Serikali lawamani kuruhusu Mkusanyiko wa Maelfu kwenye Kilimanjaro Marathon wakati Taifa linapambana na Virusi vya Korona

Serikali lawamani kuruhusu Mkusanyiko wa Maelfu kwenye Kilimanjaro Marathon wakati Taifa linapambana na Virusi vya Korona

Tatizo moja tulilonalo watanzania, huwa tukiwaza korona tunafikiria mtu mmoja mmoja huwa hatuwazi hatari ya huyo mtu mmoja kwa wengine....
Jifungie wewe sisi tuache tuendelee na maisha yetu. Mlitaka Kili Marathon isifanyike ili nyinyi na mabwana zenu mtoe taarifa kuwa Kili Marathon haikufanyika kwa sababu ya corona.

Imekula kwenu na bado mwezi ujayo corona hutaisikia tena hapa TZ. Endelea kulalamika as if unalipwa kwa kulalamika....!!
 
1.Ukimwi Upo Ila bado watu wanaowana na KUNYANDUWANA.

2.Malaria ipo watu bado hawalali na VYANDARUA.

3.elimu bure(sio ya meko pekee) Ila bado watu ni WAJINGA

4.Barabara za lami zipo Ila bado watu hawana MERCEDEZ BENZ.

5.REA imejitahidi Ila bado watu hawana MWANGA.

6.TB IPO Ila bado watu wanapumuliana kwenye VIDALADALA.

7.CORONA ITAJIBEBA.
 
siajabu muandish wa uzi kwny kampen za lissu alikuwa hakosi tena ktk halaiki ile.huku akijua korona ilikuwepo.

siajab huyuhuyu kwny viwanja vya michezo anajihudhurisha

hv leo serikali ikiruhusu mikusanyiko/mikutano ya kisiasa kama ile ya m4c kwa kipindi hiki cha korona, huyu bwana ataacha kwnda kumsikiliza lema? Awe mkweli.
sijasema tahadhal isichukuliwe ila yeye anasimamia hoja yake kwa mizani sawa.
 
Hivi mpaka leo Kuna watu wanaamin barakoa zinasaidia eeh
Me nawashaur tu ikiwezekana hameni nchi nenden huko wanakoo vaa hizo barakoa na hawana misongamano
Kwa usalama wenu zaidi
Yaan tatizo watu hatuna shukran tunaangalia upinzan tu anayetupony corona ni MUNGU sio hizo barakoa
Nimeona likes za mataga hapo chini kama zote,yaani namaanisha Tanzania hamnazo.
 
Wao wasipoathirika, watabeba virusi na kuja kuambukiza wazee na watoto ambao nao wataenda kuambukiza family members na community zao mitaani.

Ugonjwa una side mbili. Athari kwa mhusika mwenyewe au la basi mhusika kuambukiza wengine
Unataka kuniambia hujawahi kuumwa kichwa,viungo na mafua katika kipindi Cha miaka miwili hii?
 
Mkuu, watu wameamua wenyewe acha wafanye kile kitu wanataka.
 
Hee kwako wewe kufa watu 300 kati 10m ni kawaida tu na acha wafe maada ni idadi ndogo.

Wakati kunawenzio wanatamani asipotee hata mmoja. Hapo ndipo ilipo tofauti.

Hivi unaelewa kwa mfano idadi ya watumishi wa serikali ni asilimia ngapi ya watanzania? Unafaham umuhimu wao.?

Covid sio ugonjwa hatari, umekuwa overated, nimeugua huu ugonjwa mara 2 na sasa nahisi naumwa corona nasubiria tu harufu ikate nianze dose. Mara zote 2 sikunywa dawa yoyote na nimepona. Death rate ni asilimia 3 ya waathirika wote hivo 3% ni ndogo sana.

View attachment 1714198
 
Wewe unazumgumzia nini subiri hutaona chochote huku Dar mbona Uwanja wa Taifa huwa tunaangalia mechi na hakuna tatizo lolote
Na juzi kati Viongozi wetu walikuwa na ziara Jijini Dar na mikutano kadhaa ya mikusanyiko. Hilo nalo ni sahihi?
 
Hilo kusanyiko ni la wapenda ngono na walevi tu.. hakuna wakimbiaji hapo
 
Back
Top Bottom