Serikali iboreshe sheria ya Ndoa za Kikristu ili ziruhusu talaka kuepusha mauaji na fumanizi

Talaka ndio mwanzo wa kuwa na watoto wasiojua ni maana ya kuwa baba au kuwa mama. Na talaka husababishwa tabia za kizinifu.
Kama hutokuwa mvumilivu utatembea na wanawake zaidi hata ya elfu moja , kutokana hakuna mkamilifu swala ni uvumilivu
 
JEHOVAH Ndiye YESU KRISTO?
Hapana .
JEHOVAH ni MUNGU wa Israel , ambaye ndiye aliyeumba kila kitu. MUNGU huyu aliabudiwa na manabii waliotokea Israel Musa , Daudi., na manabii wote wa biblia , kwa nini wa Israel - dunia ilipotoka watu wakaabudu kwenye Miungu ya uongo(Fallen Angels) kwa hiyo MUNGU Alitengeneza taifa liwe mfano wa kuigwa na mataifa mengine ambalo ndo Israel , ndio maana manabii wote wanatokea Israel
Yesu ni kiumbe wa kwanza kuumbwa na MUNGU na baadae alihusika katika uumbaji(mbingu na nchi) na hii ilikuwa ni kabla ya kutumwa na MUNGU kuja duniani kutufundisha jinsi ya kuishi maisha kama ya mbinguni ili tufikie vigezo vya kuishi mbinguni Wakolosai 1:15-17 "Kristo ni mfano wa Mungu asiyeonekana; ni mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote. Maana kwake vitu vyote viliumbwa kila kitu duniani na mbinguni, vitu vinavyoonekana na visivyoonekana: Wenye enzi, watawala, wakuu na wenye nguvu. Vyote viliumbwa kwake na kwa ajili yake. Yeye alikuwako kabla ya vitu vyote; vyote huendelea kuwako kwa uwezo wake."
 
Nani aliyekwambia kuwa ndoa za Kikristo hazina talaka? Hiyo ni misconception. Ndoa zote nchi hii zinaratibiwa na sheria ya ndoa ya mwaka 1971.

Hata hao wanaofungisha ndoa za kidini wanapewa leseni na serikali.

Sheria hiyo imeruhusu mtu yeyote bila kujali dini yake kwenda mahakamani kuvunja ndoa kwa kupeleka maombi mahakamani. Ila tu sheria hiyo imeweka sababu mahususi za kuvunja ndoa ambazo zikiwepo basi ndoa itavunjwa szisipokuwepo haivunjwi.

Hivyo mleta uzi nadhani hukuwa na taarifa sahihi.
 
Vipi kwa wanao fungisha ndoa za kimila , Je ndoa ya kimila haitambuliki na serikali na wafungishaji wa ndoa za kimila(wazee wa ukoo) wamepewa kibali na serikali?
 
Hakuna cha ghafla, ukiikuta mezani aidha umeiomba au umepewa na kwa maana hiyo mapenzi yameisha hapo. Chukua talaka yako endelea na maisha yako. Penzi la kung'ang'aniza ni hatari.
 
Hakuna cha ghafla, ukiikuta mezani aidha umeiomba au umepewa na kwa maana hiyo mapenzi yameisha hapo. Chukua talaka yako endelea na maisha yako. Penzi la kung'ang'aniza ni hatari.
Vipi kwa watoto, wataishi vizuri. mana hapo naona kuna element za ubinafsi. Kwa mfano mimi nimelelewa na mzazi mmoja yani mam najua nini maana ya kulelewa na mzazi mmoja. Vipi ambao baba yao yupo duniani na mama pia yupo duniani but hawapati upendo na malezi ya pande hizi mbili , Ukiangalia kwa undani , kwa wanaume ni tamaa au hamu ya uyo mwanamke imemuishia na mwnamke huwa pesa imemuishia mwamme ndo mana wameachana
 
-Kiufupi Mkuu,bado una uelewa mdogo wa masuala ya sheria hasa sheria ya ndoa (Tanzania Marriage Act 1971) pamoja na mawazo hafifu kuhusiana na katiba ya nchi.Kuna a lot of limitations zilizowekwa na katiba juu ya serikali kuingilia mambo haya ya kidini na ndoa ikiwemo kama ulivyoainisha hapo juu.
-Katiba inatoa uhuru kwa raia wa Tanzania wa kuabudu wanachokiamini,na sheria ya ndoa ambayo iliundwa na ambayo ni consistent na katiba inatambua hilo-Na hata mashauri ya talaka mahakamani yanazingatia sana miongozo ya ulipofungia ndoa (kanisani,msikitini nk.) katika kuamua mashauri yake.

Role ya Wafunga ndoa.
-Wafunga ndoa wamepewa choices kwa mujibu wa sheria ya Tanzania,na kila choices huambatana na wajibu wake pamoja na consequences zake.Mfano-Choice ya kuamua kufunga ndoa ya kiserikali ambayo haifungwi na mambo ya imani.Choice ya kufunga ndoa ya kidini,choice ya kufunga ndoa ya kimila and so on.
-Kila choice unayoifanya inafungwa na taratibu zake,sheria zake,wajibu,tamaduni zake etc.Hivyo ni wajibu wa mwanandoa mtarajiwa kuelewa taratibu za dini husika au dhehebu kiundani kabla ya kufunga ndoa.Tendo hili ni la hiari
-Ukiangalia kiundani utaona sheria imekupa kila aina ya choices (uhuru wa kuamua) kwendana na matakwa ya kikatiba.
- Wanandoa wanatia saini kwenye vyeti vya ndoa kuonesha kukubaliana na yaliyomo kwenye mkataba huo-Unakuwa mkataba Rasmi unaotambulika kisheria pale unapotia sahihi na pande husika ikiwemo mashahidi nk. na kuzingatia taratibu zote halali kwa mujibu wa sheria.
-Tendo la kufungisha ndoa limekaa kiimani zaid kuliko kiserikali hvyo utaona serikali ina role ndogo sana.

*Changamoto nyingi katika maswala haya hujitokeza hasa pale wahusika wanapokuwa wanaongozwa zaid kihisia kuliko kufikiria sawasawa juu ya wajibu mzito uliopo mbele yao (kutokupevuka).Wahusika wanaotarajia kufunga ndoa kutokuelewa sheria na Taratibu za nchi na kiimani kwa ufasaha nk.Mfano- haiwezekani wahusika kufunga ndoa kikristo halafu kutaka kuishi kwendana taratibu za ndoa za kiislam nk.
*Tafiti yako ina base kwenye upande mmoja tu-Unazungumziaje trend inayoongezeka ya wachumba ambao wanauana kabla ya ndoa katika jamii yetu? Unazungumziaje trend ya michepuko kushiriki kuua baadhi ya wanandoa? nk.The problem is very very wider

Who to blame.
-Wanaopaswa kulaumiwa kwa changamoto hz ni wanandoa wenyewe husika kwa kutokufanya machaguo sahihi ya nn wanafanya na wajibu wao ni nn,na consequences ni zipi hasa nk.
 
Itakuwa na maana gani pale mtu anajinasibu ni Muislamu au Mkristo ilihali haziishi au kuziamini taratibu,sheria,kanuni nk za imani husika? Je,Serikali kumtambua mtu tu kama mkristo au muislam ingawa haiishi imani yake inaweza kumwongezea maana yeyote? These are hard questions to ask ourselves.
 
Sidhani kama mwamba ameoa au kama ndivyo basi atakua anakaa na mwenza tu kisela kama sio basi si mkristo na hajui utaratibu wa taraka ukoje

Sent from my SM-G9350 using JamiiForums mobile app
 
Hata uking'ang'ania hapo wakati upendo umeisha sio guarantee kwamba watoto wataishi vizuri tena inaweza ikawa mbaya sana. Sometimes tunavumilia mateso sababu ya watoto wakati kumbe watoto wanajiuliza kwa nini huondoki kwani wanateseka kukuona wewe ukiteseka. Unaweza kwenda mahakamani ukadai matunzo ya watoto, otherwise unapambana tu dear Mungu anasaidia. Muhimu amani.
 
Kutengana kwa baba na mama. Ndo mwanzo wa kupata mashoga, au wanaume wenye tabia ambazo si za kiume au kama ni mtoto wakike kalelewa na baba anakuwa na tabia za kiume. Mtoto wa kiume anakuwa hawezi kuafanya kazi za kiume kama kujenga banda la kuku . Mtoto hata kama akipewa kila kitu bado upendo wa mama na baba unamtengeneza mtoto, ndio mana MUNGU akamfanya baba na mama - kila mtu anachakuchangia katika ukuaji wamtoto. Ili kusuluisha inabidi mmoja ajishushe momja ajifanye Lofa ili manufaa yatoke makubwa kiroho na kimwili
 
Kwa walio oa wanafahamu kuwa cheti cha ndoa unachopewa SIO cha kanisa, ni cha serikali.
Kanisa halina cheti (hapa nazungumzia katoliki ambalo nina uzoefu nalo, mengine sijui kama wanavyo). Hata mashahidi wa ndoa ni matakwa ya serikali. Kanisa limeamua kuchukulia advantahe ya wao kuwapo na kuwapa majukumu kama wasimamizi wa ndoa. Kiuhalisia unaweza kuwa na msimamizi wa ndoa ambaye hata kanisani kwenye ndoa yako hakuja. Kabla ya kubisha uliza watu waliobobea sheria za kanisa. Hii hata mapadre wengine inawatatiza.
Ukiona ndoa imekushinda kwa sababu inayofaa, nenda mahakamani utapata talaka yako kiserikali. Hiyo ni hatua moja.
Kisha unaweza kwenda kanisani nako ukaomba talaka. Hapa ni pagumu lakini zinatoka japo chche. Sanasana inaishia kwenye separation lakini sio divorce.
Talaka ya mahakamani itakusaidia katika mambo ya kidunia. Mgawanyo wa mali, n.k
Talaka ya kanisani itakusaidia after life, just in case ....
 
Vipi kwa wanao fungisha ndoa za kimila , Je ndoa ya kimila haitambuliki na serikali na wafungishaji wa ndoa za kimila(wazee wa ukoo) wamepewa kibali na serikali?
Ndoa ya kimila inatambulika na sheria ya ndoa ya Tanzania. Tizama kifungu cha 25 (1) (d).
 
Duh jf ina wajenga hoja wazuri sana
SWALI: kuna rafiki yangu ndoa ilifungwa KKKT, wakazaa watoto watatu, mke akazingua na kutoka nje ya ndoa, jamaa akamkamata lkn hakutaka skendo ikaisha kimya kimya bila kukusanya ushahidi, baadae fununu zikazagaa kwamba mkewe anaendelea kimahusiano na mgoni wake, yeye akachukua hatua mwenyewe.
Akamwambia mkewe tukiendelea kuishi pamoja iko siku nitakuua, nifungwe, watoto wakose wa kuwatunza. Akamtimua mkewe nyumbani, mke akaitisha vikao vya usuluhishi jamaa akagoma, akabaki na wanae mwaka wa kumi sasa. Akachukua mwanamke mwingine kimila akaoa
Je anaweza kuvunja ndoa ya kwanza kisheria ili mke mdogo apate haki zake kama mke halali? Utaratibu ni upi? Kwa mwenye mawazo na ushauri karibu
 
Labda ndoa za kikristo kung'ang'ania mke mmja wakati sio utamaduni wa kiafrika,ujinga huo huwezi ukuta kwa Waislamu maana wao dini yao inaakisi tamaduni ya kiafrika na mfumo dune,habari za haki sawa sijui empowerment kwenye ndoa hakuna huo ujinga.

Nimewahi kuandika kwamba ndoa za kiislamu zinadumu na zina Furaha kuliko ndoa za kikristo.
 
Utamaduni wa Kiafrika ni kumkeketa mwanamke, Mkeo na mtoto wako wa kike umewakeketa?
 
Sasa huo ushahidi sasa ndio shida,afu nasikia eti ukienda mahakamani kutaka kuachana wanaanza kukuzungusha yaani wanakataa will yako hususani kama mwenza hataki,hii sasa mahakama na mabalaza yanaanzaje kunilazimisha? Kwani wakati naoa niliwashirikisha?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…