Serikali inayobadilisha maamuzi yake kwa kutegemea upepo ni Serikali dhaifu, haifai

Serikali inayobadilisha maamuzi yake kwa kutegemea upepo ni Serikali dhaifu, haifai

zimmerman

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2011
Posts
1,644
Reaction score
3,176
Nimeshangazwa na hili hapa kama ni kweli: Mwigulu: Tumesikia malalamiko ya Watanzania kuhusu tozo za miamala na Rais ametoa maelekezo ya kuzitazama upya

Hivi inawezekanaje serikali (hapa serikali kwa maana ya watendaji wakuu wa serikali, mawaziri wakiwemo na vyombo vyao vinavyowasaidia katika maamuzi ya kisera) kuamua kitu na baadaye ikifikirie upya baada ya kusikilizia mwitikio wa watu?

Hebu imagine, hivi serikali ya aina hiyo itawezaje kweli kufikia malengo yake? Maana serikali ya aina hiyo itakuwa inaamua hili halafu sisi raia tukipiga kelele inaacha kulitekeleza.

Hii ni dalili kubwa kabisa kwamba tunaongozwa na watu dhaifu sijapata kuona. Hata JK hakuwa dhaifu hivi. Tulimpigia kelele kweli JK kuhusu safari zake but the man believed he was doing the right thing kwa masafari yake yasiyoisha. Na huyu mzee alisafiri hadi sekunde ya mwisho. Kiongozi wa aina yoyote ile anayestahili kuwa kiongozi lazima aamini katika maamuzi yake na kuyatetea ipasavyo.

Hivi mama ameshindwa kusimama na kujenga hoja ya kutushawishi watanzania kwa nini miamala ya simu ni muhimu kwa wakati huu?

Ameshindwa kusimama na kusema, kwa mfano, kwamba nchi yetu imehama kutoka kwenye uchumi wa kutegemea mataifa mengine, na ya kwambaa kuitwa nchi ya uchumi wa kati maana yake ni kwamba ni lazima kama wananchi tujitegemee kwa asilimia kubwa?

Ameshindwa kutetea ongezeko la kodi zake kwa kuutangazia umma wa watanzania kwamba miradi ya kimikakati iliyoachwa na JPM ni ya muhimu sana na ni lazima ikamilike kwa wakati, lakini zinahitaji pesa nyingi?

Ameshindwa kujenga hoja kwamba kwa mfumo wa zamani wa kukusanya kodi pesa ya kuendesha serikali na kutimiza miradi hiyo ya kimikakati ilitegemea kuwakamua watu wachache pesa nyingi, mfumo ambao haukuwa endeleve na ulileta malalamiko mengi na kukwamisha ukuaji wa sekta binafsi?

Ameshindwa kutushawishi watanzania kwamba ni kawaida kwa jambo jipya kama hilo la kukusanya kodi kwa njia ya miamala ni lazima lipokewe kwa mshtuko na watu na hilo linaeleweka, lakini uwaombe watu hao wawe na uvumilivu maana pesa yao inakwenda kufnaya mambo makubwa yatakoyogeuza sura ya nchi yao na kuwafanya wajivunie kuitwa watanzania?

Hakuna sababu ya kutikiswa iwapo unachokifanya unaamini ni sahihi. Sasa utafanya kitu gani ambacho hatutakupigia kelele -- baadhi yetu.

Aisee!
 
Mkuu huna ozoefu na mambo ya serikali. Kuna serikali ziliondolewa katika uongozi kwa kukataa kushusha bei ya mkate tu, sembuse tozo!
Tulipompigia kelele JK kuhusu safari zake hadi tukamwita Vasco da Gama, serikali yake iliondolewa?

Mlipompigia kelele JPM kuhusu kile mlichokuwa mnakiita udkiteta serikali yake iliondolewa?

Ni kawaida ya raia kutoridhika, uongozi ni kujenga hoja na kuwashawishi watu kwamba maamuzi yako ni sahihi.

Urais ni mgumu, na usipokuwa na uthabiti wa maamuzi hiyo kazi haikufai.
 
Tulipompigia kelele JK kuhusu safari zake hadi tukamwita Vasco da Gama, serikali yake iliondolewa?
Mlipompigia kelele JPM kuhusu kile mlichokuwa mnakiita udkiteta serikali yake iliondolewa?

Ni kawaida ya raia kutoridhika, uongozi ni kujenga hoja na kuwashawishi watu kwamba maamuzi yako ni sahihi.

Urais ni mgumu, na usipokuwa na uthabiti wa maamuzi hiyo kazi haikufai.
Inaweza isiondolewe, lakini ikapoteza viti vingi vya ubunge. Hilo nalo ni tatizo
 
'Hata JK hakuwa dhaifu hivi. Tulimpigia kelele kweli JK kuhusu safari zake but the man believed he was doing the right thing kwa masafari yake yasiyoisha. Na huyu mzee alisafiri hadi sekunde ya mwisho. Kiongozi wa aina yoyote ile anayestahili kuwa kiongozi lazima aamini katika maamuzi yake na kuyatetea ipasavyo.'.

Hivi sio JK aliyepigiwa kelele khs Kodi za laini ya Simu kila mwezi akawa mpole?
 
Inaweza isiondolewe, lakini ikapoteza viti vingi vya ubunge. Hilo nalo ni tatizo
Hapo ndipo ninapowakubali wanasiasa wasiofikiri in terms ya kupata au kukosa kura. Na ukweli wa mambo serikali hukubalika kwa sababu ya uimara wake katika kutekeleza yaliyomo kwenye ilani yake ya uchaguzi.
 
Leo Mwigulu ITV DK 45
Alichoongea siku 4
Natamko la Leo,otherwise ITV wasirushe.
Hapo ndipo utakapojua uwezo mdogo wakuchambua mambo.
Atawaamuru wasirushe hayo majadiliano. ITV itabidi warushe vipindi vya nyuma. Huyu jamaa kaaibika kuliko watu wanavyofikiria.
 
Tatizo sio udhaifu wa kiuongonzi tatizo ni maamuzi ya kukurupuka yasiyoegemea kwenye maridhiano na tafiti ili kupata matokeo. Maamuzi ya mwingulu na ndungulile yaliengemea kwenye mawazo ya zungu, tarimba, shabiby nk ambao wameingia bungeni kulinda maslahi yao ya kibiashara na binafsi sio ya wananchi walio wengi ukizingatia watanzania wengi ni makabwela sio wafanya biashara
 
Chadema 2010 ilipata viti vingi vya ubunge bungeni, kwasbb ya udhaifu wa mkwele katika hoja ya ufisadi, Richmond, IPTL, mwisho wa siku wananchi wakapatwa na hasira na kuihamini Chadema.

Kwa hiyo hata hoja hii ya Tozo na inaweza mende akaangusha kabati.
 
Serikali isiyosikiliza wananchi wake ndio udhaifu wenyewe...

Huo ubabe eti ili uonekane una msimamo hivyo uendelee kwenda tofauti na wananchi ni upuuzi...

Wabunge waliopitisha Sheria ni wawakilishi wa wananchi sasa kama Sheria hiyo inawaliza wananchi wengi hao wabunge wanamwakilisha nani

Kutenda Kosa sio Kosa..., Ila kuendelea kufanya Makosa ili tu uonekane una Msimamo ni Ujuha....
 
Serikali ya JPM ilichukiwa na kupigwa zengwe kwa misimamo ya hayati. Ni pale aliposimama Ubungo na kuuambia umma kwamba hawezi kumfukuza kazi Makonda kwa kutegemea presha za mitandaoni.

Rais Samia amevaa sura ya kibinadamu na huo sio udhaifu bali ni hulka ya kistaarabu aliyonayo, anaweza kabisa kuamua kuwa mnyama na asiguswe na mtu yoyote kama ambavyo JPM alivyoamua kuendesha nchi kibabe.

Kuelezea nini serikali yake inasimamia pia ni kazi ya mawaziri wake na makatibu wakuu, demokrasia inawaruhusu kufanya hivyo na madaraka waliyonayo yanawaruhusu kufanya hivyo.

Pia Rais kusikiliza sauti nyingi za watu ni sifa ya ubinadamu, ni sifa ya uongozi. Kwani sauti ya wengi ni sauti ya Mungu hivyo hekima ya kweli ni kusikiliza kilio cha wengi.

Katiba yetu ndio imetupatia Rais huyu hivyo tujenge hoja zetu tukitambua juu ya ukweli huo.
 
Back
Top Bottom