Serikali itunge sheria kuhusu uzazi wa mpango angalau watoto wawili kila familia maana kasi ya uzazi Tanzania inatisha

Tanzania idadi ya watu ni ndogo mno ukilinganisha na ukubwa wa eneo,USITUTINGISHE TUNAPOFYATUA,lengo ni kuifikia China na pia to be most populated country in Africa.
Kwa kuwa na watu wapya,labda watakuja na fikra mpya!!!
 
Nchii hii tukifika milioni 300 ndio akili zetu zitapumzika kuzaliana

Mtaji wa maendeleo ni watu sio fedha

Bila watu hakuna fedha
 
Serikali isiingilie suala la uzazi lkni Vilevile watu wajitambue...
Kuna watu wanawaza ardhi tu,,jena una resources za kustahimili population hio yote!milioni 60 yenyewe hali ngumu,,tukifika milioni 100 sitamani kuona itakuaje
resources tunazo nyingi sana za kuweza kuhudumia population ya billion people,tunachotakiwa Ni kupanua na kuboresha huduma za afya, kurekebisha mfumo wa elimu ili tuwe na elimu ya kisasa. kama madini, mistu, mafuta, gesi, water bodies , ardhi yenye rutuba, vivutio vya utalii vyote tunavyo
 
Mimi nilifika mji mdogo wa isaka, kila mwanamke inayokutana naye kama hanyonyeshi basi ana mimba. Hali kanda ya ziwa inatisha
 
Hujui ulinenalo

Sent from my SM-G9350 using JamiiForums mobile app
 
Kuna baadhi ya vitengo hapa Tanzania havina wataalam wa kutosha,
Acha tuzae tujaze wataalam.
 
Mimi mfanyabiashara wa nguo za watoto sikubaliani na Hilo wazo

Watu zaeni tu
 
Ungekuwa umeizunguka Tz japo robo tu ya nchi,nadhani usingeleta uzi huu.
 
Nigeria kwa sasa haikamatiki kwa uchumi kwasababu ya wingi wa watu.Mfano ukienda Dar hata ukifungua kibanda cha chips biashara inaenda mana watu wqpo wa kutosha.Chukulia ndio kila mkoa uko hizo.Tuzae jamani.Tufyatue watoto.
 
Ni ujinga sana kuleta kiumbe duniani wakati haujamuandalia mazingira ya kulea,ni utesaji,ujinga na laana. Ni kutengeneza majambazi,magaidi, dada poa n.k. tuepuke huu ujinga!

Wenzetu waliyaona haya ya uzazi wa mpango zamani sana,usiwe sehemu ya wajinga kwa kuzaa ovyo
 
Kuna kijiji kipo karibia na Kilindi Tanga, Watoto chini ya miaka mitano hawajawahi kuisha, yaani nafikiri ndio alama ya kufahamu unapokwenda..
 
Umeuliza swali la msingi sana maana mwanaume mmoja anaweza kuwa na wake hadi watatu na mwanamke anaweza kuwa aliolewa akazaa watoto wawili kisha akaachika na kuja kuolewa tena na mwanaume ambaye hana kabisa mtoto.
πŸ™πŸ™βœ
 
Kwa kwel hali ni mbaya,ukiwa hospital kitengo cha watoto unaweza fanya kazi mpaka ukasahau kunywa chai,kuna mijitu mpaka unataman uipige makofi ni masikin la kutupwa hata kujenga limeshndwa lakin linazaa asubuhi na mchana
Naisikitikia Sana nchi yetu Mana watu wanabeza ushauri wangu wakati watoto wanaozaliwa hata mahitaji mhimu hawapati.Ukicheki watoto wengi wametelekezwa au wanalelewa na bibi kijijini ajabu Hawa ndo wanadai eti nchi kubwa Sana hii rasilimali kibao,ni ajabu Sana.
 

Hatupangiwi....acha kuingilia mambo ya watu
 
mwendazake aliwaambie wafyatue, mana utajiri wa nchi ni utajiri wa watu
 
Hatupangiwi....acha kuingilia mambo ya watu
Sio hivo mkuu Wala sikupangii tatizo lipo kuzaa watoto na kuwatelekeza .Zaa watoto ambao unaweza watunza na kuwaendeleza kielimu na kiuchumi.Cheki mtaana kwako watoto wengi wanalelewa na bibi Sasa huo ni ustarabu kweli?
 
mwendazake aliwaambie wafyatue, mana utajiri wa nchi ni utajiri wa watu
Utajiri gani wa watu ambao ni masikini? Hata mstaafu Jk Kikwete mwaka 2012 kipindi anapokea riport ya sensa ya watu na makazi alionya ongezeko kubwa la watu wakati uchumi ni mbovu.
Tukuze kwanza uchumi badae ndo tuzaliane.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…