Serikali iweke wazi orodha ya watumishi wanaostahili kupanda vyeo mwaka 2021

Serikali iweke wazi orodha ya watumishi wanaostahili kupanda vyeo mwaka 2021

Mimi nawasubiria tu wasinipandishe, halafu wataona nitakavyo wazingua. Kila siku asubuhi nikifika kazini, naomba ruhusa kwenda kufuatilia suala langu la kupandishwa daraja. Mpaka kieleweke.

Kuna viongozi vilaza wengi sana serikalini! Naamini hata Prof Assad alikuwa sahihi kwa 100%! Wanasumbua wafanyakazi kupeleka opras za tangu 2015! Kiasi cha kujiuliza kwa muda wote huo walikuwa wapi? Na hizo opras zilizokuwa zinakusanywa makazini na kupelekewa hao vilaza wa kwenye Halmashauri zetu, walizipeleka wapi?

Hopeless kabisa!!
Oprah ukishaajaza huwa wanazitupia hapo chini hata hawashugulikia Chochote zikiihitajika tena wanakwambia upeleke , tena ili hali wao ndo wanazo halmashauri kuna kuna mafisa mtumishi ni vilaza sana
 
Mbona ili Jambo liko wazi ,labda katika Halmshauri yako Tu ,vyama vya wafanyakazi viko macho katika ili ,vinatembelea kila wiki Kwa maafsa Utumishi kuona zoezi linaendaje
Kabsaa mfano CWT Wana orodha ya majina kabsaa ya watumishi watakaopanda
 
Wakati mwengine kupanda cheo ni bahati tu.
Kunawatumishi nawafahamu wasiopungua watatu wanatumikia cheo chao cha sasa tangu January 2012.
Wazembe, mimi nikiwa chuo, kuna jamaa wao wanafundisha cha kushangaza nikapanda daraja mimi baada ya miaka minne, wao wakaachwa ingawa walinitangulia kuajiriwa. Huwezi Amin wale jamaa walipandishwa madaja Wizarani huko huko waligoma kufundisha wakaenda kueleza shida zao. Mwezi uliofuata wakapanda. Hii nchi usipojihanagikia mwenyewe unakufa masikini
 
Kiukweli hoja yako ina mashiko Sana. Kuna idara ya afya hapa sengerema imeacha kuwaweka kwenye orodha zaid ya watumishi 50 wa kada ya afya kupanda daraja mwaka huu. Kiukweli nimefuatilia nikaona mwenye tatizo ni katibu wa afya mwenye jukumu la kuchambua hayo majina. Ikitokea ana chuki na mtumishi yeyote lazima kadhia hiyo uipitie.
 
Kiukweli hoja yako ina mashiko Sana. Kuna idara ya afya hapa sengerema imeacha kuwaweka kwenye orodha zaid ya watumishi 50 wa kada ya afya kupanda daraja mwaka huu. Kiukweli nimefuatilia nikaona mwenye tatizo ni katibu wa afya mwenye jukumu la kuchambua hayo majina. Ikitokea ana chuki na mtumishi yeyote lazima kadhia hiyo uipitie.
Hii nchi ngumu sana ndugu yangu. Hata hili nililoshauri walipaswa wao wenyewe wawe wameshalifanya. Kwa sasa wanasubiri malalamiko yaanze ndio wachukue hatua badala ya kuwa na mikakati ya kuzuia mambo kama haya yasotokee

Yaani wako reactive badala ya kuwa proactive.
 
tatizo kubwa la watumishi wa umaa wanapigana "PINI" wao kwa wao, chuki,wivu, majungu na fitina kibao, mnaharibiana sana, hawapendani wao kwa wao, wanachongena ubenya sana!!
sasa mbaya zaidi ukikuta boss naye chaumbeya basi hapo huna chako utabaki kula vumbi labda itokee miujiza ya Mungu.
na katika hili viongozi kuanzia Mhe. waziri, naibu waziri, katibu mkuu na watendaji wote wa wizara ya Utumishi wa Umma wawe makini sana tena sana,
kuna uonevu mkubwa unao endelea ndani kwa ndani, , kuna baadhi yabwatumishinwamepigwa PINI za maksudi tu ili mtu asisogee mbele lkn ukimchunguza mtumishi huge utakuta ni mchapa kazi na muadilifu lkn zengwe limeundwa IPO kumpiga PINI asipande.
chunguzeni tatueni kero haswa kwa wale wasio kuwa na mtu wa kuwasaidia yaani godfather, sioni kama tabia ya kuwa na godfather ni jambo la kuachiliwa liendelee ktk mifumo yetu, hapa! watu wato watumishi wote watendewe haki sawa. kamwe kusiwe na matabaka ktk utumishi wa umma, kwa kufanya hivyo mtajenga imani kwa wananchi.
hakikisheni anayestahili anapewa haki yake bila kuwekewe pini au zengwe.
Upatikanaji wa haki za wananchi unaanzia kwa watumishi wao kwa wao kutendeana Haki ndipo na sisi wananchi tutapata haki, kinyume chake hakuna haki.
Rais wetu Mpendwa mama Samia anataka kuona Haki ikitamalaki, hataki kuona UONEVU/UNYANYASAJI na upendeleo au kujuana.
acheni kutoa kadi nyekudu ovyo ovya, waleeni watumishi walio chini yenu badala ya kuwagawa, wajengeeni uwezo badala ya kuwaharibu.
wapo viongozi wenye roho mbaya sana ambao wanapenda kuwaharibia kazi walio chini yao kwa maksudi tu au chuki binafsi, mizengwe mizengwe mizengwe na chuki
uonevu, uonevu, uonevu ndicho huwa kinatendaka ndani kwa ndani, viongozi wana waonea sana watumishi walio chini yao, kiongozi anaweza kuamua tu kwa hila kumharibia aliye chini yake hiyo ndio tabia iliyo kithiri ndani kwa ndani na bahati mbaya hakuna wa kuwatetea.
Waziri Mchengelwa safisha tabia hiyo ya uonevu mkubwa iliyo kithiri ndani ya utumishi wa umma.
Huku maofisini ukiwa mtu wa kuhoji vitu, ukiwa mtu wa kutaka haki utaitwa mkorofi na hutapewa kazi za za michongo ya hela hasa ukiwa na boss asiyejiamini
 
Mbona ili Jambo liko wazi ,labda katika Halmshauri yako Tu ,vyama vya wafanyakazi viko macho katika ili ,vinatembelea kila wiki Kwa maafsa Utumishi kuona zoezi linaendaje
Hivyo vyama vinasubiri hadi utemwe kwenye orodha uwafate ndio wanaanza kushughulikia usijidanganye kuwa wanafuatilia kila kitu. Mimi yalinikuta
 
Huku maofisini ukiwa mtu wa kuhoji vitu, ukiwa mtu wa kutaka haki utaitwa mkorofi na hutapewa kazi za za michongo ya hela hasa ukiwa na boss asiyejiamini
Umeongea ukweli mtupu. Yaani utachukiwa na kuonekana unajifanya mjuaji.
 
Huku maofisini ukiwa mtu wa kuhoji vitu, ukiwa mtu wa kutaka haki utaitwa mkorofi na hutapewa kazi za za michongo ya hela hasa ukiwa na boss asiyejiamini
True umesema yote wao hawataki watu wa Kuwa challenge
 
Mimi nawasubiria tu wasinipandishe, halafu wataona nitakavyo wazingua. Kila siku asubuhi nikifika kazini, naomba ruhusa kwenda kufuatilia suala langu la kupandishwa daraja. Mpaka kieleweke.

Kuna viongozi vilaza wengi sana serikalini! Naamini hata Prof Assad alikuwa sahihi kwa 100%! Wanasumbua wafanyakazi kupeleka opras za tangu 2015! Kiasi cha kujiuliza kwa muda wote huo walikuwa wapi? Na hizo opras zilizokuwa zinakusanywa makazini na kupelekewa hao vilaza wa kwenye Halmashauri zetu, walizipeleka wapi?

Hopeless kabisa!!
Aisee hili la opras Ni Bomu .Tumeandika opras Hadi tukataka kugemea ,,
 
Eti wameshaanza tena mambo ya Ophras ili kupata sababu ya kuwapora baadhi ya watu haki zao za kupandishwa madaraja. Yaani mama anaturudisha kulekule kwa mwendazake. Akitunyima haki zetu tutamchuka kwelikweli. Mambo ya Ophras yanatoka wapi tena. Mtu mwenye haki yake apewe. Mwambieni kuwa akituzingua tutamzingua.
Hakuna Haki bila Wajibu dogo. Kama unataka Daraja, JAZA OPRAS.
 
Maswala ya kitumishi ni siri.

Kama kuna mtumishi ataachwa ipo nafasi ya malalamiko.

Na kila mtumishi anajua kama anastahili kupanda ama la.
 
Eti wameshaanza tena mambo ya Ophras ili kupata sababu ya kuwapora baadhi ya watu haki zao za kupandishwa madaraja. Yaani mama anaturudisha kulekule kwa mwendazake. Akitunyima haki zetu tutamchuka kwelikweli. Mambo ya Ophras yanatoka wapi tena. Mtu mwenye haki yake apewe. Mwambieni kuwa akituzingua tutamzingua.

Ni taratibu za kitumishi miaka yote, wala hakuanza mwendazake.
Kama hukuwa na sifa njema kwenye opras usimlaumu mama.
 
Hizo opras mbona kila mwaka watumishi wanajaza? Sasa nini ambacho wanakitaka tena?Ukiona hivyo, ujue visngizio ndio vinaanza kama ilivyokuwa wakati wa Mwendazake alipokuja na kisingizio cha uhakika kabla ya kupandisha mishahara.

CCM ni shida!

Hakuna kisingizo

Opras ipo miaka yote
 
Mimi nawasubiria tu wasinipandishe, halafu wataona nitakavyo wazingua. Kila siku asubuhi nikifika kazini, naomba ruhusa kwenda kufuatilia suala langu la kupandishwa daraja. Mpaka kieleweke.

Kuna viongozi vilaza wengi sana serikalini! Naamini hata Prof Assad alikuwa sahihi kwa 100%! Wanasumbua wafanyakazi kupeleka opras za tangu 2015! Kiasi cha kujiuliza kwa muda wote huo walikuwa wapi? Na hizo opras zilizokuwa zinakusanywa makazini na kupelekewa hao vilaza wa kwenye Halmashauri zetu, walizipeleka wapi?

Hopeless kabisa!!
I strongly support you. Kuna takataka nyingi serikalini kitengo chs HR
 
Back
Top Bottom