Serikali ifanye maamuzi magumu ya kupiga marufuku bodaboda mjini, zitumike vijijini ili kupungiza ajali au iweke kodi kubwa

Tatizo ni kuwa serkali haibuni ajira kwa vijana
Serkali ikizuia bodaboada bila kubuni ajira nyingine tarajia ujambazi wa kutisha km miaka ya 90
 
Nchi hii kuna viongozi wa ajabu sana.Walivipiga marufuku Vipanya vya abiria 20 kuingia katikati ya jiji la Dar ila wakaruhusu bodaboda na bajaj kuingia katikati ya jiji
Bajaji zilianza Route moja tu ya kariakoo Kivukoni kwa ajili ya walemavu. Sasa hiv mjini kote ni bajaji na bodaboda tupu.
Tunaenda kufanana India soon.
Yaan waliondoa Daladala na kuruhusu bajaji
 
Tatizo umasikini ushafanya mpaka boda boda imekuwa ajira, sio rahisi hili kufanyika.
 
Naunga mkono hoja. Tujiulize tu kabla ya ujio wa bodaboda kama njia ya usafiri tulikuwa tunatatua vipi changamoto za usafiri.

Kiukweli tumejiendekeza tu kupanda bodaboda. Imagine mtu anatoka TRA Longroom pale karibu na Central Police anakodi boda kwenda Askari Monument??

Bodaboda zitumike kuwatoa watu swekeni kama Mabwepande kuwaleta Bunju A. Baada ya hapo daladala ziendelee kubeba watu wa main roads
 
Kwa anayefahamu dynamics za ukuaji wa miji kiholela km inavyotokea kwa miji mingi Africa na pace ya maendeleo kwa ujumla huwezi zuia boda boda, tafuta namna ya kupambana na uvunjifu wa sheria unapotokea..si boda boda wote ni wavunjifu wa sheria.
 
Serikali yoyote duniani huwalinda huwalinda wananchi wake. Kuna kipindi serikali ya nchi moja ya Ulaya ilipiga marufuku kuendesha skuta za kukodi wakati wa usiku baada ya kuona vijana wengi wanapata ajali wakati wanatoka night club!
Wanakwambia wamepata ajira.watakuja kula kwako?
 
Issue ya bodaboda wanaichukulia poa. Ila naamini tukipata takwimu vizuri za ajali za bodaboda kwa mwezi, siziopikwa. Ni hatari
 
Kwa tulipofikia ni vigumu kuzuia hiyo biashara, watawala nao wanapenda waendelee kutawala hawana haja ya kutafuta purukushani. Cha muhimu japo wengi niliona wakilaumu aliyechukua video kwenye Lile tukio wakidai ilibidi akafanye uokozi badala ya kuchukua video. Sasa bila video kama hizo kuwafikia hao bodaboda Kona zote za nchi wakajionea ikawa Somo unafikiri wataelewa? Elimu itolewe zaidi, tusifiche matukio ya ajali ziwekwe wazi waone kinachotokea.
 
Wanakwambia wamepata ajira.watakuja kula kwako?
Kuwekewa sheria na kanuni za kuwalinda ajali kutawafanya waje kula kwangu? Bodaboda inatakiwa walindwe kwa kudhibitiwa. Serikali yoyote inayowajibika huwa inachukuwa hatua pale inapoona madhara yanatokea
 
Kuwekewa sheria na kanuni za kuwalinda ajali kutawafanya waje kula kwangu? Bodaboda inatakiwa walindwe kwa kudhibitiwa. Serikali yoyote inayowajibika huwa inachukuwa hatua pale inapoona madhara yanatokea
Kumbe hata wewe haujui mleta mada anataka nini.haya soma tena uelewe
 
Nadhani kwa busara tusingesema Serikali ipige marufuku bali iboreshe usafiri wa UMMA ili kusiwepo na ulazima wa Bodaboda in the first place...

Lakini what do I know...., Ni kama unalaumu watu kutumia vidole kula tambi wakati hakuna umma wala vijiti.....
 
Kumbe hata wewe haujui mleta mada anataka nini.haya soma tena uelewe
Nimeelewa vizuri kabisa. Tatizo ni kuwa hujui nilichojibu nini. Mimi nimejibu comment iliyosema kuwa serikali haipaswi kufanya lolote kwa sababu wao bodaboda hawajihurumii. Mimi nikatoa mfano wa nchi ya Ulaya iliyokataza watu kuendesha skuta za kukodi wakati wa usiku kwa sababu walevi wengi walikuwa wanaziendesha wakiwa wamelewa na kupata ajali. Yaani nimeonyesha maana ya serikali kujali wananchi wake i.e. serikali kuweka sheria. Upo?
 
Kumbe hata wewe haujui mleta mada anataka nini.haya soma tena uelewe
Tena ni wewe uliye-suggest kuwa bodaboda wanatakiwa kujionea huruma ndiyo nikakupa mfano wa serikali kuwajibika kwa kuweka sheria!!
 
Ni kweli hawajihurumii.hakuna watoto pale.hata useme uwachape fimbo hawatasikia.kikubwa acha wafe.wenye akili watazingatia sheria za barabarani.dunia ya sasa si yakuoneana huruma.jihurumie kwanza wewe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…