Serikali inaogopa nini kufanya lugha ya kufundishia iwe kingereza kuanzia shule ya msingi hadi chuo kikuu?

Umenena vizuri. Na itakuwa rahisi kujifunza Kiingereza kama somo la lugha na si vinginevyo.
Fikiria kuna msomi na PhD yake aliamua tuu watoto wakianza kidato cha kwanza wafundishwe kozi ya kingereza wiki 6 wame wameshakua mahiri kuanza kusoma masomo kwa kingereza[emoji28][emoji28][emoji28].

Wiki 6 kweli ??

Kwanini wasianzie tangu chekechea
 
Ghana, Nigeria, Zambia nk kingereza kimewasaidia nini ?
Ukionesha kwa data basi ntaishauri serikali ibadili mara moja.
Usisahau kueleza wahitimu wa english medium zaidi ya miaka 20 sasa. Je wameeelimika na wameleta tofauti gani kwe ye nchi kuanzia ubunifu,sanaa, michezo, teknolojia, ofisini kwenye jamii na kimataifa.
Ukishindwa basi futa uzi.
 
Sasa kwavile unahisi hakijawasaidia Ghana ndio tukiache wakijue tuu watoto wa kina madelu
 
Sasa kwavile unahisi hakijawasaidia Ghana ndio tukiache wakijue tuu watoto wa kina madelu
Wewe unaekijua kimekusaidia nin ? Mkinga wa makete anapouza misitu yake anauza kwa kingereza ? Muha wa kigoma anapouza sabuni za mawese anauza kwa kingereza ?
Msukuma anapouza pamba., ng'ombe minadani anauza kwa kingereza ?
Kwa nini unataka kakundi kadogo ka watu wa maofisini kawe kigezo kwa watu milioni 55.
Watu milioni 55+ Tanzania hawahitaji ki gereza kwa lolote. Watu milioni 1 wafanye wajuavyo kujifunza hicho kingereza haiitaji vijiji vya njombe ndani walazamishwe kuongea kingereza wakati kiswahili tu wanakiongea shuleni. Kuundoa ukoloni wa kifikra ni vita ngumu sana japo inafanikiwa taratibu sana
Ukielimika huta abudu kingereza na uzungu. Kwanza sasa dunia inaelekea uchina, je tubadili mitaala iwe ya kichina ?
 
Wachina wenyewe wanajifunza kingereza
Tunahitaji kuongeza wigo zaidi ya hapa
 
Mtaala mbovu ni mbinu ya kutawala
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…