DOKEZO Serikali imchunguze Mwalimu huyu wa Shule ya Mandimu (Singida), matendo yake ni tishio kwa Wanafunzi

DOKEZO Serikali imchunguze Mwalimu huyu wa Shule ya Mandimu (Singida), matendo yake ni tishio kwa Wanafunzi

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
Snapchat-2067079470.jpg
HIvi karibuni katika hekaheka za kutafuta mashamba kwa ajili ya msimu ujao wa kilimo nilifika katika kijiji kimoja kinaitwa Mandimu kilichopo Kata ya Mungaa, Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida.

Baada ya kukamilisha mambo yangu nikakaa kijiweni na Vijana wa eneo hilo kujua mbili tatu za eneo hilo.
Katika storI za hapa na pale akapita kijana mmoja ambaye alionekana kumfokea mzee mmoja, nikauliza kulikoni mbona 'dogo' anakosa adabu.

Nikaambiwa bwana huyo ni Mwalimu flani (akamtaja kwa jina la kwanza - Frank) huyo bwana hachezewi hakuna anayemgusa. Ilibid nidadisi zaidi kwani ana ishu gani. Ndipo wakanipa kisanga kizima.

Soma Pia: Mwalimu huyu wa Shule ya Msingi Mungu Maji aangaliwe, ananyanyasa Wanafunzi

WhatsApp Image 2024-10-28 at 05.20.45_664fa42f.jpg
Wakasema tangu Mwalimu Frank afike kijijini hapo kabla ya kuwa Mwalimu Mkuu amekuwa akitandika watoto wetu kinyama sana.

Watoto wanashika nondo juu kwenye dirisha ndio wanachapwa, kutandikwa huko sio kwenye makalio tu. Fimbo zinachapwa mgongoni miguuni hadi kichwani, sio fimbo tu anatumia hadi mateke na ngumi. Vipigo hivi ni wasichana na wavulana.

Nikaelezwa kuwa Watoto wengi wameacha shule kwa kuhofia kipigo cha kinyama cha mwalimu huyo pindi wanapokosea. Baadhi ya Wazazi hawana budi kukubali watoto kubaki nyumbani kwani wanahofia pia wanaweza kuumizwa vibaya kwasababu ilishawahi kutokea mtoto mmoja ambaye angemaliza la saba mwaka huu (2024) alichapwa na Mwalimu huyo baadaye akaanza kulalamika maumivu ya tumbo na wiki moja baadaye alipoteza maisha, so haikujulikana wazi kama chanzo ni mwalimu au alikuwa na changamoto zake nyingine.

Wakazidi kunieleza kuwa kuna Wazazi wawili walikwenda kumhoji kwa nini anawatesa watoto wao nasikia yalitokea mabishano na mama huyo wakashikana na mwalimu kupigana. Mama mwingine yeye aliwashwa kibao hakuthubutu tena kuuliza chochote.

Naiomba Serikali imchukulie hatua mwalimu huyu kwani anawakatili watoto sio kwa kipigo cha kinyama bali pia kukosa haki yao.ya msingi ya kupata.elimu. Pili anawanyanyasa wanakijiji hiko yy amekuwa mungumtu.

Tanzania yetu ni nchi ya Amani mtu mmoja anawezaj3 kunyanyasa watoto na wazazi wao kwnye ardhi yao?

NAOMBA SERIKALI IMSHUGHULIKIE MTU HUYU HARAKA.

Tamko la Serikali ~
DC wa Ikungi: Tunachunguza tuhuma za Mwalimu wa Shule ya Mandimu (Singida) anayedaiwa kudhalilisha Wanafunzi
 
HIvi karibuni katika hekaheka za kutafuta mashamba kwa ajili ya msimu ujao wa kilimo nilifika katika kijiji kimoja kinaitwa Mandimu kilichopo Kata ya Mungaa, Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida.

Baada ya kukamilisha mambo yangu nikakaa kijiweni na Vijana wa eneo hilo kujua mbili tatu za eneo hilo.
Katika storI za hapa na pale akapita kijana mmoja ambaye alionekana kumfokea mzee mmoja, nikauliza kulikoni mbona 'dogo' anakosa adabu.

Nikaambiwa bwana huyo ni Mwalimu flani (akamtaja kwa jina la kwanza - Frank) huyo bwana hachezewi hakuna anayemgusa. Ilibid nidadisi zaidi kwani ana ishu gani. Ndipo wakanipa kisanga kizima.
Wakasema tangu Mwalimu Frank afike kijijini hapo kabla ya kuwa Mwalimu Mkuu amekuwa akitandika watoto wetu kinyama sana.

Watoto wanashika nondo juu kwenye dirisha ndio wanachapwa, kutandikwa huko sio kwenye makalio tu. Fimbo zinachapwa mgongoni miguuni hadi kichwani, sio fimbo tu anatumia hadi mateke na ngumi. Vipigo hivi ni wasichana na wavulana.

Nikaelezwa kuwa Watoto wengi wameacha shule kwa kuhofia kipigo cha kinyama cha mwalimu huyo pindi wanapokosea. Baadhi ya Wazazi hawana budi kukubali watoto kubaki nyumbani kwani wanahofia pia wanaweza kuumizwa vibaya kwasababu ilishawahi kutokea mtoto mmoja ambaye angemaliza la saba mwaka huu (2024) alichapwa na Mwalimu huyo baadaye akaanza kulalamika maumivu ya tumbo na wiki moja baadaye alipoteza maisha, so haikujulikana wazi kama chanzo ni mwalimu au alikuwa na changamoto zake nyingine.

Wakazidi kunieleza kuwa kuna Wazazi wawili walikwenda kumhoji kwa nini anawatesa watoto wao nasikia yalitokea mabishano na mama huyo wakashikana na mwalimu kupigana. Mama mwingine yeye aliwashwa kibao hakuthubutu tena kuuliza chochote.

Naiomba Serikali imchukulie hatua mwalimu huyu kwani anawakatili watoto sio kwa kipigo cha kinyama bali pia kukosa haki yao.ya msingi ya kupata.elimu. Pili anawanyanyasa wanakijiji hiko yy amekuwa mungumtu.

Tanzania yetu ni nchi ya Amani mtu mmoja anawezaj3 kunyanyasa watoto na wazazi wao kwnye ardhi yao?

NAOMBA SERIKALI IMSHUGHULIKIE MTU HUYU HARAKA.
Siamini kama ulimwengu wa leo kuna Mwalimu anaweza kuwa jeuri kiasi hiki na akaendelea na maisha kama kawaida.

Yaani hicho kijiji hakuna hata mwanaume mmoja wa kumshughulikia ipasavyo ili ajifunze kwamba ualimu wake sio chochote kwenye jamii ya watu waliostarabika.

Binafsi hakuna kitu ninachochukizwa kama ukatili dhidi ya mtoto aise suala hilo huwa nalibeba mwenyewe kwenye vyombo vya sheria.

Sheria ya mtoto inamlinda mtoto vizuri sana tena ushahidi wa mtoto hauhitaji uwe mzito bali akithibitisha tu anafanyiwa ukatili basi mtuhumiwa atakumbana na adhabu kali sana.
 
Kama unaweza kupata access ya namba yake ya simu nicheki PM.

Tusiwe watu wa kushughulikia maafa baada ya kutokea bali tuwe watu wa kuzuia maafa.

Huyo anaelekea kuua muda sio mrefu halafu ndiyo nchi nzima ianze kupiga kelele wakati tayari mtoto kapoteza maisha hata huyo mwalimu akinyongwa haitarudisha uhai wa mtoto asiye na hatia.
 
Kuhusu utetezi wa haki za watoto huwa najitolea kufanya kazi hiyo bure kabisa ikiwemo kuwapeleka walimu/wazazi mahakamani maana taaluma yangu inanitaka niwe mstari wa mbele kutetea haki za binadamu wakiwemo watoto.

Nipatie mawasiliano ya huyo Mwalimu Mkuu nitamuonya kwa maneno kama kweli anafanya vitendo hivyo aache mara moja.

Akishupaza shingo basi mwaka huu hautapinduka atakuwa mahakamani anapambana na kesi na cheo chake kitakuwa rehani wakati huo alipambana na kesi.

Jamii kwa pamoja tupinge ukatili dhidi ya mtoto maana mtoto hana nguvu za kujitetea bali watu wazima ndiyo wana dhamana ya kumtetea mtoto.

Kwakweli baadhi ya walimu ni vichaa sema tu bado hawajawa certified Mirembe hospital.
 
Dkt. Gwajima D kazi unayo. Kama haya yanayosemwa yana ukweli KU ya mkoa wa Singida wana kila sababu kufuatilia kwa kina Kifo cha huyo mtoto aliyepoteza maisha kwa hicho kinachodhaniwa kipigo ikiwezekana mwili ufukuliwe vipimo vifanyike. Lakini Mhe kama Waziri mwenye dhamana na Watoto fuatilia mdogo mdogo uwaponye watoto wetu dhidi ya huu ukatili.
 
Kusubiri serikali ichukue hatua ni udhaifu, ndio maana mpaka leo watanzania tumekwama hapo, je hicho kijiji hakina WACHAWI, hao wachawi wanafaida gani sasa.!?

Wamlaze nje mara 2, 3 tu ashike adabu. 😂
Au ticha nae hajalegea, wachawi wamemshindwa, maana mie nawajua wachawi wana nongwa wanatafutaga kasababu kadogo tu.
 
HIvi karibuni katika hekaheka za kutafuta mashamba kwa ajili ya msimu ujao wa kilimo nilifika katika kijiji kimoja kinaitwa Mandimu kilichopo Kata ya Mungaa, Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida.

Baada ya kukamilisha mambo yangu nikakaa kijiweni na Vijana wa eneo hilo kujua mbili tatu za eneo hilo.
Katika storI za hapa na pale akapita kijana mmoja ambaye alionekana kumfokea mzee mmoja, nikauliza kulikoni mbona 'dogo' anakosa adabu.

Nikaambiwa bwana huyo ni Mwalimu flani (akamtaja kwa jina la kwanza - Frank) huyo bwana hachezewi hakuna anayemgusa. Ilibid nidadisi zaidi kwani ana ishu gani. Ndipo wakanipa kisanga kizima.

Soma Pia: Mwalimu huyu wa Shule ya Msingi Mungu Maji aangaliwe, ananyanyasa Wanafunzi
Wakasema tangu Mwalimu Frank afike kijijini hapo kabla ya kuwa Mwalimu Mkuu amekuwa akitandika watoto wetu kinyama sana.

Watoto wanashika nondo juu kwenye dirisha ndio wanachapwa, kutandikwa huko sio kwenye makalio tu. Fimbo zinachapwa mgongoni miguuni hadi kichwani, sio fimbo tu anatumia hadi mateke na ngumi. Vipigo hivi ni wasichana na wavulana.

Nikaelezwa kuwa Watoto wengi wameacha shule kwa kuhofia kipigo cha kinyama cha mwalimu huyo pindi wanapokosea. Baadhi ya Wazazi hawana budi kukubali watoto kubaki nyumbani kwani wanahofia pia wanaweza kuumizwa vibaya kwasababu ilishawahi kutokea mtoto mmoja ambaye angemaliza la saba mwaka huu (2024) alichapwa na Mwalimu huyo baadaye akaanza kulalamika maumivu ya tumbo na wiki moja baadaye alipoteza maisha, so haikujulikana wazi kama chanzo ni mwalimu au alikuwa na changamoto zake nyingine.

Wakazidi kunieleza kuwa kuna Wazazi wawili walikwenda kumhoji kwa nini anawatesa watoto wao nasikia yalitokea mabishano na mama huyo wakashikana na mwalimu kupigana. Mama mwingine yeye aliwashwa kibao hakuthubutu tena kuuliza chochote.

Naiomba Serikali imchukulie hatua mwalimu huyu kwani anawakatili watoto sio kwa kipigo cha kinyama bali pia kukosa haki yao.ya msingi ya kupata.elimu. Pili anawanyanyasa wanakijiji hiko yy amekuwa mungumtu.

Tanzania yetu ni nchi ya Amani mtu mmoja anawezaj3 kunyanyasa watoto na wazazi wao kwnye ardhi yao?

NAOMBA SERIKALI IMSHUGHULIKIE MTU HUYU HARAKA.
Hata wewe ulipigwa acha kuficha ficha, kumbuka mficha uchi hazai.
 
Kuhusu utetezi wa haki za watoto huwa najitolea kufanya kazi hiyo bure kabisa ikiwemo kuwapeleka walimu/wazazi mahakamani maana taaluma yangu inanitaka niwe mstari wa mbele kutetea haki za binadamu wakiwemo watoto.

Nipatie mawasiliano ya huyo Mwalimu Mkuu nitamuonya kwa maneno kama kweli anafanya vitendo hivyo aache mara moja.

Akishupaza shingo basi mwaka huu hautapinduka atakuwa mahakamani anapambana na kesi na cheo chake kitakuwa rehani wakati huo alipambana na kesi.

Jamii kwa pamoja tupinge ukatili dhidi ya mtoto maana mtoto hana nguvu za kujitetea bali watu wazima ndiyo wana dhamana ya kumtetea mtoto.

Kwakweli baadhi ya walimu ni vichaa sema tu bado hawajawa certified Mirembe hospital.
Nikiona mtu anaetetea haki za watoto natamani awe Raisi wa Nchi
 
Kama ni kweli basi namshauri mwalimu huyo aache tabia hiyo.

Zama zimebadilika, kwa sasa watu wanapigana na maisha ili kutimiza ndoto zao.

Ukiona mtoto anafanya yasiyofaa ukamuonya kwa mdomo akaendelea na tabia isiyofaa, achana naye hilo ni jukumu la mzazi wake na ulimwengu.
 
Nikiona mtu anaetetea haki za watoto natamani awe Raisi wa Nchi
Mkuu kwenye utetezi wa haki za watoto huwa sina mzaha kuna walimu kadhaa wa sekondari na msingi wametema bungo baada ya kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria.

Nilipomaliza masomo ya sheria nilianza rasmi kazi hii na huwa natumia gharama zangu za nauli kusafiri kutoka mkoa mmoja hadi mwingine kwa ajili ya kazi hii.

Ndiyo maana nimemwambia mleta mada kama bado yupo hapo kijijini afanye mpango wa mawasiliano ya huyo mwalimu hamnazo nianze kushughulika naye kisheria.
 
Back
Top Bottom