Serikali irudishe Tsh 20,000/= Ada ya sekondari kwa mwaka

Serikali irudishe Tsh 20,000/= Ada ya sekondari kwa mwaka

Kipindi wananchi wanatozwa kodi ya kichwa na baiskeli waliacha kufyatuana? Hizi kodi zilikuwa zinamgusa kila mwananchi moja kwa moja je ni mabadiliko gani ya maana yalitokea?
 
Pumzi imekata.

Mapato yamepungua mno.

Serikali haiwezi tena kutoa elimu bure na kufanya miradi ya maendeleo.
 
Bure inasababisha watu wasiwe responsible na maisha yao
 
Wazo lako hovyo kabisa kuwahi kulileta humu.

IHivi kama tunatozwa tozo kwa Mambo mengineyo kusaidia taifa,
Basi iongezwe tozo nyingine kwa ajiili ya elimu.

Ili mzigo huu wa elimu ubebwe na kila mtanzania..

20000 si kitu chochote kitakacho izidishia serikali.

Kama kila mwanainchi anakatwa tozo zaidi ya 500,000 kwa mwaka mzima,
Na hakuna cha maana kinachofanyika kwa tozo hizo.
Huo mchango wa 20000 itasaidia nn?

Sasa ni Bora tuongezewe tozo,,
Ili Maisha yawe magumu zaidi..
 
Hivi hapa hoja ni bure ama umuhimu wa huduma husika?.

Ni kweli bure ni aghali...lakini tuangalie lengo kuu la kufanya hivyo kabla ya hayo mengine...nadhani msingi hapa ni kwanza kwa serikali kutimiza wajibu wake, na pili ni kuhakikisha Mwananchi hapati kisingizio cha kutokumpeleka Mtoto shule.

Na wakati unatamani kuwe na ada ujue tu kuwa bado wapo wanaoshindwa kupeleka Mtoto shule kwa visingizio vingine kama kukosa unifomu n.k.

Kutokuweka ada kuwe kama njia mbadala ya kuwalazimisha Wazazi kuwapeleka Watoto shule...wakielimika wengi nadhani hata hiki unachokiandika watakuelewa kwa urahisi.
 
Wewe ndiyo hujamuelewa!
Taikoni anamaanisha kwamba tusubiri tutajirike ndipo tutoe elimu ya bure..
Maana bado tu maskini mno.
Nami namuunga mkono.
Sijui Kama ulichoandika unakielewa vizuri. Nchi zenye uchumi imara karibu zote hutoa huduma za kijamii bure, Sasa tuseme na wao wanaupenda umaskini?

Mara kadhaa humu watu wanasifi nchi za ulaya kuwa elimu kuanzia kindergarten hadi chuo kikuu ni bure. Sasa sijui na wao tusemaje
Huko wameenda mbali wana hadi package kwa wale ambao ni unemployed.
 
ILI KUWEZA KUPATA KURA ZA WANAWAKE UCHAGUZI WA MWAKA 2015 IKABIDI WATEUE MGOMBEA MWENZA MWANAMKE ILI KUZIPATA KURA HIZO KWA URAHISI.

WAKASAHAU KUWA KUNA KESHO NA YULE WALIEMTEUA HAWAKUJUA AU KWA KUJUA KUWA HATOSHI KABISA KUWA RAISI LIKITOKEA LA KUTOKEA.

WOTE WALIOSHIRIKI MCHAKATO ULE WALAANIWE WAO NA KIZAZI CHAO HADI CHA NNE.
yet unakula na kulala.... chini ya huyo asiefaa
 
watu ni masikini, simple! niko wa kabila fulani, wao ni madarasa, hiyo mtoto atapigwa mpaka afe kama hakwenda, lakini hizi formal classes ni hiari ya mtoto kwenda. Ukiweka na ada umewamaliza!

😀😀

Waache kusoma waendelee kuwa Watumwa wa wengine huo ndio uchaguzi wao
 
Anaeshauri kuwa elimu iwe na ada yeye mwenyewe chuo kikuu kadoma kwa mkopo na hajalipa deni Sasa sijui akili za wapi hizi anatumia.
Elimu bure iliwekwa kwa Sababu ya umasikini wa Wananchi ili watoto waweze kusoma kwa Sababu elimu ni haki na Kila mwenye sifa ya kuipata anatakiwa aipate .
Kwenye swala la uzazi wa mpango nakuunga mkono
 
watu ni masikini, simple! niko wa kabila fulani, wao ni madarasa, hiyo mtoto atapigwa mpaka afe kama hakwenda, lakini hizi formal classes ni hiari ya mtoto kwenda. Ukiweka na ada umewamaliza!

Umasikini WA watu unatokana na Mtazamo mbaya na ujinga ulioletwa na Uvivu.

Mtu anawatoto wakubwa wa miaka 15 wapo sekondari anashindwaje kuwafanya wapate 20,000 Kwa mwaka wapate Ada ya shule?

Ni vile serikali nayo bado inazembeazembea makusudi ili nchi uendelee kuwa Masikini.

Burebure haijawahi kumsaidia masikini tangu dunia ianze mpaka itakapoisha

Watu walipie Kwa kila watakacho hiyo ndio namna ya kuisaidia nchi

Sema gharama ndio iangaliwe kulingana na Hali za watu wa nchi.
 
Kwema Wakuu!

Serikali inapaswa iirejeshe Ada kwa wanafunzi wanaosoma shule, nchi yetu bado hatujafikia nyakati za kutoa vitu bure,

Shule ya Msingi ndio iwe Bure lakini sekondari, wanafunzi watoe pesa,
Isiwe pesa kubwa Sana, iwe Tsh 20,000/= Kwa familia yenye watoto watano ni 100,000/= Kwa mwaka, nusu mhula 10,000/=

Raia wasipende Dezodezo, wasipende burebure Kwa kisingizio nchi ni Tajiri, hakunaga Utajiri Kwa watu wanapenda Dezo, wanaopenda vyabure.

Mimi sikubalianagi na Wanasiasa wanaohubiri kutoa vitu vya bure, unatoa vitu vya bure kwa misingi ipi, bure inafaa Kwa makundi maalumu ya watu Kama Walemavu lakini tofauti na hapo hakuna bure.

Watoto wanatoka shuleni mapema Kwa vile hawana kazi wanaishia mitaani vijiweni Kupiga Umbeya, kujadili vitu vya kipuuzi, wengine wanajiingiza kwenye madawa ya kulevya huku wasichana wakijitafutia mabwana Kwa sababu ya kukosa kazi watokaoo shuleni.

Wakati tunasoma wengine tumeshalima Sana vibarua, tumebeba Kago, tumeosha magari, tumeuza miwa na sambusa ili kupata pesa za kujikimu kuwasaidia wazazi ambao ni masikini.

Ndio wazazi wetu Sisi Kama watoto ilikuwa wajibu wetu kuwasaidia na sio kwenda vijiweni bila ya kazi alafu ukikosa Ada shuleni mnailaumu serikali.

Serikali lipisheni Ada na iwe ni lazima watoto waende shule,
Ada itasaidia mambo mengi, itawarahisishia mambo katika sekta ya elimu,

Masuala ya mishahara ya waalimu unaweza kusaidia, kuajiri waalimu wapya itasaidia, na miundombiny mingine katik sekta ya elimu.
Kila sekta inatakiwa iwe na uwezo wa kujitegemea ili Kupunguza utegemezi Kati ya sekta moja na nyingine.

Faida zingine za kurejesha Ada
1. Uzazi wa mpango utazingatiwa.
Tabia ya watu kuzaa bila mipango itapungua.
Maana kuna watu wanazaa bila mpango alafu watoto wanawatupia shuleni Kwa waalimu Asubuhi mtoto anaondoka hanywi hata chai anarudi jioni. Wanaichukulia shule Kama sehemu ya Kupunguza bajeti ya familia. Elimu sinibure bhana!

Moja ya mbinu ya kudhibiti ongezeko kubwa la watu lenye athari Hasi ni kupandisha gharama za maisha, ukiachia mbinu zingine Kama Elimu, propaganda, Maradhi n.k.

2. Kuondoa kasumba ya Kupenda burebure na utegemezi!
Kasumba ya uburebure ipo Kwa jamii masikini, mtoto tangu akiwa mdogo anasoma lazima aone wazazi wake na Yeye mwenyewe akiwajibika, hii itamfanya ayaelewe maisha Kwa upesi zaidi kuwa Maisha sio burebure.

Vile mtoto anavyosumbuliwa Ada au kufukuzwa Ada inamjengea fikra za majukumu, nyakati za jioni akirudi lazima ashiriki kazi za nyumbani za uzalishaji kama kilimo, ufugaji, au biashara ndogondogo kuwasaidia wazazi wake kwani anajua Kwa kufanya hivyo ni ili apate Ada asome.

Wazazi nao wawaambie watoto kuwa kazi wazifanyazo ndizo zinazolisha familia na kuwasomesha watoto, hii itafanya watoto waheshimu kazi kwani watakuwa wanashiriki kazi hizo.

Siku hizi ni nadra Sana kumkuta mtoto akimsaidia mzazi wake kazi za uzalishaji Mali awapo likizo au akitoka jioni shuleni Ile saa tisa, hasa huku mjini.

Mambo ya burebure yametengeneza Matoto ya burebure, kupenda vitu bila kutoa jasho, sio Kwa mabinti sio Kwa Vijana.
Mabinti yanapenda pesa za burebure Kwa vile yamelelewa hivyo, yaani kisa ni mwanamke ndio upewe bure hiyo ni Akili za jamii fukara.

Taikon mara zote nawaambiaga ukiona Msichana anapenda burebure kuomba pesa hata hajafanya kazi yeyote huyo ni Shetani chumaulete, ni aibu Kwa mtu mwenye akili timamu zenye kufanya kazi kuomba pesa au kukubali pesa ya burebure.
Halikadhalika na vijana.

Mambo haya yalisababishwa na ujamaa, mambo ya ujamaa tuachane nayo Kwanza.

3. Kizazi chenye kuwajibika na wachapakazi.
Huwezi ukazaa watoto ukitegemea serikali ikusomeshee watoto hao, huo ni uhuni. Ukizaa watoto wajibika Kwa watoto wako, wazazi wanachopaswa kuiomba serikali ni Kupunguza gharama na sio kuiondoa kabisa, huko ni kuipa serikali mizigo alafu baadaye unailaumu serikali Kwa nini inakopa.

Wazazi waelewe kuwa kadiri unavyozaa ndivyo unatakiwa kuzidi kuchapa Kazi zaidi na zaidi Kwa ajili ya familia yako. Sio uzae Matoto mengi alafu Ada utake bure alafu uanze kuilaumu serikali haijajenga madarasa, sijui haijaajiri waalimu WA kufundisha watoto wako, sijui shule haina vifaa huo ni ukichaa.

Wingi unamaana Kwa watu wenye akili, unaweza kuzaa watoto hata Mia moja lakini kama ni wazembe hawana maana yoyote zaidi ya kuleta mabalaa katika Dunia.

4. Watoto kuwa na uchungu wa shule.
Siku zote kitu cha Bure kamwe hakijawahi kuwa na thamani. Mtoto vile anavyoona wazazi wake wanahenyeka kumsomesha anapata hamasa ya kusoma zaidi ili kuwafurahisha wazazi wake.


5. Kuongeza Upendo wa mtoto Kwa wazazi.
Alafu jinsi ilivyo kadiri mzazi anavyohangaika kumsomesha mtoto Kwa nguvu kubwa ndivyo mtoto anavyoongeza mapenzi Kwa mzazi wake.

Wazazi wanaopenda mambo ya burebure husababisha watoto wao wasiwachukulie Sirius Sana ukilinganisha na wazazi waliomenyeka kuwalea watoto wao(shule ikiwemo).

Ndio maana watoto wa Matajiri wanaupendo mara mbili Kwa wazazi wao tofauti na watoto wa masikini, kanuni inasema ukitoa kidogo utapendwa kidogo, ukitoa kikubwa utapendwa pakubwa.

Mzazi aliyemenyeka kuuza mitumba au pombe za kienyeji au vitumbua kisa kumsomesha mtoto, anapendwa zaidi na mtoto wake kuliko mzazi ambaye hakufanya jitihada yoyote zaidi ya kuitupia serikali asome mtoto bure Kwa kisingizio cha umasikini. Upendo hauna kisingizio.

Serikali inachopaswa kufanya ni kuweka gharama ndogo zinazoendana na Watanzania waliowengi na sio kuondoa kabisa Ada katika shule za sekondari.

Tuache kulipia Ada za Shule ikifika mwaka 2200 huko Nchi ikiwa imeendelea,
Sio sasa Waalimu hawatoshi, hakuna vifaa, hakuna miundombinu.

Hao wanaotoa elimu bure walimenyeka miaka iliyopita,
Vinginevyo tuvamie mataifa mengine Kama nilivyowahi kusema.

Nawatakia maandalizi Mema ya SABATO

Sijasoma makala yako, lkn nilivyo nilivyoona heading nimeunga mkono hoja yako. Wazazi lazima wawajibike na kuipa thamani elimu ya watoto wao. Labda kwa wale wenye hali ngumu ndiyo wapate elimu bila malipo.
 
Anaeshauri kuwa elimu iwe na ada yeye mwenyewe chuo kikuu kadoma kwa mkopo na hajalipa deni Sasa sijui akili za wapi hizi anatumia.
Elimu bure iliwekwa kwa Sababu ya umasikini wa Wananchi ili watoto waweze kusoma kwa Sababu elimu ni haki na Kila mwenye sifa ya kuipata anatakiwa aipate .
Kwenye swala la uzazi wa mpango nakuunga mkono

Kusoma Kwa mkopo tangu lini ikawa bure Sheikhe?
Au hujui maana ya mkopo?

Sijawahi kusoma bure, sijafundishwa kupewa mambo ya burebure.

Na ndio maana nalitumikia taifa kuielimisha jamii bila kulipwa na yoyote Yule nikijua nchi yangu inanidai na mambo mengi, achilia mbali kusoma Chuo kikuu.
 
Sijasoma makala yako, lkn nilivyo nilivyoona heading nimeunga mkono hoja yako. Wazazi lazima wawajibike na kuipa thamani elimu ya watoto wao. Labda kwa wale wenye hali ngumu ndiyo wapate elimu bila malipo.

Wenye Hali ngumu watoto wao wanaweza kuchangia Matofali Kwa kuyafyatua yanayolingana na gharama za Ada. Mbona rahisi tuu.

Wala usingesikia habari za uhaba WA madarasa.

Mtaji wa masikini ni nguvu zake mwenyewe, Kama sio mzazi basi mtoto awajibike.

Ndio maana nikasema watoto wa shule ya Msingi wao Kwa vile ni wadogo wasilipe Ada, Ila hawa wa sekondari walipe Ada, Kama hawawezi Kwa ufukara WA pesa basi serikali kupitia kila shule iandae Miradi ambayo watoto hao kupitia likizo wawe wanafanya kazi kujilipia Ada.
 
Wenye Hali ngumu watoto wao wanaweza kuchangia Matofali Kwa kuyafyatua yanayolingana na gharama za Ada. Mbona rahisi tuu.

Wala usingesikia habari za uhaba WA madarasa.

Mtaji wa masikini ni nguvu zake mwenyewe, Kama sio mzazi basi mtoto awajibike.

Ndio maana nikasema watoto wa shule ya Msingi wao Kwa vile ni wadogo wasilipe Ada, Ila hawa wa sekondari walipe Ada, Kama hawawezi Kwa ufukara WA pesa basi serikali kupitia kila shule iandae Miradi ambayo watoto hao kupitia likizo wawe wanafanya kazi kujilipia Ada.

Tumefyatua sana matofali kwenye kazi au elimu ya kujitegemea (ek) almaarufu kama self reliance activities.
 
Kwema Wakuu!

Serikali inapaswa iirejeshe Ada kwa wanafunzi wanaosoma shule, nchi yetu bado hatujafikia nyakati za kutoa vitu bure,

Shule ya Msingi ndio iwe Bure lakini sekondari, wanafunzi watoe pesa,
Isiwe pesa kubwa Sana, iwe Tsh 20,000/= Kwa familia yenye watoto watano ni 100,000/= Kwa mwaka, nusu mhula 10,000/=

Raia wasipende Dezodezo, wasipende burebure Kwa kisingizio nchi ni Tajiri, hakunaga Utajiri Kwa watu wanapenda Dezo, wanaopenda vyabure.

Mimi sikubalianagi na Wanasiasa wanaohubiri kutoa vitu vya bure, unatoa vitu vya bure kwa misingi ipi, bure inafaa Kwa makundi maalumu ya watu Kama Walemavu lakini tofauti na hapo hakuna bure.

Watoto wanatoka shuleni mapema Kwa vile hawana kazi wanaishia mitaani vijiweni Kupiga Umbeya, kujadili vitu vya kipuuzi, wengine wanajiingiza kwenye madawa ya kulevya huku wasichana wakijitafutia mabwana Kwa sababu ya kukosa kazi watokaoo shuleni.

Wakati tunasoma wengine tumeshalima Sana vibarua, tumebeba Kago, tumeosha magari, tumeuza miwa na sambusa ili kupata pesa za kujikimu kuwasaidia wazazi ambao ni masikini.

Ndio wazazi wetu Sisi Kama watoto ilikuwa wajibu wetu kuwasaidia na sio kwenda vijiweni bila ya kazi alafu ukikosa Ada shuleni mnailaumu serikali.

Serikali lipisheni Ada na iwe ni lazima watoto waende shule,
Ada itasaidia mambo mengi, itawarahisishia mambo katika sekta ya elimu,

Masuala ya mishahara ya waalimu unaweza kusaidia, kuajiri waalimu wapya itasaidia, na miundombiny mingine katik sekta ya elimu.
Kila sekta inatakiwa iwe na uwezo wa kujitegemea ili Kupunguza utegemezi Kati ya sekta moja na nyingine.

Faida zingine za kurejesha Ada
1. Uzazi wa mpango utazingatiwa.
Tabia ya watu kuzaa bila mipango itapungua.
Maana kuna watu wanazaa bila mpango alafu watoto wanawatupia shuleni Kwa waalimu Asubuhi mtoto anaondoka hanywi hata chai anarudi jioni. Wanaichukulia shule Kama sehemu ya Kupunguza bajeti ya familia. Elimu sinibure bhana!

Moja ya mbinu ya kudhibiti ongezeko kubwa la watu lenye athari Hasi ni kupandisha gharama za maisha, ukiachia mbinu zingine Kama Elimu, propaganda, Maradhi n.k.

2. Kuondoa kasumba ya Kupenda burebure na utegemezi!
Kasumba ya uburebure ipo Kwa jamii masikini, mtoto tangu akiwa mdogo anasoma lazima aone wazazi wake na Yeye mwenyewe akiwajibika, hii itamfanya ayaelewe maisha Kwa upesi zaidi kuwa Maisha sio burebure.

Vile mtoto anavyosumbuliwa Ada au kufukuzwa Ada inamjengea fikra za majukumu, nyakati za jioni akirudi lazima ashiriki kazi za nyumbani za uzalishaji kama kilimo, ufugaji, au biashara ndogondogo kuwasaidia wazazi wake kwani anajua Kwa kufanya hivyo ni ili apate Ada asome.

Wazazi nao wawaambie watoto kuwa kazi wazifanyazo ndizo zinazolisha familia na kuwasomesha watoto, hii itafanya watoto waheshimu kazi kwani watakuwa wanashiriki kazi hizo.

Siku hizi ni nadra Sana kumkuta mtoto akimsaidia mzazi wake kazi za uzalishaji Mali awapo likizo au akitoka jioni shuleni Ile saa tisa, hasa huku mjini.

Mambo ya burebure yametengeneza Matoto ya burebure, kupenda vitu bila kutoa jasho, sio Kwa mabinti sio Kwa Vijana.
Mabinti yanapenda pesa za burebure Kwa vile yamelelewa hivyo, yaani kisa ni mwanamke ndio upewe bure hiyo ni Akili za jamii fukara.

Taikon mara zote nawaambiaga ukiona Msichana anapenda burebure kuomba pesa hata hajafanya kazi yeyote huyo ni Shetani chumaulete, ni aibu Kwa mtu mwenye akili timamu zenye kufanya kazi kuomba pesa au kukubali pesa ya burebure.
Halikadhalika na vijana.

Mambo haya yalisababishwa na ujamaa, mambo ya ujamaa tuachane nayo Kwanza.

3. Kizazi chenye kuwajibika na wachapakazi.
Huwezi ukazaa watoto ukitegemea serikali ikusomeshee watoto hao, huo ni uhuni. Ukizaa watoto wajibika Kwa watoto wako, wazazi wanachopaswa kuiomba serikali ni Kupunguza gharama na sio kuiondoa kabisa, huko ni kuipa serikali mizigo alafu baadaye unailaumu serikali Kwa nini inakopa.

Wazazi waelewe kuwa kadiri unavyozaa ndivyo unatakiwa kuzidi kuchapa Kazi zaidi na zaidi Kwa ajili ya familia yako. Sio uzae Matoto mengi alafu Ada utake bure alafu uanze kuilaumu serikali haijajenga madarasa, sijui haijaajiri waalimu WA kufundisha watoto wako, sijui shule haina vifaa huo ni ukichaa.

Wingi unamaana Kwa watu wenye akili, unaweza kuzaa watoto hata Mia moja lakini kama ni wazembe hawana maana yoyote zaidi ya kuleta mabalaa katika Dunia.

4. Watoto kuwa na uchungu wa shule.
Siku zote kitu cha Bure kamwe hakijawahi kuwa na thamani. Mtoto vile anavyoona wazazi wake wanahenyeka kumsomesha anapata hamasa ya kusoma zaidi ili kuwafurahisha wazazi wake.


5. Kuongeza Upendo wa mtoto Kwa wazazi.
Alafu jinsi ilivyo kadiri mzazi anavyohangaika kumsomesha mtoto Kwa nguvu kubwa ndivyo mtoto anavyoongeza mapenzi Kwa mzazi wake.

Wazazi wanaopenda mambo ya burebure husababisha watoto wao wasiwachukulie Sirius Sana ukilinganisha na wazazi waliomenyeka kuwalea watoto wao(shule ikiwemo).

Ndio maana watoto wa Matajiri wanaupendo mara mbili Kwa wazazi wao tofauti na watoto wa masikini, kanuni inasema ukitoa kidogo utapendwa kidogo, ukitoa kikubwa utapendwa pakubwa.

Mzazi aliyemenyeka kuuza mitumba au pombe za kienyeji au vitumbua kisa kumsomesha mtoto, anapendwa zaidi na mtoto wake kuliko mzazi ambaye hakufanya jitihada yoyote zaidi ya kuitupia serikali asome mtoto bure Kwa kisingizio cha umasikini. Upendo hauna kisingizio.

Serikali inachopaswa kufanya ni kuweka gharama ndogo zinazoendana na Watanzania waliowengi na sio kuondoa kabisa Ada katika shule za sekondari.

Tuache kulipia Ada za Shule ikifika mwaka 2200 huko Nchi ikiwa imeendelea,
Sio sasa Waalimu hawatoshi, hakuna vifaa, hakuna miundombinu.

Hao wanaotoa elimu bure walimenyeka miaka iliyopita,
Vinginevyo tuvamie mataifa mengine Kama nilivyowahi kusema.

Nawatakia maandalizi Mema ya SABATO
Naunga mkono hoja,Ada itafanya wazazi wafuatilie mwenendo na maendeleo ya mtoto wao..

Saizi kwenye bure wanawasukumizia walimu na Serikali afu wanaanza kulaumu.
 
Umasikini WA watu unatokana na Mtazamo mbaya na ujinga ulioletwa na Uvivu.

Mtu anawatoto wakubwa wa miaka 15 wapo sekondari anashindwaje kuwafanya wapate 20,000 Kwa mwaka wapate Ada ya shule?

Ni vile serikali nayo bado inazembeazembea makusudi ili nchi uendelee kuwa Masikini.

Burebure haijawahi kumsaidia masikini tangu dunia ianze mpaka itakapoisha

Watu walipie Kwa kila watakacho hiyo ndio namna ya kuisaidia nchi

Sema gharama ndio iangaliwe kulingana na Hali za watu wa nchi.
Nasema ukiweka ada hiyo kuna watu haya mambo ya western education is not an issue to them, wataacha na nchi itakuwa na lundo la wajinga, I guess you see my point! Let them at least have primary and if possible secondary education
 
Ujinga wa kiwango cha marumaru.

Unamlipia mzazi ada ya mwanae tshs 70000/- kwa mwaka wakati huo huo mzazi mwenyewe ana uwezo wa kunywa bia 6 kwa siku
 
Back
Top Bottom