Serikali inayobadilisha maamuzi yake kwa kutegemea upepo ni Serikali dhaifu, haifai

Haifai kabisa huu ni udhaifu uliopitiliza,watu tulilopa kodi ya kichwa kwa jasho na damu,tulipigania uhuru kwa jasho na damu afu eti Serikali inaacha kutoka nje kuwaeleza watu kwa nini tozo imeongezeka ,inataka ifanye nini inakuja kusalimu amri kwa ujinga?

Kodi yenyewe ni sio lazima ni unaamua mwenyewe.Rais kanikera Sana bila shaka hata Watendaji wake wamemshangaa.

Kuna mtu wa kutuletea maendeleo nchi hii? Na wapiga. Makelele ndio walikuwa wanashangilia watu kuporwa pesa na kutumbuliwa.

Mwendazake sijawahi mkubali ila kusimamia anachokiamini alikuwa vizuri,miradi mikubwa itaishaje? Changamoto lukuki zitapunguzwaje? Udhaifu Sana huu na kutojiamini.
 
Nakuunga mkono mtoa mada hii nchi imejaa watu wavivu, walalamishi wasio na majibu afu hawataki kuwajibika.

Tangu lini mwananchi akaenda kununua au kuuza akatoa risiti kama sheria inavyotaka Ili serikali ipate mapato ya kugharamia maendeleo na kujiendesha?

Sasa tozo kama hizi zilikuwa zina offset hapo kwenye Ukwepaji kodi eti Serikali inaenda kusalimu amri,pengo la bajeti litakalojitokeza watatoa wapi pesa? Kukopa kwenye masharti ya kibiashara yanayoumiza zaidi? Hivi watu wanajua kwamba Serikali inatumia karibu Tilioni 10 kulipa madeni yaliyoiva
 
waturudishie na makato adi sasa washa chukuwa makato makubwa
 
Huna haya viongoz wasikivu kwa Raia ndo strong learder with empathy characteristics ambayo ni muhimu kiuongozi, wewe mshamba unafikiria kiongozi mzuri ni yule anayeumiza na kutokusikiliza Raia anaowaongoza. In short wewe ni mwovu huna huruma na watanzania go to hell
 
Mkuu huna uzoefu na mambo ya serikali. Kuna serikali ziliondolewa katika uongozi kwa kukataa kushusha bei ya mkate tu, sembuse tozo!
Hajui huyu na madhara yake kiuchumi ya hyo tozo, vipi transcations za makampuni ya simu ka yameshuka, mawakala kukosa ajira na serikali kukosa kabisa hyo kodi
 

Nadhani unapotosha watu, na unaipotosha hiyo serikali. Watu hawajakataa hiyo tozo au kodi - vyovyote vile itakavyoitwa. Ila watu wamelalamikia kiwango. Tatizo ni viwango vilivyowekwa, sio tozo au kodi. Nadhani kama ingekuwa imewekwa labda 10% au 20% kutoka zile gharama za kampuni ya simu, isingekuwa shida sana. Sasa kuwekwa 150% au 200% ya ile gharama ya muamala ya kampuni ya simu, ndio imekuwa tatizo...
 
Wewe mchawi kweli hzo tozi zilikuwa ghali Mimi binafsi nisharudi kutumia bank tu siwezi kupata hasara kwa Kodi za wizi hivo
 
Mama Samia, if you had arrive at a decision on taxes of telephony transactions with considered reasons, you are not suppose to change.

For you to change the decision now you are showing us your total and complete weakness.

A leader must be firm when you arrive at a considered decisions. We don't want weakling leaders anymore on issues of countries importance. VACATE OFFICE.
 
Katibu mwenezi wa CCM kata unajiona unajua meeengi!!
 
Uwezo mdogo wa kutunga sera wamezoea kutunga sera ambazo hazina muelekeo 'uncertainty policy' or regime uncertainty
 
Wewe mchawi kweli hzo tozi zilikuwa ghali Mimi binafsi nisharudi kutumia bank tu siwezi kupata hasara kwa Kodi za wizi hivo
Kwani ukitumia benki kuna shida gani? Cha msingi lazima serikali iwe na msimamo,upuuzi kama huu ndio unatufanya miaka 60 ya uhuru shule zinahangaika na vyoo, watoto wanarundikana hovyo madarasani afu Hali ya maisha Vijijini inazidi kuwa mbaya huku nyie wa mjini mnadwmka tuu eti tozo kubwa .
 

Kwa tozo wamekurupuka , walalahoi ndio wanatumia sana miamala ya simu maana transaction za bank zimewaweka mbali ,sasa ukiwaongezea tozo tena kubwa hakika wanakimbia ,kilichotokea kuanzia walivyo implement changes miamala imeshuka kwa kiwango cha lami inabidi wabadili gear angani kuokoa uchumi.
 
Serikali kama ni ya watu itawasikiliza raia wake wanasema nini , sisi wananchi ndio tumewaajiri wao. Wewe utamvimbia mtu anayekupatia chakula mezani. Sisi wananchi tuna nguvu kubwa sana -ila hatujiamini. Tunasahau kwamba kupitia uchaguzi ni sisi tunaowapata kazi hao unawaita serikali. Serikali makini lazima si hiari - kusikiliza kilio cha wananchi. Serikali ilitumia wataalamu kubuni huo mkakati- je wataalamu waliangalia kwa kina viashiria vyote , inawezekana kuna kosa kwenye hiyo "model" yao.
 
Hayo ndiyo madhara ya kuwa na wabunge vibogoyo na wachumia tumbo yaani walipotishwa tu na Ndungai kuwa wasipopitisha bajeti basi mama atavunja bunge wakapiga kura ya ndiyo bila kujua madhara yake
 
Serikali ya kidemokrasia ni serikali ya watu kwa ajili ya watu na kwa faida ya watu.

Serikali isiyosikia VILIO vya watu ni serikali ya kiimla.

Labda serikali ingeweka time frame katika makato ya miamala hapo kidogo tungewaelewa lakini sio Wizi wa kimachomacho namna hiyo au wao walipobuni hiyo miradi yao mikubwa hawakujua pesa watatoa wapi??, kabla hawajabuni hiyo miradi walishauri wananchi kwamba pesa za hiyo miradi zingetoka kwenye miamala ya simu??, kulikuwa na mapatano au referundum juu ya suala hilo??--- katika miamala ya fedha mtu hukatwa pesa ya huduma ya muamala tu (transaction service charge), sasa hizo kodi zingine zinaingiaje hapo kama sio wizi wa kimachomacho??!!.-----A failed state is the one which use tricks to snatch forcibly her citizens unwillingly the little they have in pretext of development. Hatuwezi kujenga nchi kwa pesa za WIZI.

Tusipokataa jambo hili ipo siku hata michango ya misiba itatakiwa itozwe kodi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…