Serikali kuajiri Zaidi ya walimu 35,000

Mnyakyegi

Member
Joined
Sep 12, 2014
Posts
81
Reaction score
21
Waziri Mkuu Mizengo Kayanza Peter Pinda,amesema serikali imepanga mwaka huu kuajiri walimu zaidi ya 35,000 kwa ajili ya shule za sekondari ili kukabiliana na tatizo la uhaba wa walimu nchini.

Ametoa kauli hiyo Jana (Alhamis) Tarehe 19 February 2015 wakati akizungumza na wakazi wa kata ya Kiwere, mara baada ya kukagua ujenzi wa maabara na kuzindua nyumba nne za walimu kwenye shule ya Sekondari Kiwere, tarafa ya Kalenga wilaya ya Iringa.

Alisema pia walimu hao watasambazwa kulingana na mahitaji ya maeneo husika Lengo ni kuhakikisha kuwa uhaba wa walimu unapungua kutokana na kufahamika kuwa baadhi ya maeneo kuna uhaba mkubwa wa walimu hasa vijijini.

N.B: Ondoeni wazo la kusema ajira hakuna.

Source: Radio One




 
Acha wasiwasi kijana. Unadhani tukiacha kukuajiri mwaka huu na jinsi ulivyopigika mtaani, utatupa kura yako kweli!
Wewe andaa nauli!
 
Ni kweli ajira za walimu wapya zimetokaa?
 
Sehemu yenye uitaji wa walimu ni vijijini so ukipelekwa uko uturie uijenge Tanzania
 

Wewe kweli............ Huoni hats aibu kucoment, ngoja nikuulize ivi katibu mkuu na Waziri mkuu nani mwenye mamlaka, halafu huyo katibu mkuu ulimsikia wewe peke yako?

Pinda amezungumza akiwa katika shule ya sekondari Kiwere navyombo vya habari hususani magazeti ya Leo karibia yote yameandika iyo habari, wewe uyo katibu mkuu alikuwa akizungumzia wapi?

navyombo gani vya habari viliandika au alikwambia peke yako.Ndugu kabla ya kucoment uwe unafikiria sababu umetuonyesha ni jinsi gani ulivyo na uwezo mdogo Wa kufikiri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…