Serikali inapambana na Wamasai kutoka Arusha kwenda pwani na Morogoro; hakuna kabila linalopitia magumu haya

Ujinga ni mzigo,soma mada ya mwandishi, usikurupuke kuandika tu pumba bira hata kuelewa kilichoandikwa.
Sasa nisingesoma ninge comment? Wamasai hata wakiingia Mbeya watakwambia wamekuwepo pale tangu mwaka 1920.

Kama wewe kila kitu unachokijua ni hicho kilichoandikwa na Mwandishi, basi jua kwamba wengine tunajua zaidi ya hapo na kabla ya hiyo habari.
 
Tuseme ukweli hapa, bila kuwadhibiti Wamasai migogoro ya wakulima na wafugaji haitokwisha. Hii tabia yao ya kutangatanga na mifugo muda wote inafanya waonekane ni watu hatari Kwa mustakabali wa kilimo.
 
Niliwahi kulima mpunga ifakara Kuna Kijiji kinaitwa Signali.Nililima heka 40. Basi bana nikaondoka kuja dar kama wiki mbili hivi, Ile kurudi nkakuta Masai wameingiza shambani Ng'ombe wamekula kama heka 15,yaani wamefyeka kabisa zinaonekana kwato zao tu walipokuwa wanapita.
 
Hao jamaa hawawezi hata kutofautisha kati ya mimea ya mahindi na nyasi zingine unadhani akili zinawatosha.

Miaka ya nyuma ilikuwa huwezi kuona masai wilaya ya Meatu na Bariadi, walikuwa wamepigwa "Fatwa" sababu ya wizi wa mifugo.
 
Kwani wamasai wenyewe wanasemaje? Sijamuina maasai wa kweli akilalamika zaidi ya wanaharakati
 
Ila wamasai wanaonewa sana hilo jambo la Ngorongoro Tu ni kubwa kuzidi hata DPWorld lakini halikupewa airtime hakuna mtu wala taasisi ya kuwaongelea wanaonekana kama wanyama tu wa porini
 
Hivi jamii ya Kimaasai kwa upande wa kule Kenya inapitia madhila kama haya ya ndugu zao kwa upande wa Tanganyika? Wazee wa Pwani hawana huruma yoyote ile kwa wazee wenzao kutoka jamii hii.

Tamaa ya fedha kwa wawekezaji wa kigeni, kwa hila na kificho cha utunzaji hifadhi ndiyo hasa kosa ambalo linawagharimu kupitia watawala hawa. Maeneo yao ya asili yanatwaliwa kwa nguvu mbele ya macho yao, ndito zao, na watoto wao.

Shujaa kama Moringe Sokoine yupo wapi hii leo ili kupinga dhuluma hii ya wazi kwa jamii hii!? Ni lazima watambua kuwa haki haitolewi kama hisani, bali hutafutwa kwa machozi, jasho na damu.

Wakati umefikia wa wao kujitetea wenyewe nje ya wanasiasa. Morani hupambana na simba bila woga wowote ule, sembuse iwe binadamu?
 
Naona ni mikakati tu ya kuwauzia wawekezaji sehemu zote wanapoishi
Sina kipangimizi kama uuzwaji huo una tija na maisha yao pia ila kama kuwajengea nyumba sehemu ambazo ni kupya kabisa na hiyo ndio imetoka
Basi huo ni wizi na utapeli na uonezi kwa serikali yetu

Kama wanakula hela mabilioni kwa hao wawekezaji wajue ipo siku watadaiwa zaidi na hawatakuwa na cha kuwapa
Dunia inabadilika na sidhani hao wanaolindwa kuchukua ardhi yote hiyo kama wataishi sana

Kama tuna faida nao kwa mfano wanajenga mahoteli makubwa na kuchimba labda mabwawa makubwa kwa ajili ya wanyama waje karibu na mahoteli kama Kruger National Park na serikali inachukua kodi za uhakika kwa manufaa ya wananchi sawa
Ila kama ni majizi yale yale hapo kuna shida
 
Hamna masai mwenye akili ukiwemo wewe mleta mada.
 
Wafugaji wengi wanamiliki mifugo mingi ila kuwalisha mtihani

Ova
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…