Serikali inaogopa nini kufanya lugha ya kufundishia iwe kingereza kuanzia shule ya msingi hadi chuo kikuu?

Serikali inaogopa nini kufanya lugha ya kufundishia iwe kingereza kuanzia shule ya msingi hadi chuo kikuu?

Umesema private school na sio za serikali ama
Sasa kwani hakuna somo la kiingereza mashuleni?
Mbona kijana wa form 4 hawezi kuongea
Hapo tatizo ni nini wakati wapo waalimu wa masomo.hayo
Hakutaka kujibidiisha. Ukienda shule za kanisa (RC) kama mtoto hajitumi Wana kwambia mzazi mtafutie shule nyingine. Sijajua shule za dini nyingine na shule za serikali
 
Tuma walimu ambao ni akina mwanasesele na mwanambilimbi kiingereza sifuri unaanzaje, labda waalike experts from foreign neighbouring countries
 
Bado nashindwa kuelewa kwanini serikali bado inapata kigugumizi kuamua tuu kingereza kiwe lugha ya kufundishia kuanzia shule ya msingi hadi chuo kikuu ili kuendana na teknolojia na ulimwengu. Je nini kinawakwamisha

1. Walimu hawana uwezo?

2. Wanalinda biashara ya shule za mabasi ya njano kukosa wateja?

3. Wanaogopa kiswahili kitapotea?

Au ni nini hasa?

Mwanafunzi anamaliza kidato cha nne hata kuomba maji kwa kingereza haju.
Wenye teknolojia woooote huko duniani, mashule yao hufundisha kwa lugha za kwao, lugha inayotakiwa kufundishia hapa Tz ni kiswahili .
 
Umeshawahi kusikia Inglishi ya wale vipanga wa hisabati na fizikia? Unaweza kucheka hadi upasuke.

Lakini shughuli yao kwenye masomo si ya kitoto. Same applies kwenye masomo mengine.

Lugha is very important, but should never be overrated.
Ushasema ni vipanga. Lugha ndio inayotumika kufundishia hivyo huwezi kuichukulia poa namna hiyo. Matokeo yake tunakuwa na vipanga waliokariri vitu ambavyo hawavielewi.
 
Hakutaka kujibidiisha. Ukienda shule za kanisa (RC) kama mtoto hajitumi Wana kwambia mzazi mtafutie shule nyingine. Sijajua shule za dini nyingine na shule za serikali
Sasa kwanini wasimsaidie mpaka aelewe badala ya kumvunja moyo mzazi
Kuna watoto wasioelewa Autistic ila kama yuko sawa mbona anafundishwa vizuri tu
Au wanataka the finest
 
Bado nashindwa kuelewa kwanini serikali bado inapata kigugumizi kuamua tuu kingereza kiwe lugha ya kufundishia kuanzia shule ya msingi hadi chuo kikuu ili kuendana na teknolojia na ulimwengu. Je nini kinawakwamisha

1. Walimu hawana uwezo?

2. Wanalinda biashara ya shule za mabasi ya njano kukosa wateja?

3. Wanaogopa kiswahili kitapotea?

Au ni nini hasa?

Mwanafunzi anamaliza kidato cha nne hata kuomba maji kwa kingereza haju.
Watakubaliaje kiinglish wakati wenyewe hakipandi mwanangu? Watakubalije wakati wakishasomesha watoto wao kiinglish wanakitumia kunyonyea wengine?
Watatumiaje kiinglish wakati wanataka kuzalisha wajinga wengi ambao ni rahisi kuwaibia na kuwatawala kama ilivyo?
Kiinglish chanini wakati kitawawezesha wabongo kujua mambo wasiyopaswa kujua na kuasi?
Napendekeza tutumie kimakonde mashuleni lau tujue kitu.
 
Mkuu, kiuhalisia kabisa bila ushabiki kiswahili hakitupeleki popote. Nchi yetu bado ni tegemezi, tunategemea kutumia tafiti zote za kiteknolojia, kisayansi nk. zilizofanyika na nchi nyingine. Sisi bado wachanga mmno ktk dunia hii hatujielewi. Ukitofautisha na nchi nyingine zilizojiwekeza kwenye tafiti za sayansi na technologies. Wanasema kiswahili kitumike kufundishia watoto wao wanasoma mitaala ya kingereza kalaga baho
.Fact.
 
Ndiyo maana kwenye mikataba nchi yetu inapigwa! Wanasheria wetu hawajui Kiingereza!
Kupigwa sio kutokujua kingereza, shida ni rushwa na umimi ndio maana tunapigwa mikataba mibovu.
JPM tulikua tukimsema hajui kingereza lakini haikutaka mikataba mibovu kwake na hata iliyokua imeingiwa baadhi alianza kuivunja.
Kwahiyo ishu sio kingeresa
 
Kila taasisi na taratibu zake

Leo feza ukiwa top 3 au 10 kitaifa katika mitihani ya kitaifa ya kidato cha pili, nne

vile vile mitihani ya darasa la nne na la saba wanakupa ufadhili wa kusoma bure shuleni kwao kama sikosei

NB
ilikuwa ni muda kidogo kipindi cha top top za kitaifa, sasa hivi hawatangazi tena hayo ma top top

kwanin wachukue top kwanini wasitengeneze top??

kila taasisi na taratibu zake, ukiwauliza watakujibu vizuri

Sasa kwanini wasimsaidie mpaka aelewe badala ya kumvunja moyo mzazi
Kuna watoto wasioelewa Autistic ila kama yuko sawa mbona anafundishwa vizuri tu
Au wanataka the finest
 
Hata huko vyuoni msipoelewa Lecturer anabidi amwage kisakwinga kingi sana.

Lugha muhimu ni kichina ikiwa Taifa litaangalia miaka 50 au 100 ijayo.

Nje ya hapo, mkazo uongezwe kwenye kiswahili kwa ngazi zote na kiingereza kibakie somo tu.
 
Ajira za lugha ya kiswahili zinahitajika sehemu mbalimbali duniani

Leo wazungu wanajifunza kiswahili wakiwa kwao, wanakuja huku wakiwa wanafahamu angalau kidogo na zaidi

Balozi zetu zinafanya vizuri mfano ubalozi wa Tanzania Korea kusini, taasisi binafsi na vyuo kadhaa vina toa elimu ya lugha ya kiswahili huko ulaya na marekani (ujerumani, uingereza, marekani nk)

Hivyo kiswahili kina songa mbele kwa mwenye kukithamini, wapo ambao kingereza cha nini na wapo ambao wanakithamini kama unavyofanya
 
Jambo hilo lilishafanyiwa utafiti matokeo yakaonekana haiwezekani . Sasa sijui wewe unalenga nini mdau
 
Hata huko vyuoni msipoelewa Lecturer anabidi amwage kisakwinga kingi sana.

Lugha muhimu ni kichina ikiwa Taifa litaangalia miaka 50 au 100 ijayo.

Nje ya hapo, mkazo uongezwe kwenye kiswahili kwa ngazi zote na kiingereza kibakie somo tu.
Bado una uhuru wa kujifunza lugha zaidi ya moja

Kihindi, Kichina, kifaransa, Spanish, kireno na hata kiarabu. Sio Vibaya kujifunza lugha zaidi na lugha ikumbukwe ni kwa ajili ya kurahisisha mawasiliano

Unaweza kwenda sehemu ukajikita unatakiwa uanze kujinoa na lugha mpya. Mfano unaenda SA ukijua utapiga kizungu tu lakini utaongeza kishona au kizulu nk

Utaenda ulaya (sweden) utajikuta unajifunza kiswedesh, maisha yatakufundisha vitu vingi kama utaruhusu kufanya hivyo
 
Bado nashindwa kuelewa kwanini serikali bado inapata kigugumizi kuamua tuu kingereza kiwe lugha ya kufundishia kuanzia shule ya msingi hadi chuo kikuu ili kuendana na teknolojia na ulimwengu. Je nini kinawakwamisha

1. Walimu hawana uwezo?

2. Wanalinda biashara ya shule za mabasi ya njano kukosa wateja?

3. Wanaogopa kiswahili kitapotea?

Au ni nini hasa?

Mwanafunzi anamaliza kidato cha nne hata kuomba maji kwa kingereza haju.
Wanataka tofauti ya watoto wa kishua na wa Uswazi iwe dhahiri, kwenye nafasi za kazi hasa za mashirika ya kimataifa na opportunities za kazi nje ya nchi.
 
Tatizo la elimu yetu siyo lugha ya Kiswahili wala Kiingereza. Shida kubwa iko hasa kwenye miundombinu, vifaa/nyenzo za kufundishia na walimu mahiri na mazingira bora na wezeshi kwa walimu na wanafunzi.
Lugha ni tatizo kubwa sana
 
Watakubaliaje kiinglish wakati wenyewe hakipandi mwanangu? Watakubalije wakati wakishasomesha watoto wao kiinglish wanakitumia kunyonyea wengine?
Watatumiaje kiinglish wakati wanataka kuzalisha wajinga wengi ambao ni rahisi kuwaibia na kuwatawala kama ilivyo?
Kiinglish chanini wakati kitawawezesha wabongo kujua mambo wasiyopaswa kujua na kuasi?
Napendekeza tutumie kimakonde mashuleni lau tujue kitu.
Inasikitisha sana
 
Hakuna kitu kama hicho, mkuu. UN Kiswahili kinaheshimika, sasa je?

Nini kinachokosekana au kushindikana kufundishia kwa Kiswahili? Mbona hadi vyuoni maprofesa na wahadhiri wanakiswang'anya Kiingereza huku wakitumia Kiswahili kama kawaida?

Jambo la msingi, maandalizi muhimu yafanyike halafu utajionea mwenyewe. Tena Kiswahili kinaweza kuwa bora kabisa hata kuliko Inglishi.

Miaka zaidi ya 100 ya matumizi rasmi ya Kiswahili, halafu bado watu wanadai eti ni lugha changa?
ACHA UJINGA

hutaki wenzio nao wajue kiingereza et eee,PIMBI
 
Bado nashindwa kuelewa kwanini serikali bado inapata kigugumizi kuamua tuu kingereza kiwe lugha ya kufundishia kuanzia shule ya msingi hadi chuo kikuu ili kuendana na teknolojia na ulimwengu. Je nini kinawakwamisha

1. Walimu hawana uwezo?

2. Wanalinda biashara ya shule za mabasi ya njano kukosa wateja?

3. Wanaogopa kiswahili kitapotea?

Au ni nini hasa?

Mwanafunzi anamaliza kidato cha nne hata kuomba maji kwa kingereza haju.
Kwa hiyo wakitumia kiingereza ndo watoto watakuwa na uelewa mkubwa?...
Kiingereza ni lugha tu mkuu mataifa yaliyoendelea yoote yanatumia lugha zao kufundishia acheni kushobokea lugha za watu! Kiingereza ukitaka kukijua unakijuq tu hata kama hujaenda shule hakihusiani na akili wala maarifa
 
Back
Top Bottom