Serikali itunge Sheria ili mahojiano kati ya trafiki na dereva yafanyike huku abiria wakisikia Kila kitu. Kama inataka kufuta rushwa Kwa trafiki

Serikali itunge Sheria ili mahojiano kati ya trafiki na dereva yafanyike huku abiria wakisikia Kila kitu. Kama inataka kufuta rushwa Kwa trafiki

Unataka wakose afutatu za kubrashia?


Gari za masafa marefu(Dar -Mwanza, Mbeya, Kagera, Mara, Tunduma n.k) kila siku lazima zipoteze sio chini ya 30k kwa kuwalipa matrafiki.

Hili nimeliona mara kadhaa baada kukaa kwenye kigodoro nikipanda gari hizo. Konda kila akiona anakaribia kijiwe cha hao jamaa, anakunja elfu 5 kwenye kikaratasi, akifika anashuka fasta anasalimiana naye chini mbele ya gari, sekunde 5 tu gari inasepa.

Kuna trafiki pale Mtumbatu kuelekea Gairo walikuwa wanawake 3, bila aibu ya kike wakachukua buku 5 wakiwa wamekaza sura kabisa.

Rushwa haiwezi kuisha nchi hii hata kama sheria ngumu na kali kiasi gani zitungwe hii ni kutokana na wasimamizi wa sheria ndio vinara wa Rushwa
magari mengi hayakosi makosa madogo madogo, sasa ipi Nafuu, umpe buku ya kubrashia viatu uondoke zako au ukatiwe mkeka wa elf 30 uje utoe povu huku na unajua kabisa una makosa
 
Ndugu wanabodi huwa nakerwa sana na hii tabia ya askari wa usalama barabarani kuchukuana na kondakta au dereva wa gari na kuenda kumalizana nyuma ya gari.

Utamaduni huu unafuga rushwa na kupelekea zoezi la ukaguzi wa magari kufanywa kisanii tu.
Naiomba serikali ipitishe Sheria mahojiano kati ya dereva na traffic yasifanyike Kwa kificho.
Kwa nadharia inawezekana ila si kwa vitendo na si kwa askari tu mambo mengi waliokua wanaamua viongozi wetu mengi kwa nadharia ya darasani yana wezekana ila c ku'apply uswahilini! Kifupi haiwezekani
 
Unawazo nzuri lakini kabla hatujafikia huko ujue matrafiki wenyewe wanawahurumia hapo madereva na makondakta angalao nao wapate mboga ya watoto. Ok Sasa traffic anyooshe ruler mbele ya abiria,, kosa la kwanza mbona umesimamisha abiria hapo Kuna faini mjue, mbona hujavaa uniform, speed, uchakavu wa gari( iwe kioo cha mbele kina alama ya mpasuko tu ukumbuke ni kosa, tairi lishanza ukipara ni kosa), na Mambo mengine mengi tu. Madereva sio wajinga kuunga umoja nao.
 
Ndugu wanabodi huwa nakerwa sana na hii tabia ya askari wa usalama barabarani kuchukuana na kondakta au dereva wa gari na kuenda kumalizana nyuma ya gari.

Utamaduni huu unafuga rushwa na kupelekea zoezi la ukaguzi wa magari kufanywa kisanii tu.
Naiomba serikali ipitishe Sheria mahojiano kati ya dereva na traffic yasifanyike Kwa kificho.
Trafiki wamekuwa wasumbufu na wababaishaji sana. Na mbaya wanaonea sana watu. Mpaka nashangaa kuna nini kinaendelea.
Hawana wanalofanya. Mbona ajari zinaendelea kuongezeka? Bora hata walivyopotea
 
Ndugu wanabodi huwa nakerwa sana na hii tabia ya askari wa usalama barabarani kuchukuana na kondakta au dereva wa gari na kuenda kumalizana nyuma ya gari.

Utamaduni huu unafuga rushwa na kupelekea zoezi la ukaguzi wa magari kufanywa kisanii tu.
Naiomba serikali ipitishe Sheria mahojiano kati ya dereva na traffic yasifanyike Kwa kificho.
kila nimuonapo polisi huwa naamini nimemuona binadamu asiye na akili timamu. pigia mstari akili timamu
 
tutawaua njaa ma-trafic wetu na kazi wataiona chungu; tuwaache maana maisha yatakuwa magumu kwao - 1.2m kwa mwezi una familia ya watu 6 home utakimbia mji. 😀
Kwa hiyo turuhusu rushwa Kwa polis? Waalimu je? Manesi na daktari je? Watumishi wengine wengi wanaolipwa kima cha chini je?
 
Kwa Tanzania bado sana kuondoa au hata kupunguza hiyo rushwa ya barabarani. Hapo Kenya wameenda mbali zaidi kuondoa hii rushwa ya barabarani kwa kuweka sheria ngumu ya kuwa hakuna trafiki atakayeruhusiwa kusimamisha gari barabarani kama hana "reflactor jacket" maalum. Reflactor Jacket hiyo inayotolewa na serikali ya Kenya kwa askari wake wa barabarani ina kamera na kinasa sauti kwa hiyo kwa mazungumzo kati ya dereva na askari wa barabarani yanachukuliwa video na sauti kwa wakati mmoja.
Hii mbinu imesaidia kweli?
 
Mimi nlijuwa mleta mada,anaomba serikali itambue rushwa rasmi [emoji1]

Traffic wenyewe wanatumwa na wakubwa zao kukusanya hela

Ova
Hebu jaribu kutoa mfano wa maisha ambayo rushwa imerasimishwa yanaweza kuwaje
 
magari mengi hayakosi makosa madogo madogo, sasa ipi Nafuu, umpe buku ya kubrashia viatu uondoke zako au ukatiwe mkeka wa elf 30 uje utoe povu huku na unajua kabisa una makosa
Ninachotaka mimi Sheria zifuatwe gari likiwa na dosari lisiruhusiwe kutembea barabarani. Maana vigezo vya gari kuwa complete viliwekwa ili kuwalinda watu na madhara yatokanayo na hayo mapungufu.
Kuleta huruma kwenye mambo ya kitaalamu ni kujihatarisha kinachotakiwa ni kuizuia rushwa
 
Kawaida gari ya abiria inaposimamishwa na polisi, anatakiwa aingie ndani , asalimie abiria na aeleze sababu za kusimamisha gari. Mf. Kama dereva hana leseni abiria wajulishwe!
 
Kawaida gari ya abiria inaposimamishwa na polisi, anatakiwa aingie ndani , asalimie abiria na aeleze sababu za kusimamisha gari. Mf. Kama dereva hana leseni abiria wajulishwe!
Asante sana Kwa ufafanuzi mzuri mbona sasa traffic wetu hawafanyi hivyo kabisa? Nani wa kuwawajibisha?
 
Back
Top Bottom