Serikali kuilipa Symbion Tsh Billion 356

Ipo siku tunaotukanana humu tutaimba wimbo mmoja! Wajukuu zetu watatu address kama akina Chief Mangungo.

Kama chama chao wenyewe walijimilikisha mali itakuwa rasilimali za umma? Hizi fedha zinazunguka alafu zinarudi kwa walewale waliohodhi na wanaoona hii nchi ni yao wenyewe!

Tuendelee kutafuta ugali, mambo mengine huwezi kupata jibu leo wala kesho. Endeleeni kutukanana hadi siku utapojua ulikuwa unajitukana mwenyewe.
 
Hahahah si mliwahi kusema Kitengo ndio kinafanya vetting mara sijui Rais anatafuta tokea akiwa sekondari na kwamba upinzani hauwezi kupewa nchi sababu tunatumika na mabeberu!!

Mbona tena mnalialia wakati Rais wa CCM kamuachia Rais wa CCM?? bunge limejaa CCM kwanini lisihoji? Baraza la madiwani nchi nzima mnayamiliki nyie kwanini msihoji?

Tuliaminishwa CHADEMA inatuchelewesha sana maendeleo, kivipi Leo mmebaki wenyewe nchi imewashinda?

Msitake Kila kitu kujifichia kwa JPM, deal na matatizo yenu wananchi wanawasubiri 2025
 
Alitubu kwa wananchi... wenzake walipomsikia akitubu walimkasirikia na kumtishia vibaya... akarudi kutubu tena kwao...
Lesson from Ndugai...
Huwezi kutubu toba ya kweli alafu ukatubu kukanusha ukawa salama!
Kweli kabisa !!
 
Alafu hii kulipa CAG ameshauri tulipe haraka sana kuepusha riba zaidi [emoji2960]
Mambo yapo kisheria usipolipa itafika mpka ICC huko au ICSID mshuke ratings za investor confidence.

Ukivunja mkataba kwa mihemko ndio changamoto hiyo. Hata makocha wa Mpira akitimuliwa kisa timu inafungwa sana lazima umlipe tu hakuna namna.

Haya yote yamesababishwa na usiri wa mikataba na huyo JPM alitutoa Open Governance Initiative imesababisha mikataba isiwekwe bungeni kama Sheria ya TEIT inavyotaka.

Then madhara yake yakitokea lawama kwa Mama Samia?? Kwani bungeni si CCM watupu kwanini msipinge huko? Mahakama imejaa makada wa CCM kwanini wasiweke zuio?

Get real
 
Alafu tumpe nani madaraka? Huko upinzani wengi wapo kwenye "line" zao! Labda tuombe watokee wazalendo wengi from within wavuruge hiyo chain.
Line za nani? Mbona walifilisiwa na wengine kumiminiwa risasi wangekua na back up ya mafisadi wa CCM wangeteswa vile?

Nitajie fisadi hata mmoja aliyepo upinzani? Mlisema Mbowe anakula ruzuku CAG ameshadisapprove Hilo same as TAKUKURU waliofanya forensic auditing wakagundua Hana kosa.

Kama mnaona upinzani hawafai wakati wameprove wakiwa bungeni kupinga miswada mibovu na mikataba ya kifisadi basi msilielie hapa kuhusu Samia wakati mnajua mchawi wenu ni CCM.

Tuibiwe mpaka akili zitukae sawa na ikiwezekana mafuta yapande bei liter moja iwe elfu 10!!

Dumb Tanzanians
 
Jamaa mmoja alipata kusema " Teach me the rules I will show you how to break them !! Mambo ni Abrakadabra !! Dunia inaenda mbio sana !! Russia na NATO tunawasubiri mfanye jambo lenu ili tukae sawa !!
 
Alafu tumpe nani madaraka? Huko upinzani wengi wapo kwenye "line" zao! Labda tuombe watokee wazalendo wengi from within wavuruge hiyo chain.
Hata wewe tu, lkn CCM haina uhalali wowote kwa sasa ndie adui namba moja wa watanzania.

Kama uko timamu utaelewa
 
Hii remote jamani haina uchungu na nchi yake,lakini mwisho wa yote wataondoka na sanda tu, sasa tujue kwanini hawa wahuni walikuwa wanampiga vita mwendazake!
 

Ujasiri wa kuvunja mikataba waliyoingia wenzako bila kuwachukulia hatua? Tunaposema madaraka ya rais yapunguzwe na nguvu kuhamia kwenye taasisi hamtaki, maana mnajua ccm haiwezi kuendelea kukaa madarakani kwa mifumo yenye nguvu. Mnataka kumsifia mchafu aliyekuwa anapambana na asiowapenda badala ya wizi.
 
Ni vizuri kuheshimu sheria wakati wote. Ubabe huwa hausaidii siku zote,utasifiwa kwa muda na baadaye utaumia au utawaumiza watu wako.
Kumbuka ubabe wa Nyerere kwa yule mkulima mzungu, gharama zake zilimkuta Magufuli. Mara mbili ndege zetu zilikamatwa.
Hakujifunza tu!! Mambo ya kisheria hayamalizwi kwa ubabe hata kidogo.
 
Alafu tumpe nani madaraka? Huko upinzani wengi wapo kwenye "line" zao! Labda tuombe watokee wazalendo wengi from within wavuruge hiyo chain.
You are very right. Iwe kama Angola. Otherwise tumekwisha.

Baada ya serikali ya awamu ya 6 kuingia fidia zimelipwa haraka haraka kama ugomvi, Symbion, Dowans sijui nani.
 
Hii awamu ya 6 sijui itatufikisha wapi! Mama SSH ana nia njema na kunjufu mno lkn amezungukwa na 'mafisi' hatarae
 
Alafu tumpe nani madaraka? Huko upinzani wengi wapo kwenye "line" zao! Labda tuombe watokee wazalendo wengi from within wavuruge hiyo chain.
Ndio sababu watu wanataka katiba mpya. Itatuongoza namna nzuri ya kupata viongozi na namna nzuri ya kuwatoa wakiboronga. Refer to S/Africa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…