DOKEZO Serikali Ifanye Uchunguzi Wa Kifo Cha Dkt Faustine Ndugulile Na Kuongeza Ulinzi Mzito Kwa Dkt Tulia Ackson

DOKEZO Serikali Ifanye Uchunguzi Wa Kifo Cha Dkt Faustine Ndugulile Na Kuongeza Ulinzi Mzito Kwa Dkt Tulia Ackson

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Lakini ni wakati pia wa kumuangalia Dkt Tulia kwa jicho la kijasusi zaidi kwa kujua kuwa anawakilisha Taifa letu huko Nje ya Nchi.hivyo ni Muhimu kumuongezea ulinzi zaidi awapo ndani na nje ya Nchi.Maana ikumbukwe ya kuwa hata katika kugombea hakugombea peke yake na hivyo siyo kila mmoja anapenda kuona Taifa fulani likiwa linang'ara katika nafasi za kimataifa kama ambavyo ilikuwa tumepata kwa Dkt Faustine Ndugulile kuongoza WHO kanda ya Afrika pamoja na kuwa na Dkt Tulia upande wa IPU.
Una very narrow thinking capacity, hivi unajua teknolojia ina nguvu kiasi gani miaka hii? Siku hizi ulinzi uko akilini mwako, there is nothing kwenye hao wenye magwanda na bunduki
 
Acha ujinga wako hapa wewe.
Lucas,wewe ni kati ya macomrade was hovyo sana na hamjui hasa Nini kinaendelea japo mpo mijini na una connection ya watu wakubwa ulipo!!

Mimi nipo chaka sana lakini najua nini kinaendelea kupitia maandiko mengi ya humu!!

Huu ushindi ambao na Mimi nimehusika kukisaidia chama changu ndio uke ule wa mwaka 2019 na matukio yatakayofuata ni Yale yale!

Unaposikia TEC kupitia kitima wanapiga kelele maana yake Wana jambo lao!

Kifupi ataliwa kichwa huyo unaejifanya wewe ni chawa mkuu!!

Hatogombea na akigombea ujue nchi itaenda upinzani!!!

SOMA MAKINIKA UTAELEWA ,ACHA UCHAWA NA UZWAZWA!!
 
Tubuni maana mwenyezi mungu hapangiwi wa kumchukua.........sasa endeleeni na sarakasi zenu muone kama hamjaisha ............hakuna ujanja ujanja kwenye mambo ya mungu hata mkichunguza..........vipi kwa kibao kuna mlichoona maana ile ilkuwa kazi yenu mboga mboga hata sio ya mungu
 
Tubuni maana mwenyezi mungu hapangiwi wa kumchukua.........sasa endeleeni na sarakasi zenu muone kama hamjaisha ............hakuna ujanja ujanja kwenye mambo ya mungu hata mkichunguza..........vipi kwa kibao kuna mlichoona maana ile ilkuwa kazi yenu mboga mboga hata sio ya mungu
Acha uzushi wako hapa.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Ifike mahali kama Taifa tusikubali kila kifo kipite hivi hivi au kuacha mambo yaende hivihivi kana kwamba hakuna kilichotokea vile au kusema ni Mapenzi ya Mungu au kuona ni kawaida.Mungu ametupatia akili kwa ajili ya kufikiri na kufanya tafakari kwa msaada wake Mungu Mwenyewe.

Ikumbukwe hii ni Dunia yenye vita vya kila aina ikiwepo kuhujumiana,kudhoofishana na kumalizana kwa kila mbinu .ambavyo vinakuwa vinafanywa kwa akili na maarifa ya hali ya juu sana na kufanywa na watu wenye akili za hali ya juu sana na ambao wapo kwa ajili ya kazi hiyo tu na wamefundishwa na kuivishwa kisawasawa.

Ifahamike kuwa wakati Mwingine kama Taifa linaweza kumalizwa na kutafunwa kama ugonjwa wa kansa kwa kumalizwa viongozi wake hasa wale wenye maono,akili kubwa,upeo,maarifa na ufahamu mkubwa wa masuala mbalimbali.watu wanaweza wakawa wanamaliza viongozi na watu wako muhimu pasipo wewe kujua .unapokuja kushituka ni wakati huna uwezo wa kusimama tena kukabiliana na hujuma hizo kwa sababu unakuwa tayari umepoteza watu wote wale wa muhimu.

Hivyo ni muhimu sana tuanze utaratibu wa kufanya uchunguzi wa vifo vya watu wa muhimu au viongozi pale inapotokea vifo vya ghafla na vyenye kutatanisha ili kuweza kujua ni vifo vya Mungu au vyenye mikono ya Binadamu. Kumbukeni hapa Majuzi tu tumepoteza kiongozi mashuhuri na muhimu sana hapa Nchi ambaye ni Mafuru.na sasa tumempoteza mwingine mtu wa muhimu sana kwa Taifa letu Dkt Faustine Ndugulile.

Lakini tujiulize huko India tumepeleka viongozi wetu wangapi katika kumbukumbu zetu na wangapi wamepoteza Maisha. Ni wakati wa kufumbua macho sasa kama Taifa kwa idara zetu za Ujasusi ndani na nje ya Nchi katika ulinzi wa viongozi wetu muhimu na watu muhimu.maana kuhujumiwa unaweza kuhujumiwa kwa njia mbalimbali ikiwepo hata wafanyabiashara wako wakubwa na wenye mitaji mikubwa na wenye mchango mkubwa kwa Taifa kupotezwa.

Lakini ni wakati pia wa kumuangalia Dkt Tulia kwa jicho la kijasusi zaidi kwa kujua kuwa anawakilisha Taifa letu huko Nje ya Nchi.hivyo ni Muhimu kumuongezea ulinzi zaidi awapo ndani na nje ya Nchi.Maana ikumbukwe ya kuwa hata katika kugombea hakugombea peke yake na hivyo siyo kila mmoja anapenda kuona Taifa fulani likiwa linang'ara katika nafasi za kimataifa kama ambavyo ilikuwa tumepata kwa Dkt Faustine Ndugulile kuongoza WHO kanda ya Afrika pamoja na kuwa na Dkt Tulia upande wa IPU.

Kwa hiyo kwa nafasi ambazo watanzania wanapata kuongoza taasisi za kimataifa tuhakikishe tunaongeza ulinzi ikiwepo kwa yule ambaye yupo kwenye masuala ya Fedha. Tukilala unaweza shangaa unafanyiwa hujuma na kupigwa mapigo makubwa makubwa mahali panapouma na kuacha majeraha,mapengo na alama zisizofutika wala kuzibika.

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Alipouawa Ally Kibao na vyombo vya Tanzania mbona ulikejeli, Leo mtu ambaye hakutekwa kwenye basi kafia India wala sio Ununio unamlalamikia nani?

Bila shaka wewe ni mjinga
 
Lucas,wewe ni kati ya macomrade was hovyo sana na hamjui hasa Nini kinaendelea japo mpo mijini na una connection ya watu wakubwa ulipo!!

Mimi nipo chaka sana lakini najua nini kinaendelea kupitia maandiko mengi ya humu!!

Huu ushindi ambao na Mimi nimehusika kukisaidia chama changu ndio uke ule wa mwaka 2019 na matukio yatakayofuata ni Yale yale!

Unaposikia TEC kupitia kitima wanapiga kelele maana yake Wana jambo lao!

Kifupi ataliwa kichwa huyo unaejifanya wewe ni chawa mkuu!!

Hatogombea na akigombea ujue nchi itaenda upinzani!!!

SOMA MAKINIKA UTAELEWA ,ACHA UCHAWA NA UZWAZWA!!
Ushetani ndio umekujaa kichwani mwako na kutumikishwa na shetani.
 
Back
Top Bottom