Serikali: Kwa jiji la Dar es Salaam sasa darasa moja wanakaa Wanafunzi 35 - 40 tofauti na awamu iliyopita ambapo walikaa 70 - 80

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Mkurugenzi wa Jiji la Dar es salaam Jumanne Shauri amesema katika jiji lake kwa sasa darasa moja wanakaa wanafunzi kati ya 35 hadi 40 ndio maximum. Shauri amesema katika awamu iliyopita darasa moja lilichukua kati ya wanafunzi 70 hadi 80.

Shauri amemshukuru sana Rais Samia kwa uwekezaji mkubwa alioufanya kwenye madarasa ambapo Jiji lake sasa linajenga shule 16 mpya zote za ghorofa.

Source: ITV habari

Maendeleo hayana vyama.


 
Kwako nchi ni dar es salaam tu tena kwa miaka zaidi ya arobaini. Tanzania na afrika tuna aina mpya za ukichaa.
 


Dar iyo mzee
 
Sasa hivi ufisadi umehalalishwa tofauti na awamu iliyopita ambapo ufisadi lilikuwa ni jambo la siri🐒🐒🐒
Your browser is not able to display this video.
 
Kwako nchi ni dar es salaam tu tena kwa miaka zaidi ya arobaini. Tanzania na afrika tuna aina mpya za ukichaa.
Karipoti mkurugenzi wa jiji la Dar mkuu, hawezi kuongelea mikoa/miji mingine ambayo haipo kwenye mamlaka yake.
Back to the topic; kwangu mimi issues za madarasa tuweni wakweli, mwenye uthubutu hu sio awamu hi, ni JPM huyu ndio muasisi; changamoto alizozikuta na jinsi alivyo tatua kwa muda mfupi zilikua nyingi.
 
Kuna walimu wapya wameajiriwa?
 
Kwa nini unalinganisha na awamu iliyopita? Samia hakuwa serikalini? Linganisha na awamu ya Kikwete ambayo watoto walikaa chini tangu darasa la kwanza hadi la 7.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…