Serikali kuendelea kununua magari ya kifahari 'V8' huku ikitegemea kukusanya tozo ni kukosa uwajibikaji

Nyumisi

JF-Expert Member
Joined
Nov 10, 2010
Posts
13,499
Reaction score
19,292
Kama kichwa cha mada kinavyoeleza hili liko wazi ni kukosa uwajibikaji kwa wananchi.

Kama hali imekuwa ngumu hadi kulazimika kuwakamua wananchi tozo hii ingeonekana pia kwa serikali kubana matumizi yasiyo na tija ikiwemo hii ya maafisa kutumia magari ya anasa ambayo yanatakiwa kugharamiwa na hizi tozo alizokamuliwa mlalahoi huku yeye akishindwa kumudu hata mlo mmoja kwa siku.

Hii ni sawa na kuwasaliti wananchi.​
 
Nchi ya AJABU sana GHARAMA ya kununua KIVUKO (PANTONI) ili kuhudumia Watanzania zaidi ya MILIONI 1 kule KIGAMBONI ni BIL.8
Lakini Serikali inatumia BIL.558 kununua Ma V8 kila Mwaka kwa Sh.BIL.558 ambayo ni sawa na VIVUKO ( PANTON) 70 lakini mpaka Leo KIVUKO ( PANTONI) ni
KIBOVU kila Siku MATENGENEZO lakini SERIKALI haioni UMUHIMU wa Kununua KIVUKO KIPYA
 
Hii inaumiza sana sio siri
 
Ni kweli aisee, kama hali imekuwa mbaya namna hii hadi kukamua tozo pesa zilizohifahiwa benki, basi hii ireflect kwa kupunguza hii anasa. Uvumilivu wa wananchi una mwisho wale jamani
 
U
Kwa hilo watasema serikali haina fedha πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ ila kwenye semina na hafla za kumsifia mama na kumlaki hela zipo. Hao ndio CCM bana!
 
Ni kweli aisee, kama hali imekuwa mbaya namna hii hadi kukamua tozo pesa zilizohifahiwa benki, basi hii ireflect kwa kupunguza hii anasa. Uvumilivu wa wananchi una mwisho wale jamani
Wananchi mnatakiwa mtoke nyuma ya simu sasaπŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ tabia ya kulalamika haitaleta matokeo yeyote chanya. Tena ndo bwana Lameki ataongeza wigo wa tozo hadi mkome kuringa
 
Makes sense
 

Siku hizi Toyota hawana V8, zinazotoka mwaka huu zote ni V6, kwa taarifa yako tu
 
Bora kutawaliwa na mzungu lakini sio ngozi nyeusi
Upo sahihi mkuu, pamoja na kwamba binadamu hatukosi mapungufu lakini wazungu wana utu sana linapokuja swala la kujali hali ya maisha ya watu...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…