Serikali kuweka siku ya jumamosi kuwa siku ya Usaili ni kuwakosea Haki Wahitimu waumini wa kisabato

Serikali kuweka siku ya jumamosi kuwa siku ya Usaili ni kuwakosea Haki Wahitimu waumini wa kisabato

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017

Serikali kuweka siku ya jumamosi kuwa siku ya Usaili ni kuwakosea HAKI Wahitimu waumini wa kisabato.​


Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli

Sabato Njema. (itikia Njema Sana).

Wahitimu wa kisabato wanasikitika baada ya baadhi Yao kukosa kwenda kwenye Usaili kutokana na siku iliyowekwa kwaajili ya Usaili ni siku ya ibada. Sikukuu ya Mungu wao wanaomuamini.

Ikumbukwe kuwa Sabato kwa waumini wa kisabato ni Moja ya amri kubwa na kuu wanaamini wameagizwa kuifuata na Mungu wao wakirejelea Torati ya Musa katika Biblia, katika Kutoka 20:8-11

Tunafahamu kuwa serikali huenda ilifanya kwa bahati mbaya kwa kusahaukundi hili la Wasabato. Na hatutaki kuamini kuwa imefanywa makusudi bila kujali au kwa kudharau Wasabato kwa Sababu zozote zile.

Wasabato sio Watu wakujihusisha na mambo ya siasa na kiserikali na hii huenda ni Moja ya sababu ya wao kusahaulika hata kwa mambo muhimu kama ya Ajira.

Mimi Kama Taikon Master, ambaye ni Msabato. Baada ya kupewa taarifa hiyo kwa kweli nilisikitika Sana. Nikaona kuinyamazia inaweza kujirudia na kuwafanya Wananchi wa Kitanzania, wanaoabudu katika dhehebu la Wasabato wanaweza kukosa Haki Yao kwa wakati Mwingine.

Serikali kupitia Wizara husika, ifuatilie Jambo hilo na kulifanyia marekebisho.

Taikon Acha nipumzike sasa.

Kesho tukutane, KANISA LA MWENGE SDA, DAR ES SALAAM.

SABATO NJEMA
 
wameagizwa kuifuata na Mungu wao wakirejelea Torati ya Musa katika Biblia
Samahani,naomba ushahidi kuwa Jumamosi ni siku ya saba na ni siku ya sabato.Jibu ukitumia 'common sense' plus fikra tunduizi.Zingatia neno Jumamosi

Vipi wale wanaobadu Ijumaa, Jumapili,Jumatatu n.k?? Punguza ubinafsi na kujiona ninyi ni so special!
 
Samahani,naomba ushahidi kuwa Jumamosi ni siku ya saba na ni siku ya sabato.Jibu ukitumia 'common sense' plus fikra tunduizi.Zingatia neno Jumamosi

Vipi wale wanaobadu Ijumaa, Jumapili,Jumatatu n.k?? Punguza ubinafsi na kujiona ninyi ni so special!
NJE YA MADA.HYO MADA IMESHAJADILIWA MARA NYNG HUMU JF
 
NJE YA MADA.HYO MADA IMESHAJADILIWA MARA NYNG HUMU JF
Umeelewa maana ya 'common sense' plus fikra tunduizi??
Ukitumia hayo maneno hapo juu unaona Mungu ana majina ya siku au watu na utashi wao??
 
Umeelewa maana ya 'common sense' plus fikra tunduizi??
Ukitumia hayo maneno hapo juu unaona Mungu ana majina ya siku au watu na utashi wao??
Tutumie common sense. Unatumia Gregorian kalenda bila shaka. Siku ya kwanza ni ipi?
Si Jumapili?
 
Samahani,naomba ushahidi kuwa Jumamosi ni siku ya saba na ni siku ya sabato.Jibu ukitumia 'common sense' plus fikra tunduizi.Zingatia neno Jumamosi

Vipi wale wanaobadu Ijumaa, Jumapili,Jumatatu n.k?? Punguza ubinafsi na kujiona ninyi ni so special!
Wanaoabudu Ijumaa, Jumapili, Jumatatu, huwa hawafanyi kazi na shughuli zingine hizo siku? Imani yao inakataza?
 
Samahani,naomba ushahidi kuwa Jumamosi ni siku ya saba na ni siku ya sabato.Jibu ukitumia 'common sense' plus fikra tunduizi.Zingatia neno Jumamosi

Vipi wale wanaobadu Ijumaa, Jumapili,Jumatatu n.k?? Punguza ubinafsi na kujiona ninyi ni so special!

Hilo ni Somo Pana na refu.
Utahitaji uwe na elimu ya msingi ya Jiografia kuhusu Calendar na aina zake.

Pili, itakupasa uwe na elimu ya Historia ya Dunia.


Kuhusu wengine wanaoabudu ijumaa, jumapili au hata jumatatu wao Sheria Zao za Dini kuhusu siku ya ibada zinasemaje?
 
Back
Top Bottom