendeleee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu. 0742-676627
hata mabenki na taasisi zingine za kifedha zimeweka masharti hayo lkn bado watu hawalipi mikopo.watz bado tunadhani mikopo ni zawadi.la msingi ni kweli mikopo ya vikundi inasumbua sana na mfumo huo hauna tija kabisa.aangaliwe mtu mmoja mmoja ambaye yuko serious na biashara akopeshwe.pia kuna mapungufu makubwa kwenye utoaji wa fedha hizo kwa halmashauri.fedha nyingi hutolewa kwa watu ambao si sahihi.hutolewa kwa watu au vikundi ambavyo vina mahusiano na watendaji wa halmashauri.
 
hata mabenki na taasisi zingine za kifedha zimeweka masharti hayo lkn bado watu hawalipi mikopo.watz bado tunadhani mikopo ni zawadi.la msingi ni kweli mikopo ya vikundi inasumbua sana na mfumo huo hauna tija kabisa.aangaliwe mtu mmoja mmoja ambaye yuko serious na biashara akopeshwe.pia kuna mapungufu makubwa kwenye utoaji wa fedha hizo kwa halmashauri.fedha nyingi hutolewa kwa watu ambao si sahihi.hutolewa kwa watu au vikundi ambavyo vina mahusiano na watendaji wa halmashauri.
Naamini serikali yetu itafanyia kazi mawazo haya
 
Na katika hayo makundi alikuambia kama kuna uorodheshwaji wa mali unazomiliki zisimame kama dhamana?
Hapana,
Mkishakua kikundi ina maana hapo tayari mmedhaminiana hakutahitajika mali ya mmoja mmoja iwe kama dhamana.
 
Hapana,
Mkishakua kikundi ina maana hapo tayari mmedhaminiana hakutahitajika mali ya mmoja mmoja iwe kama dhamana.
Basi kwenu huko mna neemeka, huku mpaka muorodheshe mali zenu na baada ya hapo mnatakiwa mumtafute mdhamini mwingine mwenye mali zisizo hamishika asimame kama mdhamini

Mi niliwaambia watu kuwa mpo kwenye mkopo mwingine maana hayo masharti hayapo kwenye kanuni za mikopo ya halmashauri
 
Juzi nilienda kupata ABCD kama kijana nikaambiwa hayo hayo ya kikundi nilimchallenge yule dada Afisa Maendelo kuhusu kuruhusu mkopo wa mmoja mmoja akasema hilo suala limejadiliwa na sio muda Wizara itatoa tamko lakini hadi sasa kuna matumaini ya kuja kwa mikopo ya mtu mmoja mmoja,
Endelea kua karibu na Halmashauri yako utakuja kupokea habari njema.
Serikali ya tanzania hainaga haraka hiyo kuambiwa kuna uweza wa kuja kwa mikopo ya mtu mmoja mmoja inaweza kuchukua miaka 5 mbele..hapo ni hadi sera ifanyiwe marekebisho.
 
Basi kwenu huko mna neemeka, huku mpaka muorodheshe mali zenu na baada ya hapo mnatakiwa mumtafute mdhamini mwingine mwenye mali zisizo hamishika asimame kama mdhamini

Mi niliwaambia watu kuwa mpo kwenye mkopo mwingine maana hayo masharti hayapo kwenye kanuni za mikopo ya halmashauri
Halmashauri gani hiyo inaujinga hivyo..itaje tuifuatilie.
 
Ndugu Lucas hongera kwa uzi huu.
Nna maswali machache kwako kutokana na uzoefu wako au ulivyo shauri;

1.Serikali za mitaa huwa zinatunza taarifa za kila kijana hapo mtaani kama ulivyosema hapa "Vigezo vinavyoweza kutumika ni Kama vile uwepo wa Taarifa za kutosha juu ya mwenendo wa kiuadilifu, kiweledi, kimaadili, kiutendaji, kiuaminifu na kitabia kutoka katika uongozi wa serikali za mitaa"

2. Kama ndivyo kwy swali la kwanza, unaweza ukanipa majina ya hizo taarifa zinaitwaje na custodian wa hizo taarifa.

3. Umewahi kusikia watu wanaogopa mikopo ya benki kisa watauziwa mali zao hasa nyumba? Huoni hii itakua changamoto kwa watu kukubali kuwadhaminj hao vijana hofu ikiwa mali zao zinaweza taifishwa??

Nimependa ulivyozungumzia mfano wa mahitaji ya mbolea. Kuna namna wazo linaweza boreshwa na naona hili ni la maingi sana na halihitaji dhamana ya mtu mwingine kama likiboreshwa, shamba laweza kuwa dhamana.
 
Ndugu Lucas hongera kwa uzi huu.
Nna maswali machache kwako kutokana na uzoefu wako au ulivyo shauri;

1.Serikali za mitaa huwa zinatunza taarifa za kila kijana hapo mtaani kama ulivyosema hapa "Vigezo vinavyoweza kutumika ni Kama vile uwepo wa Taarifa za kutosha juu ya mwenendo wa kiuadilifu, kiweledi, kimaadili, kiutendaji, kiuaminifu na kitabia kutoka katika uongozi wa serikali za mitaa"

2. Kama ndivyo kwy swali la kwanza, unaweza ukanipa majina ya hizo taarifa zinaitwaje na custodian wa hizo taarifa.

3. Umewahi kusikia watu wanaogopa mikopo ya benki kisa watauziwa mali zao hasa nyumba? Huoni hii itakua changamoto kwa watu kukubali kuwadhaminj hao vijana hofu ikiwa mali zao zinaweza taifishwa??

Nimependa ulivyozungumzia mfano wa mahitaji ya mbolea. Kuna namna wazo linaweza boreshwa na naona hili ni la maingi sana na halihitaji dhamana ya mtu mwingine kama likiboreshwa, shamba laweza kuwa dhamana.
Katika swali la kwanza ningependaa kukujibu kuwa is huku mikoani tuna vijiji na vitongoji ,Ambapo Kuna kuwa na Mwenyekiti wa Kijiji na kitongoji,kijana anaweza asifahamike vizuri kwa hao viongozi wawili lakini Kuna kiongozi chini Yao anayeitwa Balozi au mjumbe,huyu kwa kiasi kikubwa anawafahamu vizuri Sana watu wake,hata ukitaka kupata taarifa za ndani juu ya mtu fulani Ni Rahisi Sana kupata kupitia watu Hawa.

Pia swala la kwamba watu wataogopa kuuziwa Mali zao hapo ndipo usalama wa fedha za halmashauri utakapokuwepo maana atakayechukua na kukubalika kudhaminika maana take Ni yule anayeaminika vizuri Sana na mdhamini,Hivyo Jambo hili litasaidia halmashauri kupata marejesho ya mkopo wake bila wasiwasi na kusaidia vijana wengine wengi kunufaika,
.
Pia mikopo hii itatolewa kwa vijana waaminifu tu maana ili mdhamini akudhamini Ni lazima awe amejihakikishia na kujiridhisha juu ya weledi uaminifu na umakini wa kijana husika na uwezo wa kuisimamia kuilinda na kuiendeleza pesa atakayopatiwa Kama mkopo
 
Basi kwenu huko mna neemeka, huku mpaka muorodheshe mali zenu na baada ya hapo mnatakiwa mumtafute mdhamini mwingine mwenye mali zisizo hamishika asimame kama mdhamini

Mi niliwaambia watu kuwa mpo kwenye mkopo mwingine maana hayo masharti hayapo kwenye kanuni za mikopo ya halmashauri
Khee!
Kweli hao wapo kwenye mkopo mwingine, mikopo ya Halmashauri haina mambo mengi kubwa ni hilo la kikundi kusajiliwa hapo mtajidhamini wenyewe, katiba, akaunti na utambulisho wa serikali ya Mtaa.
 
Katika swali la kwanza ningependaa kukujibu kuwa is huku mikoani tuna vijiji na vitongoji ,Ambapo Kuna kuwa na Mwenyekiti wa Kijiji na kitongoji,kijana anaweza asifahamike vizuri kwa hao viongozi wawili lakini Kuna kiongozi chini Yao anayeitwa Balozi au mjumbe,huyu kwa kiasi kikubwa anawafahamu vizuri Sana watu wake,hata ukitaka kupata taarifa za ndani juu ya mtu fulani Ni Rahisi Sana kupata kupitia watu Hawa.

Pia swala la kwamba watu wataogopa kuuziwa Mali zao hapo ndipo usalama wa fedha za halmashauri utakapokuwepo maana atakayechukua na kukubalika kudhaminika maana take Ni yule anayeaminika vizuri Sana na mdhamini,Hivyo Jambo hili litasaidia halmashauri kupata marejesho ya mkopo wake bila wasiwasi na kusaidia vijana wengine wengi kunufaika,
.
Pia mikopo hii itatolewa kwa vijana waaminifu tu maana ili mdhamini akudhamini Ni lazima awe amejihakikishia na kujiridhisha juu ya weledi uaminifu na umakini wa kijana husika na uwezo wa kuisimamia kuilinda na kuiendeleza pesa atakayopatiwa Kama mkopo
Asante kwa majibu nimekuelewa vyema.
 
Khee!
Kweli hao wapo kwenye mkopo mwingine, mikopo ya Halmashauri haina mambo mengi kubwa ni hilo la kikundi kusajiliwa hapo mtajidhamini wenyewe, katiba, akaunti na utambulisho wa serikali ya Mtaa.
Naskia hiyo fomu ipo kabisa imeandika vigezo hivyo na wao wakopaji wanaambiwa na Afisa maendeleo jazeni tu haina shida yeyote na watu wana tii

Ngoja nikiipata hiyo fomu ntaiweka hapa muione
 
Naskia hiyo fomu ipo kabisa imeandika vigezo hivyo na wao wakopaji wanaambiwa na Afisa maendeleo jazeni tu haina shida yeyote na watu wana tii

Ngoja nikiipata hiyo fomu ntaiweka hapa muione
Sawa ukiipata iweke, maana hata mie nimeshangaa
 
Sawa ukiipata iweke, maana hata mie nimeshangaa
Nimezipata kumbe ziko pages zaidi ya 10, ila vipengele vya udhamini ziko pages 3 covid 19

FOMU ZA MAOMBI YA MKOPO-3.jpg

FOMU ZA MAOMBI YA MKOPO-4.jpg


Hapa ndio sehemu anayojaza mdhamini
FOMU ZA MAOMBI YA MKOPO-5.jpg
 
Haya mashart Kwa kikundi cha watu 20 wanapewa milion 200 au
Kwanza naskia waliokuwa na mipango ya kukopa M50 walivyoitwa kwenye semina wakashushwa hadi 20M na bado hizo ni ahadi yani hawajapewa

Wametumia pesa nyingi wengine wanadai wametumia zaidi ya 500K na bado hakuna dalili za wao kupata mkopo
 
Back
Top Bottom