Serikali ipige marufuku utazamaji wa tamthlia hapa nchini

Serikali ipige marufuku utazamaji wa tamthlia hapa nchini

tpaul

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2008
Posts
24,225
Reaction score
22,632
Inasikitisha sana mtoto wa darasa la saba kutofahamu historia ya nchi yake. Juzi nilimsikia kiongozi mmoja wa serikali akiwahoji baadhi ya wanafunzi maswali mepesi kabisa lakini wakashindwa kujibu. Ni aibu kubwa sana mwanafunzi wa darasa la saba anayetarajia kufanya mtihani wa kitaifa miezi 8 ijayo kuulizwa ataje matunda ya muungano anataja maembe, maparachichi, machenza na machungwa!

Nimekuwa nikifuatilia malezi ya watoto hapa mjini kwa muda mrefu; nimegundua watoto wanatumia muda mwingi kutazama tamthlia za kichina, kihindi na kifilipino wawapo nyumbani na kwenye mabanda ya kutazamia video. Hata inapofika saa 2 jioni badala ya kutyuni taarifa ya habari, wazazi hubadilisha chaneli na kuanza kutazama sinema.

Matokeo yake watoto wanashindwa kujibu maswali rahisi kama vile kutaja majina ya viongozi wakubwa nchini wakimwemo Waziri Mkuu, Rais wa Zanzibar na Waziri Mkuu. Hili ni tatizo kubwa. Yaani nchi hii tunakoelekea Mungu tu atuonee huruma atufungue minyororo ya akili tuliyofungwa na shetani. Akina mama na beki 3 wanaharibu sana watoto kwa tamthlia hizi za kipuuzi. Na wakimaliza kutazama tamthlia wanahamia kusikiliza singeli, bongofleva, taarabu, vigodoro na nyimbo nyingine za kijinga kama hizo.

Inashangaza unamkuta mtoto anajua kusimulia tamthlia ya kichina mwanzo hadi mwisho lakini hajui historia ya nchi yake. Ifike wakati serikali itunge sheria kali ya kudhibiti ujinga huu ili kunusuru kizazi hiki na kizazi kijacho. Unadhani hawa watoto wanaotazamishwa tamthlia za kijinga wakiwa wazazi hili taifa litakuwa na watu wa aina gani? Nonsense!

 
Kutojua historia na kujua tamthilia vina mahusiano Kweli!?

Mbona kuna wasiojua vyote tamthilia wala historia na wapo wasiojua tamthilia wanajua historia na wale wasiojua historia wanajua tamthilia
 
Kutojua historia na kujua tamthilia vina mahusiano Kweli!?

Mbona kuna wasiojua vyote tamthilia wala historia na wapo wasiojua tamthilia wanajua historia na wale wasiojua historia wanajua tamthilia
Mbona tayari umejijibu mwenyewe mkuu? Hebu rudia kusoma uzi upya utanielewa barabara!
 
watu wasipate pesa kisa mtoto wako?
Sio mtoto wangu tu mkuu. Watoto wengi wanaharibiwa na hizi tamthlia, singeli na bongofleva. Hata yule mtoto aliyeshindwa kujibu maswali mbona sio mwanangu mkuu? Sote tukishirikiana kuokoa kizazi chetu tutakuwa na taifa bora hapo baadaye. usipinge kila kitu mkuu; be positive, flexible and humble!
 
Imekuuma Sana we jamaa watoto kushindwa kutaja Rais na makamu wa Zanzibar eeenh?

Hata wakiyajua haya yanawasaidia nini mwishowe?

Maisha Ni magumu Sana sasa hivi, acheni watu wa refresh asee hata na tamthilia, we kwa ugumu huu wa maisha unataka mtoto wa Urambo au Kitumbikwela Lindi akariri jina la waziri mdogo wa maji na nishati wa Zanzibar!
 
"Daddy gOVeRnMenT sHoulD d0 tHis,DaDdY gOveRnMenT sh0ulD d0 that"
Halafu baadae mnakuja kushangaa Serikali ikiwakatili,,wakti mnaiongezea nguvu wenyewe
 
Hilo ni jukumu la wazazi kumlea mtoto wao kwa mujibu wa maadili waiojiwekea wenyewe.

Serikali itapiga marufuku mangapi hapa nchini? Yalimshinda Nyerere hayo alikuwa hataki watu wamiliki TV, friji kwa kuwa ni anasa, matokeo yake ilikuwaje?
 
Hilo ni jukumu la wazazi kumlea mtoto wao kwa mujibu wa maadili waiojiwekea wenyewe.

Serikali itapiga marufuku mangapi hapa nchini? Yalimshinda Nyerere hayo alikuwa hataki watu wamiliki TV, friji kwa kuwa ni anasa, matokeo yake ilikuwaje?


Wewe mwache huyo aendelee kuilaumu tamthilia wakati T.V., decoder, umeme vyote analipa yeye mwenyewe🤣🤣🤣🤣
 
Hilo ni jukumu lako wewe mzazi au mlezi...

Leo watoto wako... wa mwenzio wakiwa vibaka waache ni mzigo wake...

Pambana na kibanzi ktk jicho lako na uachane na boliti ktk jicho la mwenzio...
 
Uongozi wa mkoa wa Mara ujitathmini, haiwezekani uwe muwakilishi wa Rais katika Mkoa halafu watu wasijue jina la Rais, ni aidha viongozi hawaendi kwa wananchi kwa ziara, au ni uzembe.

Huyo mkuu wa Mkoa, na wakuu wake wa Wilaya, wakurugenzi, maafisa tarafa na Kata, wameprove failure. Na kwa failure hiyo, Samia awatimue
 
Huna hoja mkuu.
Tamthilia haiwezi chanzo cha hicho unachodai
 
Inasikitisha sana mtoto wa darasa la saba kutofahamu historia ya nchi yake. Juzi nilimsikia kiongozi mmoja wa serikali akiwahoji baadhi ya wanafunzi maswali mepesi kabisa lakini wakashindwa kujibu. Ni aibu kubwa sana mwanafunzi wa darasa la saba anayetarajia kufanya mtihani wa kitaifa miezi 8 ijayo kuulizwa ataje matunda ya muungano anataja maembe, maparachichi, machenza na machungwa!

Nimekuwa nikifuatilia malezi ya watoto hapa mjini kwa muda mrefu; nimegundua watoto wanatumia muda mwingi kutazama tamthlia za kichina, kihindi na kifilipino wawapo nyumbani na kwenye mabanda ya kutazamia video. Hata inapofika saa 2 jioni badala ya kutyuni taarifa ya habari, wazazi hubadilisha na kuanza kutazama sinema.

Matokeo yake watoto wanashindwa kujibu maswali rahisi kama vile kutaja majina ya viongozi wakubwa nchini wakimwemo Waziri Mkuu, Rais wa Zanzibar na Waziri Mkuu. Hili ni tatizo kubwa. Yaani nchi hii tunakoelekea Mungu tu atuonee huruma atufungue minyororo ya akili tuliyofungwa na shetani. Akina mama na beki 3 wanaharibu sana watoto kwa tamthlia hizi za kipuuzi. Na wakimaliza kutazama tamthlia wanahamia kusikiliza singeli, bongofleva, taarabu, vigodoro na nyimbo nyingine za kijinga kama hizo.

Inashangaza unamkuta mtoto anajua kusimulia tamthlia ya kichina mwanzo hadi mwisho lakini hajui historia ya nchi yake. Ifike wakati serikali itunge sheria kali ya kudhibiti ujinga huu ili kunusuru kizazi hiki na kizazi kijacho. Unadhani hawa watoto wanaotazamishwa tamthlia za kijinga wakiwa wazazi hili taifa litakuwa na watu wa aina gani? Nonsense!
Walimu wanakula mishahara bure ila kila siku humu ni kutupigia kelele kuwa mishahara midogo for nothing....sijui serikali ina shindwa nini kutengeneza mfumo wa mishahara na mfumo wa kupanda madaraja walimu unao zingatia ufanisi wa shule na masomo kwa wanafunzi...hiyo ndiyo ingekuwa dawa ya walimu wapuuzi walio jazana mashuleni
 
Kutojua historia na kujua tamthilia vina mahusiano Kweli!?

Mbona kuna wasiojua vyote tamthilia wala historia na wapo wasiojua tamthilia wanajua historia na wale wasiojua historia wanajua tamthilia
Uzi wa Hovyo tangu kuanza kwa Mwaka
 
Back
Top Bottom