Serikali iunganishe Dar na Pwani uwe mkoa mmoja uitwe Dar ili watu wazidi kusogea nje ya mji

Serikali iunganishe Dar na Pwani uwe mkoa mmoja uitwe Dar ili watu wazidi kusogea nje ya mji

wazo lako zuri ila kwanini TZ yote isiitwe Dar es salaam ili hao wanaorundikana wabaki hapo hapo Dar waliyopo wachangamkie fursa.

mfano; mtoa mada unakuwa Dar mtaa/wilaya/kata/kitongoji/kijiji cha Singinda, Tanga,Mtwara

hapo vipi??
 
Uko sahihi, ila kwa upande wangu naona ni bora kuchukua maeneo kadhaa ya mkoa wa Pwani kama vile Bagamoyo, Kibaha, Chalinze, kisarawe na kibiti hayo maeneo ndio yawe sehemu ya Dar mana mkoa wa pwani ni mkubwa sana (hvy kwa kufanya hvy itakuwa ni sawa na kugawa mkoa wa pwani kupata mikoa miwili)
 
Tena ni beach kabisa ila watu wanapadharau sana.
Zamani hii yote iliitwa Mzizima, ila kiukweli ukienda Pwani unashangaa maendeleo bado sana yaan hata barabara tuu changamoto,

Kuna sehemu inaitwa Shungubweni waliotoka huko wakaja Mjini hawataki kurudi kwao maana hata barabara hakuna,
Sehemu ipo jirani na Mkuranga tuu hapo ambapo ni 22km kutoka Dar
 
Kwa kifupi tunasema Dar ni Pwani na Pwani ni Dar, sababu huwezi kuona gari ya abiria imeandika Dar to Mlandizi, Dar to Mkuranga, Dar to Bagamoyo, Dar to Kisarawe, Dar to kibaha, Dar to kibiti au Rufiji, ila utaona Mbezi to Mlandizi, Mbagala to Mkuranga, Gongolamboto to Kisarawe n.k, na watu wengi wa Pwani hawasemi naenda Dar ila utamsikia mtu kutoka Mkuranga akisema naenda Mbagala au Temeke, na mtu wa Kisarawe atasema naenda Gongolamboto, na mtu kutoka Dar hasemi naenda Pwani ila husema naenda Mlandizi, Chalinze, Bagamoyo au Mkuranga
Basi kama mambo ni hivi, mtoa mada hoja yake inamashiko sana mamlaka wapokee wazo hili.
 
Heri ya mwaka mpya wakuu

Hivi kwanini serikali isiunganishe mikoa ya Dar na Pwani kisha huo mkoa uitwe Dar na tubaki na mikoa 30 tu, hakuna haja ya kuwa na mikoa mingi huku maendeleo yakiwa ni madogo na idadi ya watu ikilundikana kwenye vimiji vichache tu, kusema kwamba tutamaliza mapori na kuharibu mazingira kwa vizazi vijavyo ni upotoshaji kwa sababu Tanzania bado hakuna population ya kumaliza mapori yote tuliyonayo

Ni ajabu kwamba mkoa mdogo kijiografia kuliko yote nchini ndio mkoa mkubwa kidemografia kuliko yote nchini, ukiuliza sababu hakuna sababu ya maana utapewa zaidi ya watu wengi hasa vijana, kutaka waonekane wanaishi Dar hata kama maisha yao hayaeleweki na huko mikoani wameona fursa

Juzi nilikuwa nasikiliza interview ya Mwijaku alipokuwa anawajibu watu wanaosema kwamba kajenga ghorofa lake kwenye kaeneo kadogo, akasema alikuwa na eneo karibu ekari mbili huko Bagamoyo, ila hakutaka kujenga huko sababu hati ya nyumba yake ingesoma Pwani na yeye anataka isome Dar

Sasa nimemtolea mfano huyo sababu ni maarufu lakini kiuhalisia hizi ndio akili za vijana wengi walioko kwenye hili jiji, wapo wengi sana ninaowafahamu ambao nao wana mawazo kama haya ya kutaka kuonekana wanaishi Dar tu na si sehemu nyingine, sasa tukumbuke idadi ya watu Dar inazidi kuongezeka siku hadi siku ila ukubwa wa mkoa hauongezeki

Kwa mtazamo wangu naona suluhisho pekee ni kuunganisha hii mikoa miwili Pwani yote nayo iitwe Dar, kuhusu wilaya kuwa nyingi sioni kama ni tatizo maana hata mkoa wa Tanga una wilaya nyingi kulinganisha na idadi ya wakazi wake so sioni kama ni tatizo kufanya hivyo hata kwa Dar, ambao ndio mkoa wenye idadi kubwa ya wakazi na kama wakiona utakuwa na wilaya nyingi basi wanaweza waka merge baadhi ya wilaya

Sasa hivi miji inakuwa kuelekea Bagamoyo, Kisarawe, Chalinze na Mkuranga kwa maana kwamba watu wameanza kuchangamkia ardhi huko na wengine wameanza kujenga, lakini ukuaji wake bado hauna kasi kulinganisha na idadi ya watu wanaohamia Dar kila siku, hakuna haja ya kuwa na mkoa specific unaoitwa Pwani wakati hata Dar, Tanga, Lindi na Mtwara nayo ni mikoa ya Pwani

Hapa simaanishi miji ikuwe makazi ya watu tu bali hata huduma za kijamii kama ni ofisi, masoko, shule, hospitali, hoteli, malls, bars, restaurants na huduma nyinginezo, lakini hizo asilimia kubwa hufuata makazi ya watu mtu hawezi kufungua tu biashara yake sehemu ambayo hana uhakika wa wateja wa kutosha, kwahiyo ni lazima watu waanze kwanza kuhamia ndipo huduma zitafuata, sasa kwa akili hizi za watu kutaka kuonekana wanaishi Dar tusitegemee Pwani itakuwa haraka

Kama ni ushamba wa bahari mbona hata Bagamoyo na Mkuranga bahari ipo ila bado kuna mapori, nashangaa baadhi ya watu wanataka mikoa izidi kugawanywa wakati hii iliyopo tu maendeleo yametushinda, haya ya kusema eti kawilaya kakishakuwa na tuhuduma fulani twa kijamii hata kama ni tubovu basi kanafaa kuwa mkoa unaojitegemea sioni kama yanasaidia

Kuna mahali nilisoma eti na wakazi wa Masasi nao wanataka hiyo wilaya iwe mkoa eti kisa tu biashara ya korosho yani kuna mambo yanachekesha kwa kweli, huo mkoa wa Mtwara tu bado hamjamalizana nao mnataka muanzishe mkoa wa Masasi tena, halafu hata kijiografia Mtwara siyo mkoa mkubwa kihivyo wa kuhitaji kugawanywa kuna mikoa mikubwa kama Morogoro, Tabora, Lindi nk ambayo ndio inastahili kugawanywa

Hata hivyo hii gawanya gawanya ya mikoa na wilaya inazidi kuongeza idadi ya makabila tu maana nimekuja kugundua hii nchi ina makabila zaidi ya haya tunayoyajua, mengine unakuta ni mtu tu na mkewe na wanaye walihamia pori fulani wakakuta hapana watu wakaanzisha kijiji na kikabila chao hatimaye kikakuwa na kupata watu basi nao wanataka watambulike, mara makabila mengine unasikia eti ni muunganiko wa kabila fulani na kabila fulani sasa hayo yote ya nini ikiwa vitu muhimu kama maji, umeme, afya, elimu, uchumi na teknolojia vinatushinda na ndio maana Nyerere alipiga marufuku mambo ya kuendekeza makabila

Kwahiyo maoni yangu ni kwamba badala ya kuendelea kugawanya mikoa tuangalie kama kuna mikoa ambayo inaweza kuunganishwa iunganishwe, na kwa sasa nilikuwa napendekeza tuanze na Dar na Pwani tubaki na mikoa 30 tu tupambane kuiendeleza kwanza hiyo, na siyo kuwa na mikoa mingi ambayo imejaa mapori tu na huduma mbovu za kijamii pamoja na maendeleo duni
Wazo zuri. Muhimu serikali kabla ya kuunganisha iweke huduma za msingi kama barabara, shule,masoko,hospital, vituo vya mabasi, daladala, huduma za polisi karibu nk

Viwanja muhimu vipimwe, at least vianzie 30 x 20. Mitaa ta kueleweka.
 
Wazo lako limekuja wakati mwafaka sana hata mm nilikuwaga nawaza hivihivo ingawa kuna baadhi ya wilaya ama kata zipelekwe mikoa ya jirani kwa mfano baadhi ya kata za mkuranga ziende mkoa wa lindi na baadhi za kata za wilaya ya bagamoyo ziende tanga chalinze ziende morogoro na wilaya nzima ya Mafia iende lindi au ipimwe urefu wa mzunguko wa kilomita sitini ndio iwe mpaka wa mkoa wa Daresalaam
We kilaza kweli kweli. Kata za Mkuranga ziende Lindi, wakati kutoka Mkuranga unapita wilaya za Kibiti na Rufiji ndio ufike Lind.😀😀😀
Mafia zamani huko ilikua mkoa wa Mtwara, walipoigawa Mtwara kutoa Lindi na Mzizima kutoa Dar basi automatically Mafia ikahamia Pwani.
 
Mwaka 1974 Serikali ya Tanzania ilianzisha mikoa mitatu kama ifuatavyo :-
1. Iligawa mkoa wa Pwani na kuzaliwa mkoa wa Dar es Salaam.
2. Iligawa mkoa wa Mtwara na kuzaliwa mkoa wa Lindi.
3. Ilimega Wilaya ya Mpanda kutoka mkoa wa Tabora na kumega Wilaya ya Sumbawanga kutoka mkoa wa Mbeya na kuunda mkoa wa Rukwa.

Hivyo basi, haiwezekani Tena Dar kuunganishwa na Pwani isipokuwa kwa kuwa mkoa wa Dar umejaa Cha kufanya ni kumega baadhi ya maeneo ya Pwani na kuyaingiza katika mkoa wa Dar. Nadhani nimeelewrka.
 
Heri ya mwaka mpya wakuu

Hivi kwanini serikali isiunganishe mikoa ya Dar na Pwani kisha huo mkoa uitwe Dar na tubaki na mikoa 30 tu, hakuna haja ya kuwa na mikoa mingi huku maendeleo yakiwa ni madogo na idadi ya watu ikilundikana kwenye vimiji vichache tu, kusema kwamba tutamaliza mapori na kuharibu mazingira kwa vizazi vijavyo ni upotoshaji kwa sababu Tanzania bado hakuna population ya kumaliza mapori yote tuliyonayo

Ni ajabu kwamba mkoa mdogo kijiografia kuliko yote nchini ndio mkoa mkubwa kidemografia kuliko yote nchini, ukiuliza sababu hakuna sababu ya maana utapewa zaidi ya watu wengi hasa vijana, kutaka waonekane wanaishi Dar hata kama maisha yao hayaeleweki na huko mikoani wameona fursa

Juzi nilikuwa nasikiliza interview ya Mwijaku alipokuwa anawajibu watu wanaosema kwamba kajenga ghorofa lake kwenye kaeneo kadogo, akasema alikuwa na eneo karibu ekari mbili huko Bagamoyo, ila hakutaka kujenga huko sababu hati ya nyumba yake ingesoma Pwani na yeye anataka isome Dar

Sasa nimemtolea mfano huyo sababu ni maarufu lakini kiuhalisia hizi ndio akili za vijana wengi walioko kwenye hili jiji, wapo wengi sana ninaowafahamu ambao nao wana mawazo kama haya ya kutaka kuonekana wanaishi Dar tu na si sehemu nyingine, sasa tukumbuke idadi ya watu Dar inazidi kuongezeka siku hadi siku ila ukubwa wa mkoa hauongezeki

Kwa mtazamo wangu naona suluhisho pekee ni kuunganisha hii mikoa miwili Pwani yote nayo iitwe Dar, kuhusu wilaya kuwa nyingi sioni kama ni tatizo maana hata mkoa wa Tanga una wilaya nyingi kulinganisha na idadi ya wakazi wake so sioni kama ni tatizo kufanya hivyo hata kwa Dar, ambao ndio mkoa wenye idadi kubwa ya wakazi na kama wakiona utakuwa na wilaya nyingi basi wanaweza waka merge baadhi ya wilaya

Sasa hivi miji inakuwa kuelekea Bagamoyo, Kisarawe, Chalinze na Mkuranga kwa maana kwamba watu wameanza kuchangamkia ardhi huko na wengine wameanza kujenga, lakini ukuaji wake bado hauna kasi kulinganisha na idadi ya watu wanaohamia Dar kila siku, hakuna haja ya kuwa na mkoa specific unaoitwa Pwani wakati hata Dar, Tanga, Lindi na Mtwara nayo ni mikoa ya Pwani

Hapa simaanishi miji ikuwe makazi ya watu tu bali hata huduma za kijamii kama ni ofisi, masoko, shule, hospitali, hoteli, malls, bars, restaurants na huduma nyinginezo, lakini hizo asilimia kubwa hufuata makazi ya watu mtu hawezi kufungua tu biashara yake sehemu ambayo hana uhakika wa wateja wa kutosha, kwahiyo ni lazima watu waanze kwanza kuhamia ndipo huduma zitafuata, sasa kwa akili hizi za watu kutaka kuonekana wanaishi Dar tusitegemee Pwani itakuwa haraka

Kama ni ushamba wa bahari mbona hata Bagamoyo na Mkuranga bahari ipo ila bado kuna mapori, nashangaa baadhi ya watu wanataka mikoa izidi kugawanywa wakati hii iliyopo tu maendeleo yametushinda, haya ya kusema eti kawilaya kakishakuwa na tuhuduma fulani twa kijamii hata kama ni tubovu basi kanafaa kuwa mkoa unaojitegemea sioni kama yanasaidia

Kuna mahali nilisoma eti na wakazi wa Masasi nao wanataka hiyo wilaya iwe mkoa eti kisa tu biashara ya korosho yani kuna mambo yanachekesha kwa kweli, huo mkoa wa Mtwara tu bado hamjamalizana nao mnataka muanzishe mkoa wa Masasi tena, halafu hata kijiografia Mtwara siyo mkoa mkubwa kihivyo wa kuhitaji kugawanywa kuna mikoa mikubwa kama Morogoro, Tabora, Lindi nk ambayo ndio inastahili kugawanywa

Hata hivyo hii gawanya gawanya ya mikoa na wilaya inazidi kuongeza idadi ya makabila tu maana nimekuja kugundua hii nchi ina makabila zaidi ya haya tunayoyajua, mengine unakuta ni mtu tu na mkewe na wanaye walihamia pori fulani wakakuta hapana watu wakaanzisha kijiji na kikabila chao hatimaye kikakuwa na kupata watu basi nao wanataka watambulike, mara makabila mengine unasikia eti ni muunganiko wa kabila fulani na kabila fulani sasa hayo yote ya nini ikiwa vitu muhimu kama maji, umeme, afya, elimu, uchumi na teknolojia vinatushinda na ndio maana Nyerere alipiga marufuku mambo ya kuendekeza makabila

Kwahiyo maoni yangu ni kwamba badala ya kuendelea kugawanya mikoa tuangalie kama kuna mikoa ambayo inaweza kuunganishwa iunganishwe, na kwa sasa nilikuwa napendekeza tuanze na Dar na Pwani tubaki na mikoa 30 tu tupambane kuiendeleza kwanza hiyo, na siyo kuwa na mikoa mingi ambayo imejaa mapori tu na huduma mbovu za kijamii pamoja na maendeleo duni
Nakubaliana na mtoa mada kwa 100%
 
Mbaya zaidi watu wa Dar wanaoenda kujenga huko na vikampuni uchwara vya viwanja vinakata viwanja vya 400sqm. Mwisho sehemu ambazo zingekuwa suburbs nzuri za Dar zinageuka kuwa slums flani hivi.
Mkuu kwa hili nami nakubaliana na wewe. Wizara ya ardhi itazame hii biashara ya viwanja vidogo vidogo kama visheti katika mkoa wa pwani hasa mkuranga, nk. Mkoa wa pwani utakuja kuwa kama mkoa wa mapokezi ya wakimbizi kutoka kwenye inchi zenye vita kwa mbanano utakaotokea siku za usoni. Serikali inafanya kosa lilelile la ujenzi holela alafu wanakuja na plan ya urasimishaji wa makazi.

Ukitaka kushangaa nchi hii uwe kwenye skyscrapers au usafiri wa angani alafu utazame chini utashangaa makazi ya watu yalivyokaa hovyo cha kushangaza serikali haina plani za miaka 70 au 100 ijayo.

Kama kuna watu wa ardhi humu waseme jambo kuhusu matumizi ya ardhi ya inchi hii.

Sent from my SM-A025F using JamiiForums mobile app
 
Shida sio kuunganishwa kuwa mkoa. Mmoja wa jina, muhimu ni miundo mbinu, hakuna shida kuishi kisemvule kama tu kisemvule huduma zote muhimu zinapatikana, usafiri wa kuja huku mjini uwepo.

Changamoto ni miundo mbinu, waweke vitu sawa, mkuranga tu hapo kuna sehemu hakuna umeme, barabara mboovu kinooma, unadhani mtu anashawishika vipi kwemda kujificha huko.
Wakati nahamia kigamboni miaka ya 90, 2000 mwanzoni hakuna ndugu alikuwa anashawishika kuja kununua huku, ila baada ya miaka kwenda huduma muhimu kusogea, sasa pamepanda saana thamani kuna viwanja huna milioni 50 unaambiwa hupati,
serikali ijiongeze, kuna vitu vinawavutia na kuhamasisha watu kuhamia sehemu na kuishi.
 
We unaongelea watu kulundikana dar..
Watu hawasogei nje ya dar sio kwa sababu eti wanapapenda dar

Hiyo vikindu ni kama iko dar maana hakuna umbali wa kutisha.. watu hawasogei pwan
Sababu jografia ya pwani ilivyo

Hv unawezaje kuishi vikindu kisha ukihitaji huduma za kiserikali ngaz ya mkoa uende kibaha.. yaan unavuka mkoa mwingine kufata huduma za serikali mkoan kwako

Aligawa mkoa wa pwan ana akili za kiisrael kuigawa palestina kati kwa kati

Wanaotoka west bank wawe na pasport wakitaka kwenda south palestina
 
Mkuu wazo lako ni zuri lakini huoni kuunganisha mkoa wa Dsm na Pwani litakuwa ni eneo kubwa sana kiutawala?

Kwanza ukiuchukulia tu mkoa wa Pwani ulivyokaa tenge kijiografia (Kibaha, Chalinze, Bagamoyo, Kisarawe, Mkuranga, Kibiti, Rufiji na Mafia).

Cha muhimu sana ni kuboresha tu miundo mbinu kwa mkoa mzima wa Pwani, watu watasogea tu wenyewe.

Mkuranga kabla ya kuwa wilaya yote hiyo ilikuwa ni wilaya ya Kisarawe, lakini kwasasa inaikimbiza Kisarawe kutokana na kufunguka kwa barabara (Barabara kuu) iliyopelekea mwingiliano mkubwa wa watu.

Kisarawe imeishia kuendelea kwa upande wa Kiluvya pekee.
Sambamba na Kibaha na Chalinze.
Nafikiri mchawi ni miundo mbinu tu.
 
Back
Top Bottom