Serikali: Januari 31, 2025 ni mwisho wa kutumia mkaa na kuni

Serikali: Januari 31, 2025 ni mwisho wa kutumia mkaa na kuni

Deadline hiyo imetangazwa na Waziri wa Mazingira Suleimani Jafo.

Baada ya January 31, 2024 taasisi zote za Umma na Binafsi ni marufuku kupikia kwa kutumia mkaa na kuni.

Aidha Serikali imesema inataka kufikia 2030 Asilimia 80% ya Watanzania wote wawe wanatumia Nishati safi ya kupikia.

====

"Taasisi zote za Umma na Binafsi zinazopika chakula cha zaidi ya watu 100 itakapofika Januari 31,2024 taasisi hizo zinatakiwa kusititisha matumizi ya kuni na mkaa kwa ajili ya kupikia, lakini taasisi zile ambazo zina watu zaidi ya 300 itakapofika Januari 31, 2025 zisitishe matumizi ya kuni na mkaa watumie nishati mbadala" - Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).
Mmmmmhhh ngoja tuone
 
Hizi ni hadithi za alinacha! Labda wakazi wa mijini wataacha kutumia mkaa watumie gesi, na hiyo gesi bei ishuke. Huko ndani vijijini umeme wenyewe haujafika gesi itafikaje? Hizi siasa ni hesabu za propability
 
Nikajua fursa hii hapa niagize mzigo wa jiko za gasi nije kuwauzia watanzania 😁
SIo mbaya jamani karibuni Instagram @dollrubiidecors na @dollrubiivyombo
 
Mwaka 1994 ccm walisema ikifika mwaka 2000 tatizo la maji litakuwa ni historia nchini.
 
Mwaka 1994 ccm walisema ikifika mwaka 2000 tatizo la maji litakuwa ni historia nchini.
 
Kwahivyo ule ubwabwa wenye ukoko wa juu wa mkaa tutausikia kwenye simulizi tu?

Na vipi kuhusu BBQ? tutachomaje nyama za mbuzi ili kufurahi na wageni wetu nyumbani?

Serikali iache ukatili kwa raia wake
Soma uzi vizuri boss. Ni taasis za umma
 
Huwezi zuia matumizi ya kuni na mkaa pasipo ondoa kodi kwenye gas
 
Hizi ni hadithi za alinacha! Labda wakazi wa mijini wataacha kutumia mkaa watumie gesi, na hiyo gesi bei ishuke. Huko ndani vijijini umeme wenyewe haujafika gesi itafikaje? Hizi siasa ni hesabu za propability
Hivi mnasoma uzi kweli au mnaishia kusoma vichwa vya habari tuu
 
hahahhaha, majibu rahisi kwa wengine Tanzania huwa yanakuwa magumu sana.

Easy, hakikisha bei ya gas 50kg inauzwa 20k na 30Kg inauzwa 10k, hakikisha supply ya gas ipo ya kutosha kila mahala, halafu baada ya 6month fanya sensa ya watumiaji wa mkaa.
 
Deadline hiyo imetangazwa na Waziri wa Mazingira Suleimani Jafo.

Baada ya January 31, 2024 taasisi zote za Umma na Binafsi ni marufuku kupikia kwa kutumia mkaa na kuni.

Aidha Serikali imesema inataka kufikia 2030 Asilimia 80% ya Watanzania wote wawe wanatumia Nishati safi ya kupikia.

====

"Taasisi zote za Umma na Binafsi zinazopika chakula cha zaidi ya watu 100 itakapofika Januari 31,2024 taasisi hizo zinatakiwa kusititisha matumizi ya kuni na mkaa kwa ajili ya kupikia, lakini taasisi zile ambazo zina watu zaidi ya 300 itakapofika Januari 31, 2025 zisitishe matumizi ya kuni na mkaa watumie nishati mbadala" - Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).
hasa mashule ni wakati sasa zianze kufundisha somo la Agriculture huku wakiwa na mitamba ya kuzalisha biogas
 
Deadline hiyo imetangazwa na Waziri wa Mazingira Suleimani Jafo.

Baada ya January 31, 2024 taasisi zote za Umma na Binafsi ni marufuku kupikia kwa kutumia mkaa na kuni.

Aidha Serikali imesema inataka kufikia 2030 Asilimia 80% ya Watanzania wote wawe wanatumia Nishati safi ya kupikia.

====

"Taasisi zote za Umma na Binafsi zinazopika chakula cha zaidi ya watu 100 itakapofika Januari 31,2024 taasisi hizo zinatakiwa kusititisha matumizi ya kuni na mkaa kwa ajili ya kupikia, lakini taasisi zile ambazo zina watu zaidi ya 300 itakapofika Januari 31, 2025 zisitishe matumizi ya kuni na mkaa watumie nishati mbadala" - Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).
Dadeki wanapooza CAG reports na wanajua Mei mosi inakuja na hawana hata buku la kuwaongeza watumishi
 
Anatokea mtu mmoja kutoka kisarawe anatutangazia eti kutumia kuni na mkaa sasa basi.

Unawakejeli wananchi masikini ili upate nini hasa?

Maana tayari wewe ni bilionea kwa kuwepo hapo bungeni na kwenye wizara.

Unaudharau kisa umasikini wetu? Hiyo kupata mlo wangu wa siku nashindwa leo unakejeli kuwa nisahau kutumia kuni?

Muwe mnaona aibu basi hata kama ni kuuza sura.

Screenshot_20230412-162942_Instagram.jpg
 
Labda watashusha bei ya Gas na umeme iwe sawa na sifuri ndipo wasitishe matumizi vinginevyo badamu batamwagika.
 
Labda watashusha bei ya Gas na umeme iwe sawa na sifuri ndipo wasitishe matumizi vinginevyo badamu batamwagika
Kuna familia nyingi sana vijijini hata uwezo wa kununua hilo jiko la gesi hawana
 
Anatokea mtu mmoja kutoka kisarawe anatutangazia eti kutumia kuni na mkaa sasa basi.

Unawakejeli wananchi masikini ili upate nini hasa ?
Maana tayari wewe ni billion bilionea kwa kuwepo hapo bungeni na kwenye wizara.

Unaudharau kisa umasikini wetu? Hiyo kupata mlo wangu wa siku nashindwa leo unakejeli kuwa nisahau kutumia kuni?

Muonage aibu basi hata kama ni kuuza sura.View attachment 2585444
Jafo ni tapeli kama matapeli wengine

USSR

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom