Serikali ipige marufuku biashara ya minofu ya samaki kwenda Ulaya

Serikali ipige marufuku biashara ya minofu ya samaki kwenda Ulaya

Nyumisi

JF-Expert Member
Joined
Nov 10, 2010
Posts
13,499
Reaction score
19,292
Hivi karibuni hii biashara ya kusafirisha minofu kutoka kanda ya ziwa kwa kutumia mashirika kama Rwanda Air na leo tena nimesikia Ethiopian airways imerudi kwa kasi na kimekuwa kama kitu cha kujivunia hadi waziri anaenda kushuhudia.

Wengi humu tunajua watoto wetu wamedumaa kwa zaidi ya asilimia 35 na tunaelewa samaki wana protini nyingi na madini muhimu kwa ajili ya mama wajawazito na ukuaji wa ubongo wa watoto.

Kwa nini kama watu wameona soko la minofu Ulaya wasifuge hao samaki kibiashara kwenye mabwawa kuliko kushindania hawa samaki wachache wanaovuliwa kwenye maziwa na mito yetu?

Yaani wananchi wetu washindane na wanunuaji wa Ulaya, kweli? naamini Rais ataliona hili kwa manufaa mapana ya vizazi vya watanzania.
 
kama kweli tunawajali wanyonge hizo samaki ziende masoko ya watanzania zikauzwe bei ndogo
hivi lile agizo la kuwauzia nyama ya kifimbo watanzania lilitekelezwa ?
 
Kuna furu, dagaa, nembe, gogogo, ngerengere, changu n.k, hawa wanatutosha!
una uhakika gogogo na hao samaki wengine wapo masoko yote Tanzania ? mimi nimeishi zaidi ya mikoa 5 wananchi wengi wanaoenda sokoni huenda kununua mboga za majani na dagaa tu,na hata wachache wanaonunua nyama na samaki hulia bei ni kubwa
 
Hiyo minofu yenyewe ni ya samaki aina ya sangara pekee walioletwa Ziwa Victoria na haohao mabeberu ndio inasafirishwa.

Mnadumaa kwa umasikini tu lakini si uhaba wa samaki kwa maana kuna aina kibao tu ambazo haziendi popote na hazina hata ushindani sokoni.
 
Wengi humu tunajua watoto wetu wamedumaa kwa zaidi ya asilimia 35 na tunaelewa samaki wana protini nyingi na madini muhimu kwa ajili ya mama wajawazito na ukuaji wa ubongo wa watoto.
Tanzania makabila mangapi hula Samaki hadi samaki iwe issue? Masai huwa Hali samaki ulishawahi muona mtoto wa kimasai mwenye utapiamlo? Mleta maada una agenda ya kishetani tu kuua uchumi waua uchumi Kama nyie ndio mnataka mpewe nchi Mungu hawezi kubali atatupa hata nguvu ya kuwaibia kura

wewe ni economic hitman shetani wewe
 
Tanzania makabila magapi hula Samaki hadi samaki iwe issue? Masai huwa Hali samaki ulishawahi muona mtoto wa kimasai mwenye utapiamlo? Mleta maada u a agenda ya kishetani tu kuua uchumi waua uchumi Kama nyie ndio mnataka mpewe nchi Mungu hawezi kubali atatupa hata nguvu ya kuwaibia kura

wewe ni economic hitman shetani wewe
Angalia hii documentary afu njoo na upupu wako hapa


 
Napinga kuwauzia mabeberu minofu ya samaki wetu.
 
Hivi unajua samaki wanaovuliwa ziwa victoria ni 20% tuu ya samaki waliomo kwenye ziwa

Unafahamu samaki wanaovuliwa ziwa Tanganyika ni 8% tuu ya samaki waliomo kwenye ziwa

Na unafaham samaki wanaovuliwa kwenye Pwani zetu za bahari ya Hindi ni 0.8% ya samaki waliopo eneo hilo

Kwahiyo mtoa mada pambania serikal ifanye uwekezaji mkubwa kwenye maeneo hayo ili samaki hao wato angalau tuvune samaki 60% ya waliopo kwenye maeneo hayo nauhakika tutalisha samaki dunia nzima

Fanya utafiti kabla ya kuweka bango.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi unahabari kuwa sangara alipandikizwa ziwa Victoria na wakazi wengi wa eneo hilo hawampendi?
 
Back
Top Bottom