nyapinyapileo
Member
- Oct 19, 2022
- 92
- 215
Wana Jamii Forums nawasalimu nyote
Mimi ni mkazi wa wilaya ya Kibondo hapa mkoani Kigoma. Ninaomba msaada wa kisheria kutokana na ugomvi nilionao na kampuni ya KITAPELI ya sola inayoitwa MYSOL maana tunakoenda naweza kuja kukata kichwa cha mfanyakazi wao nikapata kesi ya mauaji.
Hii kampuni hukopesha mitambo ya sola ambapo mteja hutakiwa kulipa malipo ya awali kutegemea na ukubwa wa sola mfano Tsh.180,000 au 300,000,kisha malipo mengine hutakiwa kulipa kidogokidogo mpaka atakapomaliza mkataba wake.
Hii ni kampuni ya KITAPELI kama si KIJAMBAZI. Mwezi Februari mwaka huu niliingia mkataba wa sola ya watt 180 ambapo baada ya kulipa malipo ya awali ya shilingi laki mbili, niliendelea kulipa kila siku kidogokidogo na mpaka leo tarehe 24 nimeshalipa jumla ya shilingi 1,688,000 kati ya shilingi 2,700,000.
Kama mnavyofahamu,wiki iliyopita Raisi kazindua Gridi huku Kigoma nami ni mmoja kati ya wananchi tuliounganishwa na umeme wa TANESCO.
Jambo la kushangaza ni kwamba haya MAJAMBAZI YA KAMPUNI YA MYSOL bado yanataka eti niendelee kulipia sola yao wakati nimeshapata umeme wa TANESCO ambao kwangu ni rahisi na nafuu kuliko MISOLA YAO YA KIPUMBAVU. Tangu nimefunga hilo LISOLA lao limekuwa likinisumbua mara kwa mara na wao kuja kurekebisha ni mpaka wajisikie wao kuja. Nilishagombana nao sana lakini niliendelea kuvumilia.
Kwa kuwa tayari nina umeme wa TANESCO, Sola nimeitoa na kuiweka ndani. Nashangaa wanakuja na Polisi eti kuichukua kwa sababu siilipi tena, je pesa yangu shilingi 1,688,000 nitaipataje?wananijibu hiyo pesa HAIRUDISHWI. Kwa kweli nimewazuia hao maofisa wa hiyo kampuni pamoja na polisi wawili waliokuja nao.
Naomba kama kuna mwana JF aliyewahi kudili na haya MAJAMBAZI YA MYSOL anipe msaada wa jinsi ya kukabiliana nayo maana nasikia HARUFU YA KUMWAGA DAMU wakija tena kutaka kuchukua kwa nguvu maana wameahidi kuja kuchukua na bunduki. Na tupo wananchi 7 ambao haya MAJAMBAZI YA MYSOL yamekuja yanataka KUTUDHULUMU. Msaada tafadhali
Nawasilisha
Mimi ni mkazi wa wilaya ya Kibondo hapa mkoani Kigoma. Ninaomba msaada wa kisheria kutokana na ugomvi nilionao na kampuni ya KITAPELI ya sola inayoitwa MYSOL maana tunakoenda naweza kuja kukata kichwa cha mfanyakazi wao nikapata kesi ya mauaji.
Hii kampuni hukopesha mitambo ya sola ambapo mteja hutakiwa kulipa malipo ya awali kutegemea na ukubwa wa sola mfano Tsh.180,000 au 300,000,kisha malipo mengine hutakiwa kulipa kidogokidogo mpaka atakapomaliza mkataba wake.
Hii ni kampuni ya KITAPELI kama si KIJAMBAZI. Mwezi Februari mwaka huu niliingia mkataba wa sola ya watt 180 ambapo baada ya kulipa malipo ya awali ya shilingi laki mbili, niliendelea kulipa kila siku kidogokidogo na mpaka leo tarehe 24 nimeshalipa jumla ya shilingi 1,688,000 kati ya shilingi 2,700,000.
Kama mnavyofahamu,wiki iliyopita Raisi kazindua Gridi huku Kigoma nami ni mmoja kati ya wananchi tuliounganishwa na umeme wa TANESCO.
Jambo la kushangaza ni kwamba haya MAJAMBAZI YA KAMPUNI YA MYSOL bado yanataka eti niendelee kulipia sola yao wakati nimeshapata umeme wa TANESCO ambao kwangu ni rahisi na nafuu kuliko MISOLA YAO YA KIPUMBAVU. Tangu nimefunga hilo LISOLA lao limekuwa likinisumbua mara kwa mara na wao kuja kurekebisha ni mpaka wajisikie wao kuja. Nilishagombana nao sana lakini niliendelea kuvumilia.
Kwa kuwa tayari nina umeme wa TANESCO, Sola nimeitoa na kuiweka ndani. Nashangaa wanakuja na Polisi eti kuichukua kwa sababu siilipi tena, je pesa yangu shilingi 1,688,000 nitaipataje?wananijibu hiyo pesa HAIRUDISHWI. Kwa kweli nimewazuia hao maofisa wa hiyo kampuni pamoja na polisi wawili waliokuja nao.
Naomba kama kuna mwana JF aliyewahi kudili na haya MAJAMBAZI YA MYSOL anipe msaada wa jinsi ya kukabiliana nayo maana nasikia HARUFU YA KUMWAGA DAMU wakija tena kutaka kuchukua kwa nguvu maana wameahidi kuja kuchukua na bunduki. Na tupo wananchi 7 ambao haya MAJAMBAZI YA MYSOL yamekuja yanataka KUTUDHULUMU. Msaada tafadhali
Nawasilisha